PSALM_1
JF-Expert Member
- Jan 1, 2013
- 289
- 100
Salaam wana JF
Angalizo dogo kwa wana mageuzi.
CCM wanaihujumu CHADEMA kwenye level ya juu zaidi kuliko CHADEMA wanavyofikiria. Inaonekana intelijensia ya CHADEMA inai- underestimate intelijensia ya CCM, kitu ambacho si sahihi, na kinaweza kuigharimu CHADEMA.
Inavyoonekana CCM ina watu ndani ya CHADEMA, na ni watu ambao wanaaminika sana ndani ya CHADEMA, na hao watu wamefanikiwa ku pretend na kuonekana ni very loyal kwa uongozi wa juu wa CHADEMA. Na hawa watu pia huwazushia kashfa wenzao/watendaji ndani ya chama na kuwachongea kwa wakuu wa chama, ili wafukuzwe au wawe demoted. Na wanafanya haya yote na mengine mengi tusioyajua kukivuruga chama, huku wakuu wa chama wakidhani kwamba watu hao wana nia ya kukijenga chama. Na hawa watu kwa namna moja au nyingine watahusika siku za baadae kwenye uvujaji wa mipango ya ndani ya chama, na hii inaweza kuwapa CCM urahisi wa kujua ni jinsi gani ya kui-slow down CHADEMA.
Kitendo cha ile clip ya afisa usalama wa juu kabisa wa CHADEMA kuwafikia CCM, regardless imelishwa maneno au la, kimeonyesha udhaifu mkubwa uliopo ndani ya usalama wa chadema. Na bado hatujui pengine kuna vingine vinakuja.
Inachukua hata mwaka kumshawishi mtu kujiunga na chama, lakini inachukua sekunde moja tu kumpoteza mwanachama.
Ushauri wangu kwa uongozi wa juu, na kwa wanachama, na kwa wafuasi wa chadema ni kuwa makini sana na mbinu chafu za wapinga mageuzi, hawa watu kila siku wanatafuta mbinu mpya.
Tusiwape mwanya wakatupelekesha mchakamchaka mpaka tukaomba dakika ya 90(2015) ifike haraka kwa sababu tumechoka, ila tuwapeleke wao mchakamchaka na tufike dakika ya tisini bado tuko fit na wao wawe taabani.
Angalizo dogo kwa wana mageuzi.
CCM wanaihujumu CHADEMA kwenye level ya juu zaidi kuliko CHADEMA wanavyofikiria. Inaonekana intelijensia ya CHADEMA inai- underestimate intelijensia ya CCM, kitu ambacho si sahihi, na kinaweza kuigharimu CHADEMA.
Inavyoonekana CCM ina watu ndani ya CHADEMA, na ni watu ambao wanaaminika sana ndani ya CHADEMA, na hao watu wamefanikiwa ku pretend na kuonekana ni very loyal kwa uongozi wa juu wa CHADEMA. Na hawa watu pia huwazushia kashfa wenzao/watendaji ndani ya chama na kuwachongea kwa wakuu wa chama, ili wafukuzwe au wawe demoted. Na wanafanya haya yote na mengine mengi tusioyajua kukivuruga chama, huku wakuu wa chama wakidhani kwamba watu hao wana nia ya kukijenga chama. Na hawa watu kwa namna moja au nyingine watahusika siku za baadae kwenye uvujaji wa mipango ya ndani ya chama, na hii inaweza kuwapa CCM urahisi wa kujua ni jinsi gani ya kui-slow down CHADEMA.
Kitendo cha ile clip ya afisa usalama wa juu kabisa wa CHADEMA kuwafikia CCM, regardless imelishwa maneno au la, kimeonyesha udhaifu mkubwa uliopo ndani ya usalama wa chadema. Na bado hatujui pengine kuna vingine vinakuja.
Inachukua hata mwaka kumshawishi mtu kujiunga na chama, lakini inachukua sekunde moja tu kumpoteza mwanachama.
Ushauri wangu kwa uongozi wa juu, na kwa wanachama, na kwa wafuasi wa chadema ni kuwa makini sana na mbinu chafu za wapinga mageuzi, hawa watu kila siku wanatafuta mbinu mpya.
Tusiwape mwanya wakatupelekesha mchakamchaka mpaka tukaomba dakika ya 90(2015) ifike haraka kwa sababu tumechoka, ila tuwapeleke wao mchakamchaka na tufike dakika ya tisini bado tuko fit na wao wawe taabani.