CCM, Polisi, Magazeti na Redio lao moja

CCM, Polisi, Magazeti na Redio lao moja

Lendapa

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2014
Posts
201
Reaction score
37
Najitokeza kueleza kero yangu na hasa kuwashitaki polisi,CCM na baadhi ya vyombo vya habari kama magazet na redio.

Nawaandikia ninyi nguvu ya umma kupitia jf,kuwa katika vurugu zinazoendelea katika kata 27 za kampeni ya uchaguzi,watz hasa CHADEMA,wamekuwa wakipigwa mapanga,lakini polisi na vyombo vya habari vikapiga kimya.

Waheshimiwa nguvu ya uma,haya yametokea Arusha,watu wamepigwa mapanga,wahalifu wa CCM wakatajwa lakini polisi wakawalinda badala ya kuwakamata.

CCM wamekuwa wakijua na kushiriki kwa hili,kwan kwenye mkutano wao wa ufunguzi Arusha,walisema watashinda hata kwa kuua,kwenda kwa waganga au kununua shahada.

Kule Bunda kata ya Nyasura,katibu wa CCM aliwaleta askari wa JKT kama 30 hivi kuwapiga na kujeruhi watu ili waonekane ni CHADEMA, si polisi,wala vyombo vya habari vilivyokemea hilo.

Cha kushangaza,eti kule Kahama,polisi wamepiga watu,lakini vyombo vya habari vikaripoti tena kwa kuwataja CHADEMA kuwa ndo wahusika.
Polis hajawakamata waliofanya hivo zaidi ya kumkamata mbunge wa CHADEMA na kumhoji.

Polis hamko fair na haki ya Mungu nawashitaki kwa nguvu ya umma.Kote CCM wanakopiga watu ni dalili kuwa watashindwa uchaguzi.

Ndg nguvu ya umma,hivi inaingia akilini,wavamizi wapasue gari vioo,wawapige watu mapanga,polisi mpo wapii? Kazi yenu ni nin nini?

Halafu mbona haya mapanga yamewapata tu raia wetu kichwa na mikono? Hivi ukatwe panga la kichwa jana,halafu leo ukasimama na kuongea? Mbona si nesi,wala daktari anaeonekana akiwatibu hao watu? Iweje vyombo vya habar vipige picha wagonjwa bila docta kuwa hapo?

Sasa tumechoka,nasema tumechoka,' polisi na CCM lenu moja,nasema fanyen hivi lakini siku ipo ambapo nguvu ya umma haitavumilia tena.

Naishia hapa,ila wana nguvu ya uma je hii ni haki?

Wenu katka mapambano,

lendapa
 
Mkuu tukuamini vipi make watu kama nyie ndiyo wafanya fujo namba moja halafu mnakimbilia kutengeneza uongo.
 
Lendapa
slp 276
Arusha.
6.2.2014
Nguvu ya uma tz
slp 1
jamii forum.
Ndg;
yah; uonevu wa polis na ccm

wana jf,rejea kichwa cha habar hapo juu.najitokeza kueleza kero yangu na hasa kuwashitaki polis,ccm na baadhi ya vyombo vya habar kama magazet na redio.
Nawaandikia niny nguv ya uma kupitia jf,kuwa katk vurug zinazoendelea katka kata 27 za kampen ya uchaguz,watz hasa chadema,wamekuwa wakipigwa mapanga,lakin polis na vyombo vya habar vikapiga kimya.
Waheshimiwa nguvu ya uma,haya yametokea Arusha,watu wamepigwa mapanga,wahalif wa ccm wakatajwa lakin polis wakawalinda badala ya kuwakamata...
Ccm wamekuwa wakijua na kushiriki kwa hili,kwan kwenye mktn wao wa ufunguz arusha,walisema watashinda hata kwa kuua,kwenda kwa waganga au kununua shahada.
Kule bunda kata ya nyasura,katb wa ccm aliwaleta askar wa jkt kama 30 hiv kuwapiga na kujeruh watu ili waonekane ni chadema, si polis,wala vyombo vya habar vilivyokemea hilo.
Cha kushangaza,et kule kahama,polis wamepiga watu,lakin vyombo vya habar vikarpot tena kwa kuwataja chadema kuwa ndo wahusika.
Polis hajawakamata waliofanya hivo zaid ya kumkamata mb wa chadema na kumhoji..
Polis hamko fare na haki ya Mungu nawashtak kwa nguvu ya uma.kote ccm wanakopiga watu ni dalili kuwa watashindwa uchaguzi.
Ndg nguv ya uma,hiv inaingia akilin,wavamiz wapasue gar vioo,wawapige watu mapanga,polis mpo wapii? Kazi yenu ni nin nin?
Halaf mbn haya mapanga yamewapata tu raia wetu kichwa na mikono? Hv ukatwe panga la kichwa jana,halaf leo ukasimama na kuongea? Mbona si nesi,wala daktar anaeonekana akiwatibu hao watu? Iweje vyombo vya habar vipige picha wagonjwa bila docta kuwa hapo?
Sasa tumechoka,nasema tumechoka,' polis na ccm lenu moja,nasema fanyen hiv lakin cku ipo ambapo nguv ya uma haitavumilia tena,..
Naishia hapa,ila wana nguvu ya uma je hii ni haki?

