CHADEMA inavyoliangamiza Taifa!

CHADEMA inavyoliangamiza Taifa!

MEA-MTWARO

Senior Member
Joined
May 15, 2013
Posts
128
Reaction score
40
Kwa kawaida watu makini hawaongozwi na Ubinafsi katika kujadili masuala mbalimbali muhimu ya kitaifa. Hawasukumwi na Umimi, ukabila, ukanda na Udini katika kutoa michango na maoni katika ujenzi wa Taifa, hali ipo tofauti kwa Waumini wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambao wanajitambulisha kwa Udini,ukabila,ukanda,Umimi na Ubinafsi katika kujadili mambo nyeti ya Kitaifa.

Aidha Watu wanaojipofisha jicho la kulia na kuacha la kushoto kuangalia mambo mabaya tu hawawezi kuitwa 'Great Thinkers' kama wanavyojidanganya Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Mitandao ya Kijamii.

Naam! Ndugu wapendwa, kabla ya kusogeza Mguu mbele, naomba kusema kuwa, ni Ibara ya 18(a)ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo inayonipa haki ya kuandika Makala hii kwani Ibara hiyo inatoa Uhuru wa Mtu kutoa Mawazo na Fikra zake kuhusu Nchi yake

Ndiyo! nimeamua kuandika Makala hii kutokana na maoni na michango mbalimbali iliyotolewa na Waumini wa CHADEMA katika Mtandao wa Jamiiforums ambapo walikuwa wakichangia Makala iliyoandikwa na Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Dk. Khamisi Kigwangalla. Michango na maoni hayo ni Ushahidi tosha kwamba CHADEMA inawahujumu Watanzania na Taifa kwa Ujumla.

Siku ya Alhamisi ya tarehe 30,May 2013, Mbunge wa Jimbo la Nzega,Mkoani Tabora, Dk. Kigwangwalla aliandika Makala katika Mtandao wa Jamiiforums. Katika Makala hiyo Dk. Kigwangalla alieleza Matatizo mbalimbali yanayolikabili Taifa letu huku akipendekeza njia mbadala kuyakabili Matatizo hayo.Kubwa zaidi Dk. Kigwangalla aliwataka Watanzania kubadilika Kifikra huku akisema kuwa,"Uoga wa kubalika ni sumu kwa Wapenda Maendeleo". Ngoja niendelee kumnukuu Mbunge huyo ili kwayo Maoni yake yaweze kulinganishwa na kile kilichochangiwa na 'Wanamagwanda'.

"Napenda kuona Watanzania, Sote kwa pamoja tukibadilika kifikra. Tuanze kuwa Wabunifu zaidi, wenye Uthubutu,Wachapa kazi, Waaminifu, kuweka mbele Uzalendo kwa faida ya wote badala ya Umimi zaidi kwa faida yangu. Napenda kuona Watanzania Wenzangu tukizaliwa Upya leo na kuanza nguvu mpya leo ya kuleta mabadiliko ya kifikra na Kiutendaji. Tuondoke kwenye Umbumbumbu wa kuamini kuwa,kila kitu kitaletwa na Serikali. Tuanze kuamini kuwa, tunaweza kubadilisha maisha yetu kwa kuchukua hatua sahihi katika maisha yetu binafsi na katika jamii yetu. Tuanze kuamini vingine kuwa, tunaweza kuamua kuibalisha Nchi yetu sisi wenyewe na kutoka hapa tulipo leo na kuingia Dunia nyingine kabisa kiuchumi na kijamii".

Bila shaka Mawazo yaliyoandikwa katika Makala hiyo ni ya kupongezwa,kuungwa mkono,kuhamasishwa na kufanfanyiwa kazi kwa Watu wenye Ujenzi wa Fikra kwani Mwandishi wa Makala hiyo ameonekana kuandika kwa hisia kali na hivyo kudhihirisha kuwa, ameguswa na kukerwa na matatizo yanayolikabili Taifa letu. Hongera sana Kigwangalla.

Lakini tazama! hali inakuwa tofauti kwa Wafuasi wa CHADEMA,baada ya kuunga mkono,kuhamasisha na kufanyia kazi mawazo hayo, wametumia Wino wao kubeza na kutweza mawazo hayo kwa kuwa tu yamesemwa na Mtu wa CCM. Yangesemwa na Kiongozi wa CHADEMA yangekuwa lulu. Huu ni Uzandiki wa Fikra unaoweza kuliangamiza Taifa letu kwa Misingi ya Uchama, Ubinafsi na Umimi na kwamba vitendo hivi vya hovyo hufanywa na Wasomi Uchwara na Wanasiasa Makapi wasiolitakia Taifa mema na haya ni matokeo ya kushindwa kujenga hoja na kutumia hoja za nguvu kuyafanya mambo yao yakubalike.

