CHADEMA imejipanga 2015?

CHADEMA imejipanga 2015?

KIM KARDASH

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
5,139
Reaction score
1,149
Hakuna ubishi kwamba kwa sasa chadema angalau ndio kinaonyesha upinzani wa kweli dhidi ya chama kilichopewa dhamana na wananchi kuisimamia serikali halali iliyopo madarakani kwa mujibu wa katiba.Kutokana na umuhimu wa chadema kama chama kikuu cha upinzani nadhani ipo haja ya kukitizama sawasawa cha hiki na kujaribu kuifahamu sawasawa mikakati na malengo yako kisiasa.

Kwa kuanzia je CHADEMA inao mkakati gani hasa kuhakikisha inasimamisha mgombea ubunge katika kila eneo bunge (jimbo) kwenye uchaguzi mkuu ujao tofauti na uchaguzi mkuu uliopita ambapo kwenye maeneo bunge mengi haikuwa na wagombea ubunge?

Nadhani upo umuhimu wa chadema kuwa serious kwenye eneo hili kwa kupanga mikakati kuanzia sasa ili kipate wagombea wa kweli na sio wagombea wa kuokoteza sijui wasanii wa bongo movie,bongo fleva na makapi ya ccm,no kiwe na wagombea wa kweli ambao wameandaliwa na kuiva sawasawa na hii itakisaidia sana cha kuondokana na dhana ya kuwa kina safu nyembamba ya uongozi kiasi kwamba inakilazimu kuokoteza wagombea uongozi kama ilivyotokezea kwa john shibuda kwenye ubunge na samuel sitta ambae ilibaki chupu chupu awe mgombea urais wa chadema kama sio yeye mwenyewe kuwachomolea mwishoni kabisa.Pia ipo ile kashfa ya kumsimamisha mgombea mwenza kutoka zanzibar ambae hakua na sifa,badae ikabidi afichwe na hakuwahi kuonekana tena mpaka huwa najiuliza slaa kama angeshinda angeingia ikulu peke yake bila makamu wa rais ambae ndio nembo ya muungano,wazanzibar wangeipokeaje serikali ya slaa,zipo misteps kibao ambazo inabidi zifanyiwe kazi na kutoa majawabu kabla ya kuingia kwenye uchaguzi mungine.

Upi mkakati wa chadema kuhakikisha kinasimamisha mgombea wa kweli kwenye kila eneo bunge la nchi hii???

Nawasilisha.
 
ya Juliana yamekwisha? Kama huyu tu kawatoa jasho, je watz wote?

Wamejipanga mstarini
 
Wewe unaongelea wabunge wakati uongozi ndani ya chama bado msuguano. Subiri weekend hii chama kinafanya maamuzi 'magumu', and then come back with those questions and suggestions

Viongozi hakifikilii kwa sasa swala la ubunge, viongozi wake bado wanapigana vijembe kwanza (positioning) kwa sababu kuna uchaguzi wa ndani unakuja. ngoja hilo lipite halafu njoo na tena hapa.
 
Mkuu Kim Kadash heri ya mwaka mpya. Naona kama ulipotea vile?

CDM kwa sasa wanajipanga nasikia kuna masalia wanatakiwa waondolewe, kuna tetesi za mipasuko ndani ya Chama huku mzee Wasira akirudia kauli yake kuwa CHADEMA itasambaratika punde.

Nadhani kamati kuu inakutana kuanzia leo basi huenda tukasikia maamuzi yanayotikisa.
 
Wamfukuze na zzk si wanasema msaliti!?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Kim Kadash heri ya mwaka mpya. Naona kama ulipotea vile?

CDM kwa sasa wanajipanga nasikia kuna masalia wanatakiwa waondolewe, kuna tetesi za mipasuko ndani ya Chama huku mzee Wasira akirudia kauli yake kuwa CHADEMA itasambaratika punde.

Nadhani kamati kuu inakutana kuanzia leo basi huenda tukasikia maamuzi yanayotikisa.

