CCM ni kama Cali Cartel

MchunguZI

JF-Expert Member
Jun 14, 2008
4,009
2,171
Narejea maneno haya kwa hali mpya ya sasa. Kwa hali ilivyo sasa kundi la Cartel limekuwa kubwa. Mahakama hazitendi haki, zinashirikiana na waharifu. Polisi hawatendi haki, vituo vimekuwa ni sehemu ya kuokota maiti. Mawaziri ni wezi wanashirikiana na watendaji na wanalindwa hadi Ikulu.

Tunaelekea hali ya Kolombia ambapo Waharifu walikuwa wanafadhili hadi mtu kuwa rais, IGP, CDF na wataalamu wote muhimu ktk nchi.

Je Tanzania tutaendelea kama nchi?


Kwa wale munaofahamu jinsi Cali cartel walivyokuwa wakifanya kazi halamu ya cocaine nchini Colombia ni rahisi kulinganisha mambo yanayofanywa na CCM na kikundi kama hicho. Cocaine iliwahusisha hata wanasiasa, akiwemo Rais Ernesto Samper.

Binafsi siioni tofauti kati ya Cali Cartel na CCM. Ni chama kinachoishi kwa kutumia mbinu chafu. Sasa wanauza ardhi, wanavuna madini, wanabeba pesa za serikali kifisadi, nk. Kwa ujumla sioni tena biashara halali inayofanywa na CCM kuingiza kipato cha kuwawezesha kulipa mishahara ya wenyeviti na makatibu kila Wilaya na bado wakapata pesa za chaguzi ndogo na kununua magari na sasa waingie uchaguzi mkuu.

Taasisi zote za serikali hupata pesa pungufu ya zile zilizopangwa na Bunge kila mwaka lakini hakuna anayeuliza sehemu isiyokuja huenda wapi. Inasikika ni kwenye chama. Yaonekana Bajeti yetu inahudumia serikali mbili, Serikali halisi na hii ya CCM. CCM ni Cartel wa hatari sana! Cali cartel iliangushwa kwa msaada wa America. CCM iko Jeshini, iko polisi, iko mahakamani, na kwa ujumla kila katibu Mkuu wa Wizara lazima awe na kadi ya chama ndo maana wengine walianza kutangaza niya ya kugombea wakiwa bado ni makatibu wakuu. Nani ataiangusha? Nchi gani ya nje itakayoweza kutusaidia kuiondoa wakati tunasifiwa tumetulia na tuna amani?
 
Hakikisheni mna ushahidi wa nguvu ili wapelekwe the hague,huwezi kusaidiwa na serikali nyingine hadi uwe na ushahidi wa kutosha ili mara baada ya hapo wafikishwe mahakamani kwani hapo ndiyo ule usemi wa the end justifies the means unapotake place.
 
Sasa wanauza ardhi, wanavuna madini, wanabeba pesa za serikali kifisadi, nk. Kwa ujumla sioni tena biashara halali inayofanywa na CCM kuingiza kipato cha kuwawezesha kulipa mishahara ya wenyeviti na makatibu kila Wilaya na bado wakapata pesa za chaguzi ndogo na kununua magari na sasa waingie uchaguzi mkuu.


na hii yote imetokana na sera mbovu zilizowekwa na nchi ya kwamba ardhi,madini,mafuta ni mali ya serikali thats why wanafanya watakalo since they are the government,nothing can change the situation until we decide to go liberal,bring equality .............serikali ni mm na ww,tuungane kubadilisha sheria na katiba za nchi kuleta mabadiliko.
Nani ataiangusha? Nchi gani ya nje itakayoweza kutusaidia kuiondoa wakati tunasifiwa tumetulia?