Wenu katka mapambano,

lendapa
Fanyeni huo upuuzi wenu lakini mwisho wenu utakuwa mbaya sana kuuwa na kutesa watu mnaona ni ishu halafu leo unavimba mashavu unadai eti polisi wanawaonea kwahiyo mnataka kuachwa mfanye ujinga bila kudhibitiwa.
 
Nilivyo ziona tu zile picha kwenye huo uzi wa Kahama na story yenyewe ilivyo andikwa (haikutaja chanzo cha fujo, kwanini wafuasi wa CDM walianzisha fujo) nikajua tu moja kwa moja hi kitu imepikwa, na nilipoona mtu wa kwanza ku-comment ni mwana wa mfalme anf bimkubwa FF na zemarcopolo wame like nika join dots, nikaupitiliza ule uzi. "You can fool some people sometimes but you can't fool all the people all the time" By Bob Marley and the wailers!
 
mungu atunusuru na machafuko kuna wanao yatamani. Chonde chonde siasa isituondolee undugu na ubinadamu wetu watz
 
Mkuu malipo yote ya uhafu ni hapa hapa duniani waache waendelee na uhalifu Wao, watu tunajiuliza,kwanini wanapopigwa wafuasi wa cdm hakuna anaye kamatwa Bali akipigwa mfuasi wa ccm wanakamatwa viongozi na wafuasi wa Chadema huu ni uhuni uliopitiliza

Ndipo tunajiuliza hivi kwanini walipiga marufuku baada ya Cdm kutangaza itafanya mafunzo ya ukakamavu kwa kikundi chake cha redbriged nchi nzima ili iweze kujilinda na unyama unaofanywa na ccm kupitia kundi la greenguard,kumbe ilikuwa nikutoa nafasi kwa kundi hilo kujiimarisha.
Na haya tunayo yaona yakitokea Nchi nzima ni matokeo ya kikundi hicho kunacholelewa na watawala wa Nchi hii.
 
Mkifanya vurugu lazima mkamatwe mshitakiwa, tanzania haitavurugwa na watu au kikundi cha watu wenye ulafi wa madaraka, chadema hizo damu za watu mnazomwaga kila siku mnazinywa au mnatambikia?, mungu hata waacha kamwe, lazima mtajibu tuu, damu za watanzania hazita mwagwa hivi tuu. Lazima sheria ichukue mkondo wake?
 
Mkuu tukuamini vipi make watu kama nyie ndiyo wafanya fujo namba moja halafu mnakimbilia kutengeneza uongo.

Acha utaahira wewe hivyo vi 7000 vinawapa kiburi watu tunapigwa na mapoliccm unaropoka 2mechoka na tutajihami wenyewe
 
Fanyeni huo upuuzi wenu lakini mwisho wenu utakuwa mbaya sana kuuwa na kutesa watu mnaona ni ishu halafu leo unavimba mashavu unadai eti polisi wanawaonea kwahiyo mnataka kuachwa mfanye ujinga bila kudhibitiwa.

polis hawatawasaidia kitu zaidi ya kuchukiwa tu na wananchi,maeneo yote mnayotumia kutisha watu na kufanya fujo yote mtashindwa vibaya,watz wa leo wanajitambua na watawaadhibu siku ya kura! hiicmbinu ilishakuwa zilipendwa,pigeni propaganda navhizo siasa zenu nyepesi lakn kumbukeni wananchi wa maeneo husiks wanaona na wanawajua wafanya fujo hivyo hawahitaji kusimuliwa na vyombo vyenucvya propaganda matukio wanayoyashuhudia kwenye maeneo yao!
 
Fanyeni huo upuuzi wenu lakini mwisho wenu utakuwa mbaya sana kuuwa na kutesa watu mnaona ni ishu halafu leo unavimba mashavu unadai eti polisi wanawaonea kwahiyo mnataka kuachwa mfanye ujinga bila kudhibitiwa.