Nipo kamanda,wakati mungine huwa nashiriki kwa njia ya kusoma tu,hasa kuanzia mwishoni mwa mwaka jana,nilijiweka pembeni kuwapisha wana cdm wamalize mpasuko ndani ya chama maana kama ulivyokua unaona wakilumbana na kuvuana nguo humu kuna mengi hatukua tukiyafahamu lakini waliyaweka hadharani ikiwemo suala la kumuomba samuel sitta wa ccm awe mgombea wa chadema!wakaeleza kwamba chama kama chama hakikua na mgombea kwenye nafasi ya urais mpaka baadae bwana slaa alipoombwa kuokoa jahazi kwa kupewa hela na kuahidiwa marupu rupu na stahili zote kama mbunge hata akishindwa urais,ndio akakubali,mwanzo aligoma akiamini hawezi kushinda ivyo hakutaka kuziweka rehani posho zake za ubunge wa karatu
 
Wewe mtoa Mada au yeyote yule anitajie tu mtu mmoja CHADEMA ambaye anadhani anaweza kugombea urais na KUSHINDA,kabla hatujaendelea na mada.
 
Hawa hawana uwezo wa kujenga wagombea wao wenyewe bali watasubiri makapi ya ccm.hiki hakina mwelekeo mzuri bali kitakuwa ccm b.nafikiri nccr kinakuja vizuri kinahitaji spot ya wa tz
 
Nilikua nasoma pahala nasikia zitto amemkaribisha tena samuel sitta awe mgombea urais wa tanzania kwa tikiti ya chadema kama kweli basi mzee sitta alikua na sababu ya kusema tatizo la chadema ni safu nyembamba ya uongozi ambayo ni lazima ijaziliziwe na watu kutoka vyama vingine! hapa kuna tatizo
 
Nipo kamanda,wakati mungine huwa nashiriki kwa njia ya kusoma tu,hasa kuanzia mwishoni mwa mwaka jana,nilijiweka pembeni kuwapisha wana cdm wamalize mpasuko ndani ya chama maana kama ulivyokua unaona wakilumbana na kuvuana nguo humu kuna mengi hatukua tukiyafahamu lakini waliyaweka hadharani ikiwemo suala la kumuomba samuel sitta wa ccm awe mgombea wa chadema!wakaeleza kwamba chama kama chama hakikua na mgombea kwenye nafasi ya urais mpaka baadae bwana slaa alipoombwa kuokoa jahazi kwa kupewa hela na kuahidiwa marupu rupu na stahili zote kama mbunge hata akishindwa urais,ndio akakubali,mwanzo aligoma akiamini hawezi kushinda ivyo hakutaka kuziweka rehani posho zake za ubunge wa karatu

Posho zina nguvu kama ya Sunami!
 
Wamfukuze na zzk si wanasema msaliti!?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Kulingana na Mkuu Ben Saa8 kiongozi wa masalia ni Prezo na Dr. Kitila Mkumbo. Ili kumaliza masalia watimuliwe wote
 
Wamfukuze na zzk si wanasema msaliti!?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

hiyo ni ndoto hawatathubutu la sivyo chama kitapasuka vipande viwili vikubwa mno
 
Hawa hawana uwezo wa kujenga wagombea wao wenyewe bali watasubiri makapi ya ccm.hiki hakina mwelekeo mzuri bali kitakuwa ccm b.nafikiri nccr kinakuja vizuri kinahitaji spot ya wa tz

hakika we ni mwehu.......
 
Tutajua mbele ya safari, la muhimu hivi sasa CCM iondoke kwanza madarakani, kwa sababu wakati wa ukombozi tunaancha pembeni mengineyo hadi uhuru upatikane, hata TANU hawakuwa wamejipanga ile kivile, bora hata CHADEMA ina baadhi ya makada waliokuwa CCM kipindi kirefu wakachoshwa na mbwembwe za kidhalimu wakaamua kupitia dirishani na kurukia nje, haijalishi nao wanatafuta maslahi lakini kumbuka, UKILA NA KIPOFU.... na panya mwerevu ni yule anayepuliza wakati aking'ata kisigino chako kuliko yule anayekuachia mauvimu moja kwa moja! 😱hwell:
 
Magamba kazini
jibu swali,cdm inao mkakati kuhakisha this time inasimamisha mgombea ubunge katika kila eneo bunge tofauti na uchaguzi uliopita ambapo sehemu nyingi hakikua hata na wagombea ubunge?
 
Back
Top Bottom