CCM Newala, yawahonga boda boda

CCM Newala, yawahonga boda boda

Mmawia

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
122,521
Reaction score
96,267
Uongozi wa CCM wilaya umejitahidi kukinusuru CCM kwa kujifanya kutoa mkopo wa boda boda 70 kwa waendesha boda boda ikiwa ni siku chache kuelekea uchaguzi mkuu october 2015.

Hata hivyo vijana hao waliokopeshwa Pikipiki hizo wamesikika wakisema hizo pikikpiki wanachukua na kura wanampigia lowasa na kura zao zinaenda kwa ubunge na udiwani UKAWA.
 
Nilijua habari hii kaandika mtu wa maana kumbe ni wewe mtoto wa fisadi Lowasa utumbo mtupu.
 
Nilijua habari hii kaandika mtu wa maana kumbe ni wewe mtoto wa fisadi Lowasa utumbo mtupu.

Utumbo mtupu?huo ndio ukweli na vijana wamenihakikishia kuwa lazima wagombea wa ccm wapigwe chini woote na bado hapo kampeini
 
Uongozi wa ccm wilaya umejitahidi kukinusuru ccm kwa kujifanya kutoa mkopo wa boda boda 70 kwa waendesha boda boda ikiwa ni siku chache kuelekea uchaguzi mkuu october 2015.,hata hivyo vijana hao walio kopeshwa Pikipiki hizo wamesikika wakisema hizo pikikpiki wanachukua na kura wanampigia lowasa na kura zao zinaenda kwa ubunge na udiwani ukawa
Bawacha mnapenda kuhongwa wewe umehongwa nini tuambie tujue maana kwa kuhongwa mnaongoza.
 
piki PKI chukueni msisaliti nafsi zenu kwenye kura tumieni vizur vichinjio vyenu Kama ilivyokuwa Kwa mh.Matilda ARUSHA .chukua Pikipiki Ccm kura yako Kwa ukawa
 
Bawacha mnapenda kuhongwa wewe umehongwa nini tuambie tujue maana kwa kuhongwa mnaongoza.

Akili za mkosaji,utaongea na kuita majina ya kila aina ila mjiandae kutawaliwa na lowasa kupitia cdm
 
piki PKI chukueni msisaliti nafsi zenu kwenye kura tumieni vizur vichinjio vyenu Kama ilivyokuwa Kwa mh.Matilda ARUSHA .chukua Pikipiki Ccm kura yako Kwa ukawa

Ccm kwa sasa wanahangaika kwa kutojua cha kufanya maana kila kona wameoza na lowasa amewashika kila pahala
 
Ccm kwa sasa wanahangaika kwa kutojua cha kufanya maana kila kona wameoza na lowasa amewashika kila pahala

Mmawia ndugu yangu tupinge wakipita Ukawa basi nahamia Mweda mie kama wewe unavyohangaika na EL
 
Sio Newala Hata Mmawia unajua! Newala hakuna mihemuko Ya Kisiasa kama ilivyo Monduli

Subiri lowasa atie mguu muone mziki wake maana newala ccm itabakia bendera kuwa nyingi kuliko wanachama
 
Mmawia ndugu yangu tupinge wakipita Ukawa basi nahamia Mweda mie kama wewe unavyohangaika na EL

Kinachotakiwa ni kukanusha au kukiri kama ni kweli ccm wamehonga kweli pikipiki?
 
Jamani, hivi mtu akikukopesha amekuhonga? tujitahidi kuelewa vizuri lugha. kama wamekopeshwa wanapaswa kulipa swala la kuhongwa linatoka wapi? ikiwa hao vijana wanashindwa kutofautisha kati ya kupewa na kukopeshwa, basi waelimisheni. Au ndo wameambiwa walipe kura badala ya fedha.
 
Mmawia ndugu yangu tupinge wakipita Ukawa basi nahamia Mweda mie kama wewe unavyohangaika na EL

Jiandae kabisa maana tayari lowasa ni rais wa JMT bado tu kuapishwa
 
Jamani, hivi mtu akikukopesha amekuhonga? tujitahidi kuelewa vizuri lugha. kama wamekopeshwa wanapaswa kulipa swala la kuhongwa linatoka wapi? ikiwa hao vijana wanashindwa kutofautisha kati ya kupewa na kukopeshwa, basi waelimisheni. Au ndo wameambiwa walipe kura badala ya fedha.

Poleni sana ma ccm nawashauri mjiandae kisaikolojia kutawaliwa na ukawa nanyi pambana angalau muongoze kambi rasmi ya upinzani
 
Hiyo sio habari.ingekuwa habari kama ccm imeacha kuhonga bodaboda.Hongo ni kawaida huko kwenye lichama hilo.
 
Sasa kwanini hiyo "mikopo" ije tu kipindi cha uchaguzi?

Jamani, hivi mtu
akikukopesha amekuhonga? tujitahidi kuelewa vizuri lugha. kama wamekopeshwa wanapaswa kulipa swala la kuhongwa linatoka wapi? ikiwa hao vijana wanashindwa kutofautisha kati ya kupewa na kukopeshwa, basi waelimisheni. Au ndo wameambiwa walipe kura badala ya fedha.
 
Back
Top Bottom