Aidha, ni bora kuwasilisha kwenu baadhi ya michango na maoni ya baadhi ya Wanamtandao huo wa Jamiiforums ambao mara nyingi wanajitambulisha na kujigamba kwa Uchama badala ya Utaifa kama ifuatavyo:

Mchangiaji aliyejitambulisha kwa jina la Steven Robert Masatu amesema "Huwezi kuhubiri Fikra mbadala ilihali wewe upo kwenye fikra mgando. Mkuu toka kwanza huko uliko( CCM)". Evi ni kweli kwa mfano si sahihi kwa mnyonge kuwatetea wanyoge wenzake kwa kuwa tu naye ni Mnyoge? kama hivyo ndivyo basi Mwalimu Nyerere asingeliwatetea Watanzania maana alikuwa Mnyonge, kama si upotoshaji nini?.Ingawa hata hivyo Kigwanga haonekani kuwa na Fikra mgando maana aliyoyanena hapo hunenwa na wachache tu.

Nderingosha kama anavyojitambulisha katika Mtandao huo amesema "Hizi Makala ungekuwa unawaandikia Wabunge wenzako wa CCM maana wao ndio wanatakiwa kubadilika kifikra na siyo Wananchi". Huu ni ukweli au kuwahujumu Watanzania?

Vilevi Meningits amesema kuwa "Badiliko la kwanza ni kuitoa CCM mwaka 2015" huku akifuatiwa na mwenzake anayejitambulisha kwa jina la Verified na kusema kuwa, "Tatizo ni CCM" hawa ndio wasomi wetu wanaoyaangalia mambo kwa jicho moja tena la kushoto. Ewe Mwenyezi epusha janga hili katika Taifa letu.

Hivyo,Wachangiaji hawa wanne ni wachache kati ya Wengi wanaojitambulisha kwa Uchadema katika mtandao huo wa kijamii ambao wanaonekana kukifia chama kuliko Taifa, kupinga 'Constructive Ideas' kwa sababu tu yamesemwa na Mtu wa CCM na kuyaangalia mambo kwa jicho la kushoto huku wakiziba la kulia wasione mazuri. Huku ni kulitafuna Taifa kwa Misingi ya Uchama, Umimi na Ubinafsi.

Nisingependa kumaliza makala hii pasi na kuwashauri viongozi wa CHADEMA na Wafuasi wake kuwa, wawe tayari kulifia Taifa kuliko Chama, Wawaunge mkono viongozi wetu pale wanapokuja na mikakati ya kuljenga Taifa,kuwapa moyo viongozi wetu kwa mawazo yao pale yanapoonekana ni ya tija kuliko kuwabeza, tweza na kuwakatisha tamaa kwani kufanya hivyo kwaweza kupelekea viongozi wetu kujihusisha na malumbano badala ya kusisimamia shughuli za kimaendeleo na hatimaye kulipeleka Taifa kwenye Mdomo wa Mamba. Kwa faida ya nani?

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.

NAMBA 0789357823


 
Huu nao ni utumbo mwingine uliosheheni ukame wa fikra!! Hakuna msafi ndani ya CCM! By the way, bandiko lako hili lina faida gani kwa taifa?
 
Makala murua na yenye tija humu jamvini!


Ongera mkuu kwa kufunguka.
 
Akili za kushikiwa ndivyo zilivyo!!! Mafisadi wa EPA, Richmond , Rada, Kagoda, Meremeta, Mikataba isiyo na maslahi kwa Watanzania wenye sera mbovu kwenye kila kitu na kudidimiza sekta za elimu, afya, usafiri, uchumi, huduma muhimu n.k. Huwaoni unawaona CDM!!!!
 
