CHADEMA imevuna mawaziri zaidi ya 8 kutoka CCM na Katibu Mkuu mmoja hadi sasa; Je, orodha itaongezeka au itapungua?

Nyimbo za mafisadi zimekuwa zilipendwa, polisi yake, mahakama yake na hakimu ndiye yeye, toka aingie ameshawafunga wangapi zaidi ya kelele majukwaani.
Kumbuka raisi hafungi, inayofunga ni mahakama. Kama unataka kujua zaidi kuhusu mafisadi waliofungwa iulize mahakama, sio raisi
 
Tulizo la mafisadi jaribu kuwaangalia hao wote ni mafisadi chadema na mafisadi ni uji na mgonjwa.
hao wote wanaohamia chadema wanatuhuma za ufisadi inawezekanaje CDM kuwapokea watu ambao wanatuhuma za ufisadi
Ifikie hatua tukiite chama Kimbilio la Mafisadi au Kichaka cha Mafisadi.
Ni ajabu kabisa mtu awe fisadi akiwa CCM tu, akitoka ni kamanda
umeona ee.... mafisadi wakifukuzwa ccm pakukimbilia ndio huko cdm
Hivi CHADEMA iko nje ya Tanzania kwamba inahitajika Interpol kuwakamata,

Ukweli ni kwamba mtu yeyote anayetoka CCM kujiunga CHADEMA huyo mtu lazima anajiamini sana, mafisadi na wala rushwa wamejificha CCM.
 
Itafika mahali tushindwe kutofautisha kati ya CHADEMA na CCM maana wale wote waliokuwa na makandokando ndio hao wanahamia huko na wanasaka tonge kwa njia tofauti, je na wakipata vyeo tabia zao za ki ccm zitakuwa zimebadilika?

Kwa dhana ya upinzani wa kweli ingekua poa sana tungekua na chama ambacho kimeanzishwa na watu wanaofikiri tofauti nje ya haya mavyama tuliyonayo na wakajipambanua kiitikadi tofauti kabisa na sasa. Ukitizama saana ni ngum kjua tofauti ya hivi vyama
 
Hivi CHADEMA iko nje ya Tanzania kwamba inahitajika Interpol kuwakamata,

Ukweli ni kwamba mtu yeyote anayetoka CCM kujiunga CHADEMA huyo mtu lazima anajiamini sana, mafisadi na wala rushwa wamejificha CCM.
Huyo Nyalandu fukuto lake la ujangili litaanza kurindima muda si muda.

Juzi Kigwangala alisema anayo majina ya majangili wote wakiwemo wabunge baada ya kuona kijana wake kukamatwa jana kaona aage ili akianza kushughulikiwa ajitete ni siasa,,, amekosea sana tutamshughulikia bila huruma
 
Itafika mahali tushindwe kutofautisha kati ya CHADEMA na CCM maana wale wote waliokuwa na makandokando ndio hao wanahamia huko na wanasaka tonge kwa njia tofauti, je na wakipata vyeo tabia zao za ki ccm zitakuwa zimebadilika? Kwa dhana ya upinzani wa kweli ingekua poa sana tungekua na chama ambacho kimeanzishwa na watu wanaofikiri tofauti nje ya haya mavyama tuliyonayo na wakajipambanua kiitikadi tofauti kabisa na sasa. Ukitizama saana ni ngum kjua tofauti ya hivi vyama
Lowassa yupo Chadema, kashitakiwa?
Sumaye yupo Chadema, kashitakiwa?
Kingunge bado yuko Chadema, kashitakiwa?
Masha yuko Chadema, kashitakiwa?
Ntagazwa yuko Chadema, kashitakiwa?

Ukiniambia kiongozi yeyote aliyetoka CCM akaenda Chadema ameshitakiwa kwa ufisadi nakurushia milioni moja sasa hivi.
 
Tabu kubwa ni kwamba hicho chama kinazidi kufa.. kwa hiyo ni mizoga tu huko hawajakuendeleza chama bali kuchangua kukiua.

