Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,169
- 48,451
Kwa jinsi inavyoonekana ni kama vile chama chote cha Mapinduzi kinafanya kila kitu si kwa maslahi ya Tanzania bali ili kuonesha kwamba Tundu Lissu hayuko sahihi kwa hoja anazozitetea.
Nakumbuka tangu enzi bunge linaendeshwa na Anne Makinda sheria nyingi za hovyo zilipitishwa kwa kuonesha "serikali" iko sahihi na Lissu kakosea.
Lissu inawezekana kachukua nafasi ya Dr. Slaa wa "enzi zile" ambapo alipingwa na CCM kwa kila jambo alilolifanya.
Hata Leo Lissu yuko kitandani Hospitalini Nairobi anaumwa, naona harakati zinazofanywa kushindana naye. Hata yale aliyoyasimamia leo yanapotoshwa kwamba aliyapinga.
Lissu inawezakana watu wengine wanaona ni "mropokaji" lakini CCM ndiyo wanaoijua nguvu yake. Kila mwaka akigombea kwenye jimbo lake CCM huweka nguvu ya ziada na mkazo usio wa kawaida ingawa siku ya mwisho anayeibuka mshindi ni Lissu.
Nguvu ya CCM ni watu kukaa kimya, lakini ni chama dhaifu sana linapokuja suala la watu kuikosoa hadharani. Kuna wakati walitumia kuita watu kuwa si watanzania ili kuwatia hofu, sasa wamekuja na silaha nyingine kuwaita watu wasaliti na si wazalendo.
CCM nzima kuanzia kamati Kuu yake mpaka kwa balozi wao wa mtaani kwetu na kwenu, wako bize kuipaka matope haiba ya Lissu na kutaka kumfanya ni adui wa watu na maendeleo ya taifa.
Ninachojifunza CCM ni chama kilichokufa bali uwepo wake unategemea uhai wa kuazima toka kwenye vyombo vya dola. CCM wajue wanafanya kazi ya kuendesha serikali yetu kwa niaba ya watanzania wote na si kwa faida ya chama chao.
Nakumbuka tangu enzi bunge linaendeshwa na Anne Makinda sheria nyingi za hovyo zilipitishwa kwa kuonesha "serikali" iko sahihi na Lissu kakosea.
Lissu inawezekana kachukua nafasi ya Dr. Slaa wa "enzi zile" ambapo alipingwa na CCM kwa kila jambo alilolifanya.
Hata Leo Lissu yuko kitandani Hospitalini Nairobi anaumwa, naona harakati zinazofanywa kushindana naye. Hata yale aliyoyasimamia leo yanapotoshwa kwamba aliyapinga.
Lissu inawezakana watu wengine wanaona ni "mropokaji" lakini CCM ndiyo wanaoijua nguvu yake. Kila mwaka akigombea kwenye jimbo lake CCM huweka nguvu ya ziada na mkazo usio wa kawaida ingawa siku ya mwisho anayeibuka mshindi ni Lissu.
Nguvu ya CCM ni watu kukaa kimya, lakini ni chama dhaifu sana linapokuja suala la watu kuikosoa hadharani. Kuna wakati walitumia kuita watu kuwa si watanzania ili kuwatia hofu, sasa wamekuja na silaha nyingine kuwaita watu wasaliti na si wazalendo.
CCM nzima kuanzia kamati Kuu yake mpaka kwa balozi wao wa mtaani kwetu na kwenu, wako bize kuipaka matope haiba ya Lissu na kutaka kumfanya ni adui wa watu na maendeleo ya taifa.
Ninachojifunza CCM ni chama kilichokufa bali uwepo wake unategemea uhai wa kuazima toka kwenye vyombo vya dola. CCM wajue wanafanya kazi ya kuendesha serikali yetu kwa niaba ya watanzania wote na si kwa faida ya chama chao.