CCM ni ya nani?

CCM ni ya nani?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Kuna msemo unasema CCM ina wenyewe, hao wenyewe ni akina nani?

Kila kikundi/chama kina waanzilishi wake ambao ndio huwa Na sauti Na heshima kubwa mbele au nyuma ya pazia. Sauti Na heshima hizo huwa zinarithishwa kwenye kizazi cha waanzilishi hao. Chadema, NCCR, ACT, Chauma, NRA, TLP, nk vinafahamika waanzilishi wake Na wanayo sauti Na heshima kubwa kwenye taasisi hizo. Waanzilishi wa TAA iliyozaa TANU iliyozaa CCM na CCM yenyewe ni akina nani? wapo? watoto na wajukuu wao wapo? Wana sauti na heshima kwenye CCM?

Nilidhani kuwa CCM ni mali ya Mwl Nyerere, Kawawa, Kingunge, nk lakini siioni familia za Mwl Nyerere, kingunge, Kawawa, Rupia au nani wakiwa nyuma au mbele kwenye CCM.

Nyerere alisemaga kuwa CCM sio baba wala mama yake, angeweza kuachana nacho akimaanisha kuwa CCM INA wenyewe ambao sio yeye, kingunge aliikimbia CCM, na akina Mzee Makamba, Kinana, Nape, Polepole, Bashiru, malecela, Kolimba, na wengine wengi ambaao walionekana kuwa labda ndiyo baadhi ya wenye CCM nao kuna wakati walikutana na alichokutana nacho mtema kuni ndani ya CCM kuonyesha kuwa wenye ccm, wenye TANU na ASP na wenye TAA wapo lakini wamefichwa kwa makusudi au bahati mbaya kusikojulikana pamoja na familia zao.

Wenye CCM hawaonekani, hawana sauti wala heshima tena ndani ya ccm. CCM imekuwa dude lisilokuwa na mwenyewe linalotumika tu kuingiza watu Ikulu baaasi, likishafika Ikulu linageuka kuwa mmiliki wa CCM kwa 100% na kuwa tishio hata kwa waliokuwa wakidhani kuwa ni wenye CCM kindakindaki. Kundi litamnyoa bila maji yeyote mwenye mawazo mbadala na maslahi yao.

Linaweza kubadilisha chochote kwenye katiba ya CCM na ile ya nchi. Wengine woote kula yenu itategemea utashi na huruma zao hasa kwa vile litawahitaji baadhi yenu wakati wa chchaguzi tena.

Wanaweza kubadilisha katiba na sheria kuruhusu masilahi yao yashamiri na ikiwezekana wabaki madarakani milele. Utawqsikia kwa kupitia wanufaika wakisema "utake usitake tutakuongezea muda"

Wenye TAA, TANU na baadsae CCM na ASP wako wapi? Wanapata nini?
 
Hapo kwenye dude kuubwa!! Hakika halitishii tu!! Ukilisogelea kwenye anga zake ndoutajua hujui!

img_1_1640114134963.jpg
 
Chama ni taasisi ya umma, haina mwenyewe japo wenye nguvu ya ushawishi ndani ya chama hujitwika umiliki bandia.
 
Wanaosema kina wenyewe, wanadhani wakifa watoto wao watakuwa na haki ya hatimiliki kisheria?!
 
... kinajiita chama cha wakulima na wafanyakazi! Kwani kuna wengine zaidi ya hao?
Akina Nape, Polepole, Mzee Makamba, Kinana, Msindai, Malecela, nk kuna wakati walitaka kudhani CCM inawahusu sana wakajikuta kumbe sivyo.
 
chama ni taasisi ya umma, haina mwenyewe japo wenye nguvu ya ushawishi ndani ya chama hujitwika umiliki bandia.
Vyama vyoye duniani vina nafasi ya waanzilishi wa vyama. Watoto na wajukuu na hata vilembwe wa waanzilishi wanatayalishwa (groomed) kwenye chama muda wote wa uhai wa chama hicho, hawa ni watu miongoni mwa watu ndani ya chama wanaoweza kutoa ushauri mzito sana ndani ya chama kuhusu chama. CCM kuna wakati ilikuwa inaongozwa na wasioifahamu CCM kabisaa hata kwa kusikia. Watoto na wajukuu wa waanzilishi wa TAA, TANU, CCM na ASP hawajulikani wako wapi na hawanufaiki kwa chochote na hawana sauti. Hawakusomeshwa wala kutayarishwa kuwemo kwenye chama. Hii ni dhambi ya makusudi kabisa.
 
Nape anadhani CCM ni mali ya shemeji yake wa Msoga, ndio maana anasikia raha sana siku hizi.
 
CVM ni kikundi cha watu wachache waliojiharamisha kunufaikana na kodi na raslimali zetu.
 
CCM ni ya wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wanafunzi na raia yeyote wa Tanzania anayetimiza masharti ya kujiunga.

