PreGE2025 CHADEMA Kanda ya Victoria: Viongozi na wanachama waliohama ni makapi tu

PreGE2025 CHADEMA Kanda ya Victoria: Viongozi na wanachama waliohama ni makapi tu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Kanda ya Victoria kimesema kipo imara na hakiwezi kuyumba kwani viongozi na wanachama waliohama hivi karibuni kwao ni kama makapi tu

Katibu wa CHADEMA kanda ya Victoria Zacharia Obadi amesema viongozi hao walikuwa na makosa ya usaliti na kwamba walitakiwa kujieleza kwanini wasifukuzwe kwenye chama ndipo wakaamua kuhama kwenye chama hicho

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Katibu huyo wa chadema kanda ya Victoria ameongeza kuwa viongozi na wanachama waliohama hawana madhara yoyote kwenye chama na kusema chadema haitawavumilia wasaliti

Katika hatua nyingine Obadi amesema wamejipanga kufanya ziara ya viongozi ngazi ya Taifa kwa ajili ya kampeni yao ya "NO REFORM NO ELECTION" ambapo makamu mwenyekiti John Heche na Katibu mkuu John Mnyika watazungumza na wananchi wa mikoa ya kanda ya ziwa.

 
Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Kanda ya Victoria kimesema kipo imara na hakiwezi kuyumba kwani viongozi na wanachama waliohama hivi karibuni kwao ni kama makapi tu

Katibu wa CHADEMA kanda ya Victoria Zacharia Obadi amesema viongozi hao walikuwa na makosa ya usaliti na kwamba walitakiwa kujieleza kwanini wasifukuzwe kwenye chama ndipo wakaamua kuhama kwenye chama hicho

Katibu huyo wa chadema kanda ya Victoria ameongeza kuwa viongozi na wanachama waliohama hawana madhara yoyote kwenye chama na kusema chadema haitawavumilia wasaliti

Katika hatua nyingine Obadi amesema wamejipanga kufanya ziara ya viongozi ngazi ya Taifa kwa ajili ya kampeni yao ya "NO REFORM NO ELECTION" ambapo makamu mwenyekiti John Heche na Katibu mkuu John Mnyika watazungumza na wananchi wa mikoa ya kanda ya ziwa.
View attachment 3324461
Tena ni makapi ya mpunga wa Zanzibaa.
 
Back
Top Bottom