"Napenda kuona Watanzania, Sote kwa pamoja tukibadilika kifikra. Tuanze kuwa Wabunifu zaidi, wenye Uthubutu,Wachapa kazi, Waaminifu, kuweka mbele Uzalendo kwa faida ya wote badala ya Umimi zaidi kwa faida yangu. Napenda kuona Watanzania Wenzangu tukizaliwa Upya leo na kuanza nguvu mpya leo ya kuleta mabadiliko ya kifikra na Kiutendaji. Tuondoke kwenye Umbumbumbu wa kuamini kuwa,kila kitu kitaletwa na Serikali. Tuanze kuamini kuwa, tunaweza kubadilisha maisha yetu kwa kuchukua hatua sahihi katika maisha yetu binafsi na katika jamii yetu. Tuanze kuamini vingine kuwa, tunaweza kuamua kuibalisha Nchi yetu sisi wenyewe na kutoka hapa tulipo leo na kuingia Dunia nyingine kabisa kiuchumi na kijamii".

Bila shaka Mawazo yaliyoandikwa katika Makala hiyo ni ya kupongezwa,kuungwa mkono,kuhamasishwa na kufanfanyiwa kazi kwa Watu wenye Ujenzi wa Fikra kwani Mwandishi wa Makala hiyo ameonekana kuandika kwa hisia kali na hivyo kudhihirisha kuwa, ameguswa na kukerwa na matatizo yanayolikabili Taifa letu. Hongera sana Kigwangalla.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.

Ninaitwa BAKARI MADAYA (Mwanatunduru).
Ninapatikana simu: 0789357823 au barua pepe madayabakar@hotmail.com

Sitaiomba serikali ininunulie chakula wala ininunulie nguo za watoto wangu, wala inijengee nyumba.

Lakini ni kweli kwamba serikali haina majukumu kwa raia wake? Unasema kutoka moyoni?

Kwa hiyo na umeme tujiwekee wenyewe? Kwa hiyo na barabara tujijengee wenyewe? Na hospitali za kutibiwa magonjwa ambayo viongozi wanaenda Ulaya tujijengee wenyewe?

Na kodi zetu zikikusanywa tunakuwa kama tumenyang'anywa au tumeibiwa, hatuna hata kauli kodi hiyo ifanye nini?

Na kama kodi hiyo inatumika vibaya tusihoji?

Mkuu Bakari Madaya - Unahitaji Elimu ya Uraia kujua Jukumu la Serikali kwako wewe mlipa kodi wake.
 
Mleta mada, maoni yako yananuka uccm, unaha, ukabila, ukanda na udini na siyo utaifa kama unavyofikiri. Huna utaifa wowote hapa.
 
Nchi hii imekuwa kama China. Watu wengi wanadhani China iko salama sana lakini haiku salama. China imeajiri watu zaidi ya elfu thelasini kwa ajili tu ya kuregulate mijadala kwenye social forums ili watu wasiikosoe serekali yao. Sasa huu upuuzi mtu na akili yake amekaa chini kuandika ili amdanganye nani? Hivi kweli nani mwenye akili utamwambia kuwa CHADEMA ni chama cha kikabila, Kikanda, Kidini,.. atakayekuelewa ni nani, kwa sababu hata mtoto wa darasa la kwanza hatakuelewa. Pamoja na kuwa CHADEMA hakina nguvu ya kifedha, kwa sababu CCM ilinyanganya wananchi rasilimali zao bado itakubalika kwa sera zake siku zote. Kwa hiyo ni bora usisumbuke kuharibu muda wako ambao ungeutumia kufanya jambo la maana kukichafua kwa sababu hakitachafuka. Na kwa jinsi unavyoandika uzushi usio na mbele wala nyuma ndio wanachama wengi wanajiunga.
Lakini pia, kwa kuzusha mambo ya kijinga namna hii kunaweza kuwafanya watu wakaleta maafa, nakuambia tu kuwa damu ikimwagika kwa sababu ya maandishi yako itadaiwa kwako na huyo aliyekutuma. So, watch out
 
Mijitu ina uroho wa madaraka inasahau utu na maendeleo ya wananchi
 
Tatizo CDM wanafikilia siasa chafu za kitem mda wowote hawana hoja zaid ya uongo na chuki.KWAILO WAMECHEMSHA.
 
Utadilije fikra kwa elimu duni? Afya mgogoro na rushwa iliyokithiri? Japokuwa sijajua kiwango chako cha elimu ila kwa elimu yangu ndogo najua kuwa ili nchi iendelee inahitaji:
1.watu 2.siasa safi na 3.uongozi bora. Ikiwa serikali yako unayoitukuza haisimamii hivi vitu vitatu halafu unataka kila mtanzania akubaliane na mawazo yako bila kulipwa kama wewe pengine unavyolipwa itachukua mapinduzi makubwa. Hata hivyo,si kila wazo unaloona linafaa kwako litawafaa wote labda kwa masisiemu pekee duniani.
 
