Chadema ina mtaji mkubwa sana arumeru mashariki

Feb 16, 2012
27
13
Mbio za kuwania ubunge kwa jimbo la Arumeru mashariki zimeanza kwa kila chama kuteua mwakilishi wake. Kwa jinsi yeyote ile CHADEMA kinaonekana kuwa na mtaji mkubwa sana katika jimbo hili.

Kwanza ni kura za mgombea wa CHADEMA aliye pambana kiume uchaguzi uliopita na kuambulia nafasi ya pili baada ya kura nyingi sana kuibwa na chama tawala, lakini jambo la pili muhimu ni nguvu ya CHADEMA Arusha mjini jimbo lililo karibu kabisa na jimbo hili la Arumeru Mashariki. Usisahau makamanda wapiganaji wote wanao toka Arusha mjini watakwenda Arumeru kirahisi na kutawala kampeni zitakapo anza.

Mtaji huu ukitumiwa vema, CCM hawatatoka Arumeru, huu ni wakati wa kunoa majembe kwani muda si muda mambo hote yatakuwa ni Arumeru.
 
Akili zako zinafanana na za mtatiro aliyesema kafu inamtaji igunga wa kura elfu kumi na moja. Umesahau kama kuna wakati mtaji huliwa? Dogo huyo alipata kura hizo akiwa amegombea na mgonjwa. Mazingira yamebadilika, nakuombea uwe hai mpaka tar 2 april upate majibu
 
Eti makamanda watakuja,nakumbuka Mwigulu alisema kinondoni alipotokea igunga kuwa 'Nzi hata wawe wengi kiasi gani hawezi kutengeneza asali" ngoja uone ukweli kuwa watakuja kwa njia moja makamanda wako na kutawanyika kwa njia saba. Mwigulu yupo huko
 
Huwa nasikitishwa sana na vijana kama wewe wenye mawazo ya kukataa mabadiliko wakati wao ndio wahanga wakubwa wa hali mbaya ya uchumi inayoendelea sasa nchini chini ya chama kimoja tu cha siasa tangu uhuru. Regerdless ni chama gani, nchi yetu iko pabaya hivi ndugu yangu huono haya ila ushabiki tu! nyie ndo mnaua nchi hii!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom