CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Ikungi kimelaani vikali vitendo vilivyofanywa na baadhi ya vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa kata ya Puma ya kuiba bendera za chama hicho zilizokuwa zimetundikwa na kupepea kwenye milingoti yake.
Akithibitisha kutokea kwa wizi huo,Katibu mwenezi wa Chadema wa jimbo la Singida magharibi,Bwana Yohana Anthoni alisema kuwa tukio hilo lilitokea katika kata ya Puma,wilayani Ikungi usiku wa kuamkia mei,21,mwaka huu.
Aidha katibu mwenezi huyo alifafanua kuwa siku ya tukio
Usiku wa kumkia mei,21 watu wanaodhaniwa kuwa ni vijana wa chama cha mapinduzi (CCM) kwa kutumiwa na viongozi wa chama hicho waliiba bendera mbili zilizokuwa zimetundikwa zikipepea kwa viongozi wa chama hicho kata ya Puma.
Kwa mujibu wa Bwana Anhoni bendera moja iliyokuwa imetundikwa katika Kijiji cha Nkuninkana,kwenye eneo la Maina lililopo katika kituo cha kuuzia miwa ilinusurika kungolewa na vijana hao baada ya mlinzi aliyekuwa akilinda duka lililokuwa karibu na shina ilipokuwa bendera hiyo.
Hata hivyo inasemekana kwamba baada ya mlinzi huyo kuwaona vijana hao ingawa hakuweza kuwatambua kwa majina,walimwomba awaache waondoke nayo bendera hiyo,lakini mlinzi huyo hakuwa tayari kuwaruhusu vijana hao kufanya wizi na ukatili huo.
Anafafanua katibu mwenezi huyo kwamba baada ya mlinzi huyo kutokuwa tayari kuruhusu wizi huo na ambao ni uvunjaji wa sheria za vyama vya siasa vilivyosajiliwa kisheria,ndipo vijana hao wa chama tawala walipoamua kuondoka na kuiacha bendera hiyo ikipepea.
Hata hivyo alipotakiwa kueleza ni sababu zipi zilizowafanya hadi vijana hao wafikie maamuzi hayo,Bwana Anthoni alisisitiza kuwa hali hiyo ilikuwa ikitaka kumdanganya katibu mkuu wa CCM Taifa,Bwana Abdurahmani Kinana kuwa maeneo hayo hayana viongozi wa vyama vya upinzani zaidi ya ccm peke yake.
Katibu mwenezi huyo hata hivyo alisema mara baada ya tukio hilo wameshatoa taarifa kwenye kituo kidogo cha polisi Puma ambao nao wamewaahidi kuwachukulia hatua wahusika watakapobainika na kwamba baada ya kufanya mawasiliano na OCD wameshapandisha bendera zingine kwenye Kijiji hicho.