Dalili ya mvua ni mawingu, huu mchezo unaochezwa na CCM ni mbinu za nchi za mashariki siku za nyuma kuendelea kubaki madarakani. Ila sisi watanzania tunaona nini kinaendealea, wewe utabaki unapiga propaganda hapa jukwaani ni kweli si tatizo kwa sasa ila iko siku watu watachoka na wataamua kuchukua hatua ambayo matokeo yake yatakuwa hasi. Nasikitika kwa jeshi la polisi kushindwa kutekeleza wajibu wao itakuja siku watatamani watu watii sheria haitawezekana maana watu watawaona kama mawakala wa ccm. Mchelea mwana kulia hulia yeye.

Na tatizo lingine ninaloliona hapa ni huu mfumo wa Rais kuwa juu ya sheria yaani hashitakiwi na wakati huohuo yeye ndio mteule wa hawa maboss wote wa vyombo vya dola, iwapo rais atakuwa anaegemea kuhakikisha chama chake kinabaki madarakani basi utaratibu mzima wa kufuatwa sheria utakuwa na makengeza. Sisi watanzania hatupendi vita tunataka amani na ushindani ulio huru ambao watu wote kuanzia Rais wawe chini ya sheria na yoyote atakayekiuka sheria basi mkondo wake uchukue nafasi.

Lakini hiki kinachoendelea sasa, ni ugonjwa uleule wa viongozi wengi wa nchi za kiafrika kulazimisha kubakia madarakani hata kama damu inamwagika. Hatuombi vita kutokea lakini huko tuendako naona viongozi wa vyama vya upinzani kupoteza uvumilivu na kuambua liwalo na liwe, hapo ndio patatuchukua muda kurudi kwenye hali yetu ya kawaida ya utulivu na amani. Haiwezekani kama hapa Arusha vijana wanaotumiwa na CCM ni wale wanajulikana na uhalifu ndio wanajeruhi watu kwenye mikutano ya kampeni na polisi wakiwepo bila kuchukuliwa hatua. Na mkumbuke watu wanaona na wapinzani wanashitaki kila mara lakini hatua stahiki hazichukuliwi. Narudia tena mchelea mwana kulia hulia yeye, tusiombe watu wakasema liwalo naliwe.
 
Wakamatwe tu hao CHADEMA maana tumechoka. Wanamwaga damu za watu
 
mkifanya vurugu lazima mkamatwe mshitakiwa, tanzania haitavurugwa na watu au kikundi cha watu wenye ulafi wa madaraka, chadema hizo damu za watu mnazomwaga kila siku mnazinywa au mnatambikia????, mungu hata waacha kamwe, lazima mtajibu tuu, damu za watanzania hazita mwagwa hivi tuu. Lazima sheria ichukue mkondo wake????

Ndugu yangu fanya utani na dhihaka lakini utajutia huu mchezo wa kipumbavu unaofanywa na CCM iko siku watu wataacha kutii hizo sheria mtatamani wangalau hao viongozi mnaowatukana wawatulize wananchi wao. Yetu macho. Nchi yetu ni maskini sana japo ina utajiri wa maliasili. Ni bora ungejikita huko kwenye kuelimisha na kuwataka wananchi wazalishe mali na sio hizo mbinu za ushindi wa kipumbavu. Sisi watanzania sio mara moja tunaona kila uchaguzi wanachama wa upinzani wakiumizwa na kuswekwa rumande na wanaowaumiza na wanachema wa ccm kwa kutumia mbinu za nchi za ulaya mashariki ya zamani. Tushukuru tu watanzania bado walio wengi wana hofu ya chama dola lakini kila kinachofanyika wanaona na hata hao wana ccm wenye busara wanaona na kubaki vinywa wazi. Tuombe asitokee kiongozi awaambie wanachama wake wajitetee na kufanya lolote.
 
Tunajua CCM imezidiwa kila idara, wamebaki na vyombo vya usalama tu hasa Jeshi la Polisi.

Vyombo vya habari vingi ni mateka wa siasa za makundi ndani ya ccm vipo vipo tu,badala ya kumpasha Mwananchi habari za kweli vinampotosha na kumuaminisha sivyo.
 
Waacheni wao na polisi yao na media zao lakini sie tuko Pamoja Daima,tutawanyoosha tu kwenye kura mpaka wakubali mziki wa CDM

Hata wafanyeje kuizuia CDM ni sawa na kuyazuia maji ya mto Amazoni kwa mchanga na huko mnakofanya hira ndo mnakoanza kushindwa kwanza
 
Hivi kuna organ ndani ya usalama ambayo inalaumiwa sana kupita polisi?
 
ifikie hatua jeshi la polisi liache kufanya double standard mbona inapotokea wafuasi na viongozi wa chadema wanapovamiwa na kupigwa na makada wa ccm hatuoni hatua zozote zikichukuliwa lakini ikitokea makada wa ccm kupigwa tunaona hatua zinachukuliwa mara moja
 
Back
Top Bottom