Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,635
- 6,529
Mnisamehe kwa title ila ukishansoma vizuri utanielewa.
Naamini baadhi yenu mmeshawahi ku negotiate bei ya kitu fulani kutoka kwa wachuuzi wa Kariakoo au sehemu zingine au hata wale wanaouza bidhaa zao barabarani. Au labda hata wewe umewahi kuitumia wakati unauza kitu fulani. Kuna mbinu hii kitaalamu inaitwa 'positional bargaining'.
Mbinu hii inayotumika sana kwenye mauzo ya namna hii ni kwa muuzaji kuanza na bei ya juu kuliko uhalisia, kwa lugha nyingine ni from an extreme position. Wakati huo huo ukikutana na mnunuaji anayejielewa na yeye atataja bei yake iliyo chini kuliko uhalisia. Mambo yakienda sawasawa na wote wawili wakiwa na nia kabisa ya kufunga dili, hatimaye watafikia makubaliano ya bei ambayo ipo katikati na wote wataondoka wakiwa wameridhika.
Katika masuala ya Katiba na mabadiliko mbalimbali ya kisiasa ikiwemo sheria za Uchaguzi, CCM ni muuzaji. Sisi wananchi kama wanunuzi tumeitamkia bei wakati ule wa rasimu ya Warioba, unaweza kusema chini kuliko uhalisia (kwa mtazamo wao wanaona ni hivyo kwa sababu ilikuwa inatishia hali waliyozoea na kuitegemea).
Baada ya kutafakari CCM wamekuja na bei yao. Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema wame 'double down' ambayo ni juu kuliko uhalisia. Huyu muuzaji, CCM, anasema kwanza hata kuuza kwenyewe hataki, pamoja na kwamba unaona vumbi limemjaa hadi utosini na hajala siku mbili.
Kwa mliowahi kukumbana na muuzaji wa namna hii ulifanya nini hadi akakubaliana na bei uliyomtajia au at least iliyokuwa nafuu kwako ukachukua mzigo?
Naamini baadhi yenu mmeshawahi ku negotiate bei ya kitu fulani kutoka kwa wachuuzi wa Kariakoo au sehemu zingine au hata wale wanaouza bidhaa zao barabarani. Au labda hata wewe umewahi kuitumia wakati unauza kitu fulani. Kuna mbinu hii kitaalamu inaitwa 'positional bargaining'.
Mbinu hii inayotumika sana kwenye mauzo ya namna hii ni kwa muuzaji kuanza na bei ya juu kuliko uhalisia, kwa lugha nyingine ni from an extreme position. Wakati huo huo ukikutana na mnunuaji anayejielewa na yeye atataja bei yake iliyo chini kuliko uhalisia. Mambo yakienda sawasawa na wote wawili wakiwa na nia kabisa ya kufunga dili, hatimaye watafikia makubaliano ya bei ambayo ipo katikati na wote wataondoka wakiwa wameridhika.
Katika masuala ya Katiba na mabadiliko mbalimbali ya kisiasa ikiwemo sheria za Uchaguzi, CCM ni muuzaji. Sisi wananchi kama wanunuzi tumeitamkia bei wakati ule wa rasimu ya Warioba, unaweza kusema chini kuliko uhalisia (kwa mtazamo wao wanaona ni hivyo kwa sababu ilikuwa inatishia hali waliyozoea na kuitegemea).
Baada ya kutafakari CCM wamekuja na bei yao. Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema wame 'double down' ambayo ni juu kuliko uhalisia. Huyu muuzaji, CCM, anasema kwanza hata kuuza kwenyewe hataki, pamoja na kwamba unaona vumbi limemjaa hadi utosini na hajala siku mbili.
Kwa mliowahi kukumbana na muuzaji wa namna hii ulifanya nini hadi akakubaliana na bei uliyomtajia au at least iliyokuwa nafuu kwako ukachukua mzigo?