Chadema ina nguvu sana kisipuuzwe

Chadema ina nguvu sana kisipuuzwe

simaanishi vigogo wa chdm au watu maarufu. namaanisha raia wa kawaida walio makini ktk kufuatilia mambo ya kisiasa nchini. hata wimbi la wanachuo kujiunga na chdm limepungua. unaweza kukataa lkn nikupe mfano mmoja. ktk uchaaguzi wa madiwani wiki iliyopita, ktk kata 22, ccm imeshinda kata 16. kata 6 zimechukuliwa na cuf na chdm. kama umaarufu wa chdm umeongezeka, kwa nn haijashinda angalau kata kumi hadi 15? siasa hupimwa kwa ushindi ktk chguzi na siyo makelele kwenye mitandao. Kwenye huo uchaguz wa madiwan chadema wameongeza kata tano zilizokuw zinashikiliwa na ccm sas unasemaj chama kinakimbiwa wakati kimeongeza madiwan acha siasa kuwa mkwel
 
Asante kwa maelezo yako , japo siyo mageni sana kwenye vichwa vyetu , maana hata pale ofisi ndogo - Lumumba hilo wanalielewa , labda kwa kuongezea kidogo tu inasemekana ni USHUJAA kuvaa Magwanda ya CHADEMA na huwa mara zote unaonekana kama MKOMBOZI (Mpigania uhuru ) na ni AIBU KUBWA SANA kuonekana umevaa zile sare za CCM ( Maana huonekana kama wezi - mafisadi , wakandamizaji , wenye roho mbaya ) huku Mtaani , hata hawa wanaoitwa Buku 7 fc akina HAMMY- D , Bungeni & co hawawezi kuthubutu kuvaa sare za ccm mtaani ! Sasa jaribu kuwauliza kisa na mkasa .
 
watu wanayoiangusha chdm ni wabunge. akina slaa, zitto, ndesamburo na mdee kipindi kile walikua wachache lkn walijikita kwenye kujenga hoja na watanzania wakavutiwa na hoja zao. matunda yake ni kwamba idadi ya wabunge iliongezeka mwaka 2010. tatizo la akina sugu, wenje, msigwa, lissu, lema nk... ni utangulizaji wa jazba kuliko kujenga hoja kwa nidhamu kama ile ya 2005-2010. kwa hali hii, sidhani kama chdm kinaimarika. chama kinakimbiwa na watu makini kwa ss hivi. anaekataa hili basi ana sbb zake

Endelea kujipa matumaini
 
Bila kuficha kuonesha hisia zangu za kisiasa, ni ukweli usiopingika kuwa CDM kwa sasa ina nguvu kubwa sana hapa nchini. Endapo chaguzi zitafanyika kwa mazingira ya haki na usawa sioni chama chochote kitakachothubutu kushindana nacho hasa upande wa Tanzania Bara. Kwa maoni yangu ipo haja kuheshimu matakwa ya wananchi hasa kuhusu kile wanachoamini kuwa Chama kitakachowavusha kuelekea ngazi nyingine ya Maendeleo. Yalitokea Zambia, Malawi, Kenya, Afrika Kusini, na kwingineko kwa hiyo si ajabu yakatokea hapa Tanzania. Mabavu sio suluhu, ila nguvu ya wenye nchi (Wananchi) ndio jibu. Changamoto waliyonayo CDM ni kututoa Watanzania hofu ya haya yafuatayo; 1: Ina Mipango gani ya kuivusha nchi kuelekea uchumi imara unaogusa maisha ya kila siku ya Mtanzania ambaye siku zote amekuwa mhanga wa harakati za uchumi wa kibeberu? 2. Ina Mkakati gani wa kushughulikia tatizo linalokuwa kila siku la ukosefu wa ajira kwa nguvu kazi ya taifa yaani VIJANA? Nini msimamo wa Chama katika kushughulikia Raslimali za Taifa (Gesi na Madini mengineyo?) na mwisho, ni vema tukajua mikakati iliyopo katika kuboresha huduma za kijamii mfano Afya, Elimu na Maji. Kama uchaguzi ungefanyika leo, nisingeona tabu kuwapa CDM kura yangu.

Nakubaliana na wewe kuhusu hoja za msingi zinazohusu maendeleo ya nchi kama ulivyoainisha kwenye 1 na 2 hapo juu. Pamoja na changamoto ambazo CDM wanapitia kwa sasa, nyingi zikiwa za kutengenezwa na mfumo wa utawala ili kuwapunguza kasi na kuwachafua mbele ya umma wa watanzania, ni vzr wakijikita pia katika kueleza sera za chama katika hayo uliyoyaytaja na mengine yanayogusa matakwa ya mwananchi wa kawaida mijini na vijijini.
 
wananchi kwa sasa hatuna imani na chadema kwa sababu mnatajwa tajwa sana kuhusika ktk matukio mabaya na kinyama hapa nchini. la kibanda mmetajwa, la tindikali kesi iko mahakamani, la sumu ndio hivo tena lwakatare, utamshaiwishije mtu kuwa nyie ni waadilifu??? achilia mbali wake za watu
 
Back
Top Bottom