Kwa mda mrefu mbowe na lema wamekuwa wakifanya mambo mengi wakiwa pamoja.

katika mambo hayo wanayofanya mengi yamekuwa si ya kuleta amani katika taifa letu bali ni ya uvunjifu wa amani.

katika matukio hayo yakiwemo ya mandamano kukaidi amri za jeshi la polisi,kufanya mikusanyiko haramu na mengineyo mbowe na lema wamekuwa wakihusika pamoja.

hata katika mkusanyiko haramu wa jana ambao ulitawanywa na polisi hatimaye mbowe na lema kukimbia na baadhi ya wabunge wa chadema kukamatwa lema na mbowe wamekimbia pamoja.

kitu ambacho najiuliza kila siku ni nani kati yao anayemuongoza mwenzake,awali niliamini kuwa kwa vile mbowe ni mwenyekiti yawezekana anamuongoza lema katika mambo yote lakini nikabaini kuwa hata lema anamamlaka sana ndani ya chadema inasemekana hata amri ya kuwataka wabunge wa chadema kutohudhuria vikao vya bunge badala yake waende arusha kuaga waliofariki lema ndiye aliyependekeza na mbowe akakubari.

sasa mambo ya namna hii nani anamuongoza mwenzake au nani mwenye uelewa mpana zaidi ya mwenzake au wote wanamawazo linganifu hivyo wanawaza pamoja na kuamua pamoja?.wanyakyusa husema mbombo jilipo.
 
Bila shaka umetumwa na mumeo mwigulu, coz hata mwonekano wako tu upo kikahaba
 
Chama kidogo sana hata mkt anaendesha chama kama genge la mchicha hatuwezi Ms hatukubali kuwapa nchi walie tuuuu kiruuu
 
Chama kidogo sana hata mkt anaendesha chama kama genge la mchicha hatuwezi Ms hatukubali kuwapa nchi walie tuuuu kiruuu
Mkuu wale jamaa waajabu sana hakuna mkubwa wala mdogo kila mtu anamalaka kwa wakati wake na nafasi yake.
 
Wakuu siku si nyingi lema na mbowe watakuja na single nyingine baada ya hii waliyowatuhumu polisi kuchuja wameamua kuwa wabunge wa matukio na uongo.
 
Katibu mkuu wa CHADEMA taifa kwa sasa yuko hoi bin taabani kuongoza chama chake, ambacho hivi karibuni kiliweza kujizolea sifa hapa nchini, kwa kile kinacho daiwa kuwa kiliweza kutoa changamoto kubwa kwa chama tawala (CCM).

Jambo la kushangaza na kushtua kuhusu hiki chama, ni kuporomoka kwa umaarufu wake nchini, baada ya watanzania kugundua kuwa sio chama cha 'demokrasia' na 'maendeleo' kama wanavyo jipambanua, ila ni chama cha vurugu, fujo na maandamano yenye kuhatarisha amani na utulivu wa nchi.

Sifa hizi mpya kwa chama hiki, ambazo ni fujo na vurugu, zimetolewa na wananchi baada tu ya CHADEMA kumpa mamlaka Dr Slaa ya kuwa mtendaji mkuu wa chama hicho, Dr Slaa kwa siasa na mbinu zake, alidhani kwa kutumia maandamano basi ndio itakuwa njia pekee ya kuzidi kuinua jina na hadhi ya chama, kumbe imekuwa kinyume chake.

Mikakati ya Dr Slaa ya kuleta mageuzi ya siasa hapa nchini kupitia chama chake (CHADEMA) na washirika wake IMEDODA, na badala yake mikakati hiyo imefanikiwa kuondoa na kutokomeza kabisa sentensi isemayo "Tanzania ni kisiwa cha amani", na kwa sasa kuwa kisiwa cha wahanga wa mabomu.

Hoja ya msingi hapa ni kwamba, kama Dr Slaa amechemka na yuko hoi kuiongoza CHADEMA kwenye kufanya siasa za kistaarabu na safi. Je, atawezaje kuongoza nchi yetu yenye changamoto za kila aina?, haya ni mambo ya msingi sana kuhoji, kwani kushabikia uozo ambao utaenda kuliangamiza taifa sio UZALENDO hata kidogo.
 
Back
Top Bottom