mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,286
- 6,727
1) Viongozi wa CHADEMA mliuambia umma wa Watanzania Lowasa ni fisadi papa, tukawaelewa na chama chake kikamkata.
2) Viongozi wa CHADEMA, mkaongoza mapinduzi ndani ya Bunge la Katiba kwamba Katiba pendekezwa ya Jaji Warioba inachakachuliwa na CCM mkaunda UKAWA, wananchi tukawaelewa.
3) Viongozi wa UKAWA mkabadilisha muungano wenu ukachukua sura ya Chama cha siasa, wananchi tukawaelewa kwamba hatimaye mnatambua "umoja ni nguvu"
4) Viongozi wa UKAWA mkaingia katika kampeni na kaulimbiu ya "mabadiliko", wananchi wakawaelewa kwa kiasi fulani na ndiyo maana hadi sasa mmefanikiwa kupata idadi kubwa ya wateuliwa (madiwani na wabunge) kuliko chaguzi zote zilizopita.
Lakini Viongozi wa UKAWA sasa wananchi hawaelewi kwani agenda yenu ni kuingia Ikulu kwa gharama ya maisha ya wao hao wananchi waliokuwa wanawaamini.
1) Haingii akilini kuamini kuwa, kura zinachakachuliwa, ili hali karibu mikoa yote inaonesha wananchi hao hao waliowapa nafasi zaidi za kuwawakilisha, bado wana imani na CCM ambayo mlidai wameichoka.
2) Pamoja na mamluki kutoka CCM kuvuja siri za kiofisi, bado wananchi wamekiamini CCM.
3) Mtaji wenu wa nguvu ya Lowasa umebainika uko kwa vijana tu, ambao mnajua jinsi mlivyowalaghai, na ndiyo hao mnaotaka kuwatanguliza mbele wapambane na nguvu ya Dola wakati nyie mkikimbilia nje au mnakula raha majumbani mwenu
Kijana wa Kitanzania, hao viongozi kuingia madarakani kwa damu zenu, kutawaweka katika hali hatarishi ya maisha yenu na familia zinazowategemea. Amini CCM chini ya Dkt Magufuli itawapa mabadiliko bora kuliko mnavyotegemea. Mmemsikia na mmemwona kwenye Kampeni na akiwa mtendaji serikalini.
Wakati wa kudanganywa na viongozi ving'ang'anizi na madaraka ya siasa, sasa semeni HAMDANGANYIKI. Waacheni waandamane na familia zao (zitakazonufaika wakiwa madarakani).
TAFAKARI CHUKUA HATUA
2) Viongozi wa CHADEMA, mkaongoza mapinduzi ndani ya Bunge la Katiba kwamba Katiba pendekezwa ya Jaji Warioba inachakachuliwa na CCM mkaunda UKAWA, wananchi tukawaelewa.
3) Viongozi wa UKAWA mkabadilisha muungano wenu ukachukua sura ya Chama cha siasa, wananchi tukawaelewa kwamba hatimaye mnatambua "umoja ni nguvu"
4) Viongozi wa UKAWA mkaingia katika kampeni na kaulimbiu ya "mabadiliko", wananchi wakawaelewa kwa kiasi fulani na ndiyo maana hadi sasa mmefanikiwa kupata idadi kubwa ya wateuliwa (madiwani na wabunge) kuliko chaguzi zote zilizopita.
Lakini Viongozi wa UKAWA sasa wananchi hawaelewi kwani agenda yenu ni kuingia Ikulu kwa gharama ya maisha ya wao hao wananchi waliokuwa wanawaamini.
1) Haingii akilini kuamini kuwa, kura zinachakachuliwa, ili hali karibu mikoa yote inaonesha wananchi hao hao waliowapa nafasi zaidi za kuwawakilisha, bado wana imani na CCM ambayo mlidai wameichoka.
2) Pamoja na mamluki kutoka CCM kuvuja siri za kiofisi, bado wananchi wamekiamini CCM.
3) Mtaji wenu wa nguvu ya Lowasa umebainika uko kwa vijana tu, ambao mnajua jinsi mlivyowalaghai, na ndiyo hao mnaotaka kuwatanguliza mbele wapambane na nguvu ya Dola wakati nyie mkikimbilia nje au mnakula raha majumbani mwenu
Kijana wa Kitanzania, hao viongozi kuingia madarakani kwa damu zenu, kutawaweka katika hali hatarishi ya maisha yenu na familia zinazowategemea. Amini CCM chini ya Dkt Magufuli itawapa mabadiliko bora kuliko mnavyotegemea. Mmemsikia na mmemwona kwenye Kampeni na akiwa mtendaji serikalini.
Wakati wa kudanganywa na viongozi ving'ang'anizi na madaraka ya siasa, sasa semeni HAMDANGANYIKI. Waacheni waandamane na familia zao (zitakazonufaika wakiwa madarakani).
TAFAKARI CHUKUA HATUA