meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,464
- 4,828
Toka mwaka 1992 CHADEMA imekuwa ni chama cha upinzani kinachoendeshwa kitaalamu.
Ni chama kilichoanzishwa na kuendekea kwa muktadha wa kujijenga kimfumo.
Jambo hili limekifanya CHADEMA kuwa chama imara cha upinzani kinachoendelea kukua kimfumo huku kikiwekeza katika future.
Tumeshuhudia chadema ikikua na kuimarika siku hadi siku huku kikumbana na vikwazo vingi sana kutoka katika dola.
CHADEMA imeweza kuruka viunzi vingi kwa kuwa ilijengeka kimfumo na sio kimhemuko.
CHADEMA imesurvive fitina za ccm tofauti na NCCR.
Toka mwaka 2010 CHADEMA chini ya katibu wake mkuu Dr Slaa imejitengeneza na kuweza kufikia level ya chini kabisa ya kisiasa..hapa utaona kuna mitaa na vijiji bimeweza kuchukuliwa na Chadema katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Hii ndio Chadema ninayoifahamu na kuipenda.
Kwa sasa CHADEMA inapita katika wakati mgumu sana ...hili jambo sio la bahati mbaya bali ni sehemu na hatua katika ukuwaji wa chama.
Chadema ilikuwa katika mchakato wa kuendelea kujijenga kama taasisi na imekumbana na sintofahamu au dialemma kadhaa...mojawapo ni suala la katiba mpya.
Katiba mpya iliifanya CHADEMA kuingia ubia na vyama visiovyoaminika au visivyo na malengo yanayofanana nayo.
CHADEMA imeingia ndoa na vyama vyenye mirengo tofauti ili tu iendelee kufahamika na kujijenga...hili sio kosa.
CHADEMA imewahi kupokea makapi ya ccm ili tu kuendelea kujijenga.
Ni ukweli usiopingika kuwa Chadema imeweza kuachana na siasa za ushabiki na kujikita katika ujenzi wa mfumo wa chama kutoka ngazi za chini.
Kwa sasa chadema inakabiliwa na changamoto nyingine au tuseme sintofahamu nyingine.
Mwaka 2012 tulishapata tetesi za EL kujiunga na Chadema,kujisafisha na kuteuliwa kuwa mgombea wa urais kupitia Chadema.tetesi hizi zimeendelea mpaka mwaka huu wa uchaguzi pale tulipoona EL anejaribu kugombea kupitia ccm na kukatwa.
sasa habari iliyoenea mjini ni kuwa baada ya kutoswa basi EL anaweza kujiunga na CDM na kuteuliwa kuwa mgombea wao.
Hii ni changamoto kwa Chadema chama ambacho kimependwa na kuonekana kuwa muhimili wa mabadiliko nchini.
Option zilizopo kwa Chadema ni mbili tu..
1.Kumchukua El na kukubali kubeba laana waliyoianzisha ya Ufisadi au
2.kumkataa EL na kuendelea kujijenga kimfumo.hapa simaanishi wakatae makapi ya ccm yaliyoumizwa na kukatwa kwa EL bali wachukue makapi na kuyaweka pembeni halafu wasimame katika kujenga mfumo wao.
yaani changamoto hii waihandle kama vile El angepitishwa na kuwa mgombea wa ccm lazima kungekuwa na makapi kutoka ccm.
CHADEMA iendelee na safari kama ilivyopanga na isikurupushwe...mapambano ndani ya ccm yawe catalyst tu.
Nawasilisha...!
Ni chama kilichoanzishwa na kuendekea kwa muktadha wa kujijenga kimfumo.
Jambo hili limekifanya CHADEMA kuwa chama imara cha upinzani kinachoendelea kukua kimfumo huku kikiwekeza katika future.
Tumeshuhudia chadema ikikua na kuimarika siku hadi siku huku kikumbana na vikwazo vingi sana kutoka katika dola.
CHADEMA imeweza kuruka viunzi vingi kwa kuwa ilijengeka kimfumo na sio kimhemuko.
CHADEMA imesurvive fitina za ccm tofauti na NCCR.
Toka mwaka 2010 CHADEMA chini ya katibu wake mkuu Dr Slaa imejitengeneza na kuweza kufikia level ya chini kabisa ya kisiasa..hapa utaona kuna mitaa na vijiji bimeweza kuchukuliwa na Chadema katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Hii ndio Chadema ninayoifahamu na kuipenda.
Kwa sasa CHADEMA inapita katika wakati mgumu sana ...hili jambo sio la bahati mbaya bali ni sehemu na hatua katika ukuwaji wa chama.
Chadema ilikuwa katika mchakato wa kuendelea kujijenga kama taasisi na imekumbana na sintofahamu au dialemma kadhaa...mojawapo ni suala la katiba mpya.
Katiba mpya iliifanya CHADEMA kuingia ubia na vyama visiovyoaminika au visivyo na malengo yanayofanana nayo.
CHADEMA imeingia ndoa na vyama vyenye mirengo tofauti ili tu iendelee kufahamika na kujijenga...hili sio kosa.
CHADEMA imewahi kupokea makapi ya ccm ili tu kuendelea kujijenga.
Ni ukweli usiopingika kuwa Chadema imeweza kuachana na siasa za ushabiki na kujikita katika ujenzi wa mfumo wa chama kutoka ngazi za chini.
Kwa sasa chadema inakabiliwa na changamoto nyingine au tuseme sintofahamu nyingine.
Mwaka 2012 tulishapata tetesi za EL kujiunga na Chadema,kujisafisha na kuteuliwa kuwa mgombea wa urais kupitia Chadema.tetesi hizi zimeendelea mpaka mwaka huu wa uchaguzi pale tulipoona EL anejaribu kugombea kupitia ccm na kukatwa.
sasa habari iliyoenea mjini ni kuwa baada ya kutoswa basi EL anaweza kujiunga na CDM na kuteuliwa kuwa mgombea wao.
Hii ni changamoto kwa Chadema chama ambacho kimependwa na kuonekana kuwa muhimili wa mabadiliko nchini.
Option zilizopo kwa Chadema ni mbili tu..
1.Kumchukua El na kukubali kubeba laana waliyoianzisha ya Ufisadi au
2.kumkataa EL na kuendelea kujijenga kimfumo.hapa simaanishi wakatae makapi ya ccm yaliyoumizwa na kukatwa kwa EL bali wachukue makapi na kuyaweka pembeni halafu wasimame katika kujenga mfumo wao.
yaani changamoto hii waihandle kama vile El angepitishwa na kuwa mgombea wa ccm lazima kungekuwa na makapi kutoka ccm.
CHADEMA iendelee na safari kama ilivyopanga na isikurupushwe...mapambano ndani ya ccm yawe catalyst tu.
Nawasilisha...!