Mkutano wa CCM uliofanyika leo kata ya Kigera jimbo la Musoma Mjini,CCM wamejikuta wakiambulia patupu kwa kupata idadi ya watu wasiozidi 60 mbali na kwamba kila mtu aliyekuwa anaudhuria mkutano huo alilipwa elfu kumi.
Baada ya mkutano kuanza na Mathayo kupanda jukwaani kuanza kuhutubia watu walimzomea na mkutano ukasimama kwa muda.
Hii ni ishara tosha inayoonesha anguko la CCM na kama watakuwa bado hawajaelewa basi watakuwa ni sikio la kufa.
Kinachowaumiza ni maguo yao ya rangi ya kijani ,wanaonekana idadi yao hata ukiwa mita mia tano utawahesabu na kujua hamna kitu ,kwa ufupi asievaa guo la kijani sio mwenzao,ndivyo wanavyojiweka.
Kinachowaumiza ni maguo yao ya rangi ya kijani ,wanaonekana idadi yao hata ukiwa mita mia tano utawahesabu na kujua hamna kitu ,kwa ufupi asievaa guo la kijani sio mwenzao,ndivyo wanavyojiweka.
Kifo cha magamba ni pale watu wengi watakapojitokeza kujiandikisha na kupiga kura! Wao wanategemea kura za kununua tu! Nadhani 2015 hata bei ya kura moja inaweza kupanda hata kufika laki moja watu wamekuwa wajanja zaidi! Hawatakubali wapiga kura wawe wengi maana itakuwa ngumu kushinda kwa kura za kununua!
Wapinzani inabidi wawe makini sana mwakani maana kutakuwa na mizengwe ya kufa mtu na kama watu hawatashutukia wengi sana hawataruhusiwa hata kujiandikisha! Hata kwenye vitambulisho vya uraia tayari inachezwa michezo michafu sijui kunaagenda gani nyuma ya pazia kuhusiana na hvi vitambulisho na uchaguzi! Ngonja tuone ujanja wao utafika wapi, ila 2015 watu hawatafanya makosa!