HAKUNA WA KUIANGUSHA CCM,ILA NI SISI WENYEWE NA KURA ZETU NA NIA ZETU NA KUWA NA UTAYARI NA HASA KUJITOA MUHANGA.HATUHITAJI NCHI NGENI MAANA NI SISI WA NDANI NDO TUNAOJUA MACHUNGU YANAYOTUKABILI..........Colombia walisaidiwa sababu madawa yaliharibu wengi,our case is differentour politics kills us while benefiting other nations maswahiba wa CCM!
 
HAKUNA WA KUIANGUSHA CCM,ILA NI SISI WENYEWE NA KURA ZETU NA NIA ZETU NA KUWA NA UTAYARI NA HASA KUJITOA MUHANGA.HATUHITAJI NCHI NGENI MAANA NI SISI WA NDANI NDO TUNAOJUA MACHUNGU YANAYOTUKABILI..........Colombia walisaidiwa sababu madawa yaliharibu wengi,our case is differentour politics kills us while benefiting other nations maswahiba wa CCM!


Njia ya kuiondoa CCM ni mapinduzi ya kijeshi.

Africa ina serikali ambazo hazijafikia kiwango cha kuwa na ‘Red shirt movement' kama ya Thailand. Hakuna ustaarabu wa kiwango hicho ambao ungewezesha mimi na wewe kusema kwamba tuna jukumu la kuwashikisha adabu viongozi wetu. Ukiandamana risasi zitatumika na watu watakufa bila hata viongozi kujuta. Hata Rais anafahamu ndo sababu ya kufikia kutoa hotuba isiyo chagua maneno.

Jinsi CCM walivyojiingiza serikalini ni vigumu kuwaondoa, ni juhudi sawa na ile ya kupindua serikali. Hii imeshaelezwa ni tatizo la nchi mbili Afrika; Tanzania na S. Africa.

CCM huwa hawachaguliwi kushika madaraka, bali huingia kwa sababu Jeshi, polisi wako nyuma yao.

Binafsi sioni njia ya kutokea zaidi ya nguvu za kijeshi ambalo sasa hivi linahongwa marupurupu.


Yaonekana baadhi ya madikteta wana mwelekeo mzuri kuliko viongozi wetu wanaoonekana eti ni wa demokrasia. Iweje madikteta wa Tunisia waone umuhimu wa kuondoka madarakani kuliko Kikwete, hata baada ya kuuwa watu Arusha?
 
Ni muendelezo wa mambo ambayo tumewahi kuyatabiri ndani ya JF. Hisia mpya niliyo nayo ni msaada wa wafadhili wa bajeti yetu. Iweje waendelee kutoa pesa kulipa mishahara ya polisi ambao wanatumika ktk mauaji?

Njia gani tuitumie kufikisha ujumbe kwa hawa wanaoisaidia serikali hii.
 
Mchunguzi umesema kweli tupu, CCM ya sasa imekosa uongozi thabiti, sasa nchi inaongozwa kwa pressure za nje. Muda si mrefu mwenyekiti wa chama atakuja na kusema kuwa Dowans hailipiki na utashangaa ambavyo kila mtu atatoka kumpongeza rais kwa ujasiri na usikivu. Lakini ukweli ni kwamba hata kama Kikwete atapingana na waziri wake na mwansheria mkuu (kama ilivyofanya kwenye suala la katiba) hana nia ya dhati kufanya hivyo na watabuni njia nyingine ya kuiba, usije ukashangaa kusikia kuwa mradi wa makaa ya mawe wa mchuchuma ukawa umechukuliwa kufidia hela zilizotumika kwenye uchaguzi......
 
..............................................Lakini ukweli ni kwamba hata kama Kikwete atapingana na waziri wake na mwansheria mkuu (kama ilivyofanya kwenye suala la katiba) hana nia ya dhati kufanya hivyo na watabuni njia nyingine ya kuiba, usije ukashangaa kusikia kuwa mradi wa makaa ya mawe wa mchuchuma ukawa umechukuliwa kufidia hela zilizotumika kwenye uchaguzi......