Endeleeni kuita wengine wachovu wajiunge nanyu. Hawatamisiwa hata kidunchu
 
Baada ya Mhe.Lazaro Nyarandu kuachana na CCM na kuomba kujiunga na Chadema,nimejaribu kukumbuka idadi ya mawaziri wakuu,mawaziri,manaibu waziri ambao wamehamia Chadema,kwa haraka nimepata idadi ipatayo nane akiwemo Lowassa,Sumaye,Kingunge,Ntagazwa,Makongoro,Lau Masha,Ole Medeye(baadaye alihamia UDP) na sasa Nyalandu. Hawa wote walipata kuongoza Wizara mbalimbali kwa vipindi tofauti. Pia mhe.Ruth Mollel huyu alikuwa Katibu Mkuu wa wizara na sasa yupo Chadema.
Kwa hali ilivyo je idadi inweza kuongezeka ?? Maana wapo wanaomtaja Mhe. Nape kuwa yupo mbioni kuhama na wengine pia.
Zipo habari kuwa Chadema wamekuwa wakipita pita na kujigamba kuwa watawachukua wastaafu wa vyombo vya ulinzi na usalama hasa wakitajwa viongozi wawili wa TISS, Apson Mwangonda na Hassy Kitine kuwa ni watu wao.
Kama Chadema inavuna Viongozi ambao tayari CCM ilishawatema nakuwatupa nje na kuwanyima uwaziri je tuamini kuwa Chadema ni kokoro la kuvuta kila uchafu? Hebu tukumbushe Waziri ambaye alijiudhuru uwaziri nakujiunga Chadema moja kwa moja?
 
Kumbuka raisi hafungi, inayofunga ni mahakama. Kama unataka kujua zaidi kuhusu mafisadi waliofungwa iulize mahakama, sio raisi
Huna unachokijua, kabaki kubambikizia watu kesi Manji leo yuko nje, Masamaki leo yuko nje, Kitlya leo yuko nje kinachofanyika ni visasi na roho mbaya hakuna cha ufisadi.
 
Huyo Nyalandu fukuto lake la ujangili litaanza kurindima muda si muda.

Juzi Kigwangala alisema anayo majina ya majangili wote wakiwemo wabunge baada ya kuona kijana wake kukamatwa jana kaona aage ili akianza kushughulikiwa ajitete ni siasa,,, amekosea sana tutamshughulikia bila huruma
Wimbo wa Lowassa mnaugeza kuwa wa Nyalandu tumeshawazoea.
 
Huna unachokijua, kabaki kubambikizia watu kesi Manji leo yuko nje, Masamaki leo yuko nje, Kitlya leo yuko nje kinachofanyika ni visasi na roho mbaya hakuna cha ufisadi.
Kwa hioyo ulitaka wafungw ili ufurahi? Kwa kukusaidia tu nenda pale Mawasiliano kwenye shule ya Law School ulizia karani wa mahakama ya mafisadi, muombe na atakupa takwimu zinazohusu mashauri ya mafisadi yanayoendelea na yaliyokwisha sikilizwa.
 
Kama Chadema inavuna Viongozi ambao tayari CCM ilishawatema nakuwatupa nje na kuwanyima uwaziri je tuamini kuwa Chadema ni kokoro la kuvuta kila uchafu? Hebu tukumbushe Waziri ambaye alijiudhuru uwaziri nakujiunga Chadema moja kwa moja?
Inamaana ukitolewa uwaziri umeshakuwa mchafu, kama hivyo CCM ni shimo la choo kabisa maana waliotemwa uwaziri na bado wako CCM kina Pendazoe ni wengi zaidi ya mawaziri waliopo.
 
Jamaaa kauza Twiga wetu kweupeeeeeeeeeeeee kwenda arabuni na Uwindaji haramu kibao, na sasa kaenda kwa Mchungaji Msigwa aliyekuwa mstari wa mbele kumuwasha! Amazing
 
Kwa hioyo ulitaka wafungw ili ufurahi? Kwa kukusaidia tu nenda pale Mawasiliano kwenye shule ya Law School ulizia karani wa mahakama ya mafisadi, muombe na atakupa takwimu zinazohusu mashauri ya mafisadi yanayoendelea na yaliyokwisha sikilizwa.
Huna data nyamaza.
 
Back
Top Bottom