Manjagata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2012
- 16,526
- 18,608
Sasa hivi chama kinapumlia mashine, hii ni baada ya ujio wa Pombe aina ya "Mapuya" Joseph Magufuli hapa Shinyanga na kujifanya hamnazo na kujikuta akiropoka mbele ya kadamnasi kwamba kuna watu mchana ni CCM na usiku ukiingia wanahamia UKAWA. Katika mkutano wake huo alimtaja Gasper Kileo (GAKI) kama msaliti. Siku hiyo almanusura mkutano uingie dosari. Sasa kwa vile GAKI amekuwa mfadhili wa ccm kwa muda mrefu, kitendo cha kutajwa hadharani kama msaliti kimemwumiza sana pamoja na wapambe wake, hivyo wamekuwa na roho ya kinyongo kwa mgombea ubunge wa jimbo la Shinyanga town kupitia ccm.
Mtifuano huo ndani ya ccm ni faraja kubwa sana kwa UKAWA na ni ishara wazi kabisa kwamba jimbo hili ni la UKAWA, ije mvua, lije jua!! Masele hana chake na hii inachagizwa na mtifuano uliopo ndani ya ccm na umahiri wa kujieleza wa mgombea wa UKAWA kupitia CHADEMA (Patrobas "Mzimu wa Shelembi" "Sauti ya Zege" Katambi). Naomba hili jimbo liorodheshwe kwenye majimbo ambayo UKAWA tayari wameshajihakikishia ushindi.
Asante YESU kwa kuyafanya haya yatimie!!!
Mtifuano huo ndani ya ccm ni faraja kubwa sana kwa UKAWA na ni ishara wazi kabisa kwamba jimbo hili ni la UKAWA, ije mvua, lije jua!! Masele hana chake na hii inachagizwa na mtifuano uliopo ndani ya ccm na umahiri wa kujieleza wa mgombea wa UKAWA kupitia CHADEMA (Patrobas "Mzimu wa Shelembi" "Sauti ya Zege" Katambi). Naomba hili jimbo liorodheshwe kwenye majimbo ambayo UKAWA tayari wameshajihakikishia ushindi.
Asante YESU kwa kuyafanya haya yatimie!!!