CCM ya watanzania, Chadema ya wateule

CCM ya watanzania, Chadema ya wateule

MAFILILI

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2011
Posts
2,377
Reaction score
1,200
Siku zinavyozidi kusonga mbele kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa 2014, ikiwa ni JARAMBA la Uchaguzi Mkuu 2015; chama kisicho na demokrasia kimezidi kupungukiwa wapenzi huku wakiambulia kapa mahakama ya rufaa kuhusiana na majimbo ya ubunge ya Igunga na Sumbawanga Mjini. Hali katika mikoa ya DSM, Pwani, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Kusini Unguja, Mtwara, Mbeya, Iringa, Lindi, Tanga, Ruvuma, Morogoro, Singida, Rukwa, Tabora, Shinyanga, Simiyu,Geita, Kagera, Mara, Njombe na makao makuu ya nchi - Dodoma ni KUSHAMIRI kwa rangi ya kijani iliyo maarufu kwa CCM. Hali imekuwa ngumu katika mikoa hiyo kwa CHADEMA huku wakishuhudiwa uwingi wa wafuasi wao kauchana na chama hichona kurejea CCM kutokana na kuchoshwa na siasa za CHADEMA zilizoegemea kwenye mgawanyiko na upendeleo kutegemea na UDINI, UKANDA, UKABILA na UKOO. Yote kwa yote ofisi za CHADEMA zililzokuwapo katika maeneo hayo zimegeuzwa kuwa maskani ya vijana wa CCM walioachana na CDM.
Dalili zipo wazi kuwa CDM haitaweza kushiriki katika uchaguzi wa mwakani katika maeneo makubwa ya mikoa hiyo kwa vile hawajawa na misingi ya kuendeshea siasa katika mikoa husika. Hiyo ni kuashiria CCM itajihakikishia kupata ushindi wa asilimia 85% ya uchaguzi wa serikali za mitaa huku vyama vya upinzani vikigawana asilimia zilizobaki.

Watanzania wapenda amani mlioko nje ya nchi mkae kwa amani, mkijua CCM itazidi kutesa katika anga za siasa za TZ .Vijana wa CDM ni mahodari kwa kupiga proganda katika mitandao huku wakisahau kuwatembelea wapiga kura mikoani. Kutokana nakukata tamaa, CDM imeamua kuleta vurugu katika mikutano yao ya siasa, bungeni na mabaraza ya halmashauri.

CCM Oyee!
 
aisee kumbe wafu kweli huwa wanatembea.. hivi wewe unapitaga mitaa ipi??? unashukia hoteli za kitalii unakutana na mafisadi wanaisifia CCM unahisi kote sawa.... hahahaha... hebu mwambie Mwenyekiti wako aitishe uchaguzi sehemu ulizozitaja ndo utajua....
 
Hivi unafikiri watanzania unaowaaandikia wasome mawazo yako wanaufinyu wa kuelewa kama wewe?...unamwandikia mtu wa darasa la ngapi?...watanzania wana uelewa wa kutosha....labda kama umeandika kuwaridhisha waajiri wako....
 
Dodoma umedanganya.... Muulize spika wenu akupe data vizuri.... kesi zilizomahakamani haziwezi kueleza ukweli wa siasa zinavyoenda... kumbuka hapo ni hakimu, mashaidi na mawakili tu... acha ukibaraka..
 
Ccm bila mapolis, tbcc, na virushwa haiendi, ccm ni chama cha wateule kama familia ya kikwete, mkapa, membe, sitta na mafisadi wenzao! Ccm ni janga la kitaifa!
 
Dodoma umedanganya.... Muulize spika wenu akupe data vizuri.... kesi zilizomahakamani haziwezi kueleza ukweli wa siasa zinavyoenda... kumbuka hapo ni hakimu, mashaidi na mawakili tu... acha ukibaraka..
Wewe ni mvibu wa kuelewa: Kuwa mwerevu ni jimbo lipi mkoani Dodoma lililo chini ya Chadema:

CCM inaongoza Dodoma Mjini, Mtela, Kongwa, Mpwapwa, Bahi, Kondoa nk. Waambie viongozi wako wabadili mikakati ya kisiasa vinginevyo mtaishia kugombana na Ndugai na Makinda bungeni badala ya kueneza chama chenu vijijini
 
Mafilili hoja zako huwa zinanicheeekesha vibaya saana, hivi nikweli kuna watu wanalamba mshiko limumba? Lakini mtu anaye toa mshiko inabidi awe anachagua hoja, Hata hii! Kuna hoja za watu kama Ritz, na chama japo ni magamba angalau wanagusa kidoogo!

Hivi unafikiliaga kabla hujaandika? au wewe na sumu ni mtu mmoja? una elimu gani? uelewa wako ni kwa kiwango kipi? nakushauri anza kujisomea vitabu viingi kabla hujaanza kutunga haya mambo yako, utapanua mawazo kidoogo! manaake unatoaga pointless mshikaji, za kiwango cha nobel!
 
CCM na MACCM yote yameshakufa zamani KIKWETE akitembea siku hizi ana magari ya ulinzi wa mapolisi kumi ndio raisi wa kwanza Tanzania kuishi mafichoni haijawahi kutokea
 
Hv hizi mahakama kuwarudishia wabunge wenye kesi ubunge wao tena kwa kasi na mfululizo imetokea tuu au kuna aibu inakimbiwa chaguzi zikirudiwa??????????????????
 
Hili jukwaa limevamiwa,hivi huyu bougy naye ni Great thinker?.
 
Sidhani kama umeushirikisha vema ubongo wako wakati unaweka hili bandiko hapa jukwaani mkuu.
Hivi CCM inawatetea ama ina Watanzania gani upande wake ikiwa kila kukicha inazidi kuwa kandamiza na kuwamaliza kabisa kila wanapojaribu kufurukuta?
Laiti ingelikuwa upande wa Watanzania wabunge wake wake wasingekuwa wanatetea matendo maovu yanayotendwa na serikali yao, isingebariki na matendo maovu yanayofanywa na taasisi na vyombo vya dola dhidi ya Wanzania masikini.

Laiti ingelikuwa na Watanzania isingeasisi UDINI nchini ili kuwagawa na kuwachonganisha Watanzania ili wao waendelee kutawala.
Wangelimchukulia hatua katibu wao mkuu anayehusikia kwenye kashfa za biashara za meno na penmbe za ndovu wetu na hivyo kuuhujumu uchumi wa Taifa ili.

Laiti wangelikuwa na Watanzania wasingeua mfumo wa elimu, ama wasingethubutu kufuta matoke ya mtihani na kisha kuyarekebisha ili tu waonekane watoto wetu hawakufanya vibaya na kuficha udhaifu wa serikali yao katika kusimamia na kuendesha sekta hiyo hapa nchini...JIULIZE TU WANAFANYA HIVYO KWA MASLAHI YA NANI?

Haya na mengine mengi ambayo sijayaorodhesha hapa (ambayo wewe unayafahamu fika!), yanatuonesha wazi kuwa CCM haiko na WATANZANIA wala haipo madarakani kwa maslahi mapana ya WATANZANI. bali iko kwa maslahi ya wateule wachache (ambao pia wewe unawafahamu)
 
Kuitetea CCM ya sasa lazima uwe umepiga bange ukashushia na viroba 2 kwanza!!!
 
Back
Top Bottom