Msimamo wa ACT Wazalendo kuhusu
Ushirikiano wa vyama
Kumekuwa na shauku ya wananchi kwa sisi
kushirikiana na vyama vingine vya siasa ili
kufanikisha malengo yetu ya kuleta mapinduzi
ya kiuchumi kwa kuubomoa mfumo ...wa
uchumi unaonyonya wananchi. Msimamo wetu
upo wazi na tumeueleza mara kadhaa
1 tunaunga mkono juhudi zozote za kushirikiana
kwa vyama na hili linathibitishwa na jina letu
ALLIANCE na Msimamo wetu kuhusu mabadiliko
ya Katiba.
2 tunataka ushirikiano utakaonufaisha wananchi
na sio ushirikiano wa kugawana nafasi za
uongozi.
3 hatuna shida na Tupo tayari kushirikiana na
chama chochote kilicho tayari kushirikiana na
sisi ikiwemo UKAWA ili kuunganisha nguvu
kuitoa CCM kwa malengo ya kujenga uchumi
shirikishi wenye kuzalisha ajira nyingi na bora,
wenye mfumo wa hifadhi ya jamii kwa wananchi
wote na wenye kutokomeza umasikini.
ACT Wazalendo haijatoa kauli yeyote dhidi ya
UKAWA kama inavyoaminishwa na baadhi ya
watu. Bali tumeweka wazi kuwa lazima misingi
ya kiitikadi na kifalsafa izingatiwe katika
ushirikiano. Tupo tayari kwa UMOJA. UMOJA ni
moja ya misingi mikuu 10 ya chama Chetu na
Umoja ni nguvu.
Tupo tayari