Ni jana tu nimesikia kwamba huenda kwa mara nyingine tena dakika za mwisho wazungu watapunguza zaidi ya billioni 900 ktk misaada yao maana hazionekani toka ktk bajeti hii. Huenda zimetumika ktk uchaguzi kinyume na matakwa yao. Hebu tusubiri maana Machi tu lazima waseme muelekeo wa bajeti.
 
Naona kama CCM imekwisha hama toka kwenye Cartel system. Ni 180[SUP]o[/SUP] shift. Upinzani naona umedoda wakati wagombea wote muelekeo ni CCM.
 
Niliwahi kuandika thrd hii siku za nyuma nikiamini kabisa kwamba ndani ya CCM hakuna anayeweza kusema itabadirika. Hali tuliyo nayo inazidi kudhihirisha maandishi yangu maana kwa vitendo tunavyoviona vikifanyika ndani ya chama au na vigogo wa chama sina sababu ya kusema CCM ni chama cha siasa. Chama tawala kinacholinda na kusimamia malipo ya DOWANS, 'adui' wa nchi, aliyeshitaki alipwe.

Sasa tena tunaona eti UVCCM wakijifanya wako upande mwingine wa chama. Hizi ni mbwembwe ili kuonyesha kwamba hayo ya DOWANS hayawahusu CCM. Mwenyekiti wao, Kikwete, yuko wapi???
Naomba niirejee meseji yangu kwa wakati huu.


Kwa wale munaofahamu jinsi Cali cartel walivyokuwa wakifanya kazi halamu ya cocaine nchini Colombia ni rahisi kulinganisha mambo yanayofanywa na CCM na kikundi kama hicho. Cocaine iliwahusisha hata wanasiasa, akiwemo Rais Ernesto Samper.

Binafsi siioni tofauti kati ya Cali Cartel na CCM. Ni chama kinachoishi kwa kutumia mbinu chafu. Sasa wanauza ardhi, wanavuna madini, wanabeba pesa za serikali kifisadi, nk. Kwa ujumla sioni tena biashara halali inayofanywa na CCM kuingiza kipato cha kuwawezesha kulipa mishahara ya wenyeviti na makatibu kila Wilaya na bado wakapata pesa za chaguzi ndogo na kununua magari na sasa waingie uchaguzi mkuu.

Taasisi zote za serikali hupata pesa pungufu ya zile zilizopangwa na Bunge kila mwaka lakini hakuna anayeuliza sehemu isiyokuja huenda wapi. Inasikika ni kwenye chama. Yaonekana Bajeti yetu inahudumia serikali mbili, Serikali halisi na hii ya CCM.

CCM ni Cartel wa hatari sana!

Cali cartel iliangushwa kwa msaada wa America. CCM iko Jeshini, iko polisi, iko mahakamani, na kwa ujumla kila katibu Mkuu wa Wizara lazima awe na kadi ya chama ndo maana wengine walianza kutangaza niya ya kugombea wakiwa bado ni makatibu wakuu. Nani ataiangusha? Nchi gani ya nje itakayoweza kutusaidia kuiondoa wakati tunasifiwa tumetulia na tuna amani?
Inaongozwa na Capo di Capo wa Indrangheta
 
Naona kama CCM imekwisha hama toka kwenye Cartel system. Ni 180[SUP]o[/SUP] shift. Upinzani naona umedoda wakati wagombea wote muelekeo ni CCM.
Ihame wapi? Ukitaka kujua wanakokwenda angalia mbinu wanazotumia kutafuta ushindi. Tangu serikali za mitaa na sasa madiwani na wabunge. Njama za kitoto vile!
 
ccm ina sifa zote za kuwa “cartel”, na wamechanganya mbinu za kikomnisti. Ni chama hatari kupita maelezo. Pia kina mbinu za kigaidi.
 
Naikumbuka thread hii! IMekuwaje wizara isiyo ya muungano ikawa na waziri toka Zanzibar, katibu mkuu toka Zanzibar? Halafu baadaye wanauza bandari ya Bara!
 
Back
Top Bottom