Pia wahamiaji haramu huweza kujipenyeza na kupitia huko hujihalalisha na kupata nguvu kweli kweli.

Hata hivyo, wanachama wengi ni masikini wa mali na fikra, hivyo kuburuzwa na yeyote mwenye nguvu ya madaraka kwa wakati husika.
 
Ccm ni kikundi cha watu wachache waliojiharamisha kunufaikana na kodi na raslimali zetu.
Hao watu ni akina nani? Kwa namna CCM ilivyo leo haina mwenyewe, sio waanzilishi wala wafuasi wake wanaonufaika nayo. Wanaonufaika nayo ni aliyeko madarakani na ndugu na marafiki wa karibu. Punde tu wakishatoka madarakani na wao hawana chao. Unaweza kusema ni chukua chako mapema na wewe uondoke.
 
CCM ni ya wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, wanafunzi na raia yeyote wa Tanzania anayetimiza masharti ya kujiunga.
Pia wahamiaji haramu huweza kujipenyeza na kupitia huko hujihalalisha na kupata nguvu kweli kweli.
Hata hivyo, wanachama wengi ni masikini wa mali na fikra, hivyo kuburuzwa na yeyote mwenye nguvu ya madaraka kwa wakati husika.
Mitaala yetu mashuleni iongezewe somo LA namna ya kufikiri kwa makini, critical thinking. Watu wetu wengi wanaponzwa Na T-shirt Na kofia tu basi
 
Wenye CCM hawaonekani, hawana sauti wala heshima tena ndani ya ccm. CCM imekuwa dude lisilokuwa na mwenyewe linalotumika tu kuingiza watu Ikulu baaasi, likishafika Ikulu linageuka kuwa mmiliki wa CCM kwa 100% na kuwa tishio hata kwa waliokuwa wakidhani kuwa ni wenye CCM kindakindaki. Kundi litamnyoa bila maji yeyote mwenye mawazo mbadala na maslahi yao.
Well said.
 
Kuna msemo unasema CCM ina wenyewe, hao wenyewe ni akina nani?

Kila kikundi/chama kina waanzilishi wake ambao ndio huwa Na sauti Na heshima kubwa mbele au nyuma ya pazia. Sauti Na heshima hizo huwa zinarithishwa kwenye kizazi cha waanzilishi hao. Chadema, NCCR, ACT, Chauma, NRA, TLP, nk vinafahamika waanzilishi wake Na wanayo sauti Na heshima kubwa kwenye taasisi hizo. Waanzilishi wa TAA iliyozaa TANU iliyozaa CCM na CCM yenyewe ni akina nani? wapo? watoto na wajukuu wao wapo? Wana sauti na heshima kwenye CCM?

Nilidhani kuwa CCM ni mali ya Mwl Nyerere, Kawawa, Kingunge, nk lakini siioni familia za Mwl Nyerere, kingunge, Kawawa, Rupia au nani wakiwa nyuma au mbele kwenye CCM.

Nyerere alisemaga kuwa CCM sio baba wala mama yake, angeweza kuachana nacho akimaanisha kuwa CCM INA wenyewe ambao sio yeye, kingunge aliikimbia CCM, na akina Mzee Makamba, Kinana, Nape, Polepole, Bashiru, malecela, Kolimba, na wengine wengi ambaao walionekana kuwa labda ndiyo baadhi ya wenye CCM nao kuna wakati walikutana na alichokutana nacho mtema kuni ndani ya CCM kuonyesha kuwa wenye ccm, wenye TANU na ASP na wenye TAA wapo lakini wamefichwa kwa makusudi au bahati mbaya kusikojulikana pamoja na familia zao.

Wenye CCM hawaonekani, hawana sauti wala heshima tena ndani ya ccm. CCM imekuwa dude lisilokuwa na mwenyewe linalotumika tu kuingiza watu Ikulu baaasi, likishafika Ikulu linageuka kuwa mmiliki wa CCM kwa 100% na kuwa tishio hata kwa waliokuwa wakidhani kuwa ni wenye CCM kindakindaki. Kundi litamnyoa bila maji yeyote mwenye mawazo mbadala na maslahi yao.

Linaweza kubadilisha chochote kwenye katiba ya CCM na ile ya nchi. Wengine woote kula yenu itategemea utashi na huruma zao hasa kwa vile litawahitaji baadhi yenu wakati wa chchaguzi tena.

Wanaweza kubadilisha katiba na sheria kuruhusu masilahi yao yashamiri na ikiwezekana wabaki madarakani milele. Utawqsikia kwa kupitia wanufaika wakisema "utake usitake tutakuongezea muda"

Wenye TAA, TANU na baadsae CCM na ASP wako wapi? Wanapata nini?
Muulize Polepole, Nape, Lowasa, Membe, Kinana, Makamba mzee wanajua CCM ni ya nani
 
Back
Top Bottom