Mwisho wa CHADEMA unatabiriwa kila kukicha lakini haufiki!!Ukiangalia CHADEMA mwaka 2015 ilipata kura mil 6 si kua ina wafuasi hao ukiigawanya hiyo mil 6 unaipata hapa mil 2.5 CHADEMA 1.5 ni wale wasio na chama na wengine walipiga kura za hasira kwa sababu lowassa kakatwa CCM na hawa mil 2 ni CUF hivyo ukijumlisha unapata mil 6 je kwa hali ilivyo sasa chadema wanauwezo wa kupata kura hizo.
CCM wameshakaa sawa kama mnavyoshuhudia kila kukicha wimbi la hama hama wale wenye hasira wameshaamua kurudi. CUF ipo tayari kusimama yenyewe bila mwamvuli wa ukawa naiona CHADEMA ikirudi kwenye zama zake za shida na mateso kwa hesabu hizi hata CHADEMA wakiambiwa wasimamie wao huo uchaguzi kama wanavyodai kuibiwa watajikana au wamlete uhuru Kenyatta kusimamia ni aibu.
Swali ni je CHADEMA ina uwezo wa kufikisha kura mil 6 kwa hali ilivyo sasa ni ndoto!
Ndani ya CHADEMA kuna shida kubwa lakini pia ndani ya CCM kuna shida ila shida kubwa kuliko zote ipo ndani ya vichwa vya Watanzania.
Chadema wamelalamika sana hasa kuhusu uchaguzi,kuna tunayoungana nao kama fujo na hila za kutoa mawakala vituoni lakini nao watupe ushirikiano kwa kuonyesha ushahidi kama wa kuibiwa kura.Kwa kina Lijualikali tunaambiwa CDM ilishinda wazi lakini hata hiyo copy ya matokeo kutuwekea hapa hakuna.
Jambo la pili kwa CDM ni kukosa mtu mwenye authoritative voice kama ya Lissu au Slaa.Maazimio hayawasilishwi katika sauti inayostahili (Ila Benson Kigaila,hili ni jembe).
Kwa CCM na upofu uliotukuka wanaamini na wanaaminishana ya kuwa kuna wakati upinzani utakufa,hii ni ndoto ya mchana na wanachoweza ni kubadili aina ya upinzani kutoka wa hoja kuwa wa maguvu.Bila changamoto zinazoletwa na upinzani kwa hulka ya binadamu ni kuwa watalala.JPM kama ana dhamira ya dhati ya kuitakia nchi mema ni lazima ahakikishe ana upinzani wenye nguvu utakaomsaidia kusafisha nchi pia chama chake ambacho hakiwezi kujiweka kando na uchafu wote tunaouona leo.
Kwa Watanzania wenzangu,maendeleo yote yanayoonekana leo yanatokana na upinzani na hofu ya Chama tawala kutoka madarakani.Tujenge upinzani imara ili tuendelee kupata maendeleo ya kweli!!!!
Kwa Waislamu,"Ukiona katika mji hakuna kuhitilafiana katika mawazo basi jua mji huo hauna Maulamaa (Wasomi).
Nawasilisha.