CCM na sarakasi ya mdahalo, kunani??

CCM na sarakasi ya mdahalo, kunani??

pocha2

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2014
Posts
890
Reaction score
396
Mwaka 2005 walikataa mdahalo wa wagombea, Mwaka 2010 pia walikataa mdahalo tena kwenye nafasi zote mbili Ubunge na Urais, na mwaka huu kwenye Harakati za kumtafuta mgombea urais kwa ticket yao wenyewe (ccm) wameadhibu watia nia wote walioonesha dalili ya kutaka mdahalo kwamba walikuwa wanafanya kampeni mapema. Maswali yangu ni haya :

1. Kama mdahalo ni muhimu ni kwanini hawakuendesha mdahalo huo ndani ya chama?
2. Kama midahalo ni muhimu kwanini walikataa kushiriki midahalo hiyo miaka ya nyuma kwa ubunge na urais??
3. Ni kwanini tusurudishe kila kipindi cha Shabani Kissu cha midahalo ya wagombea ubunge TBC? https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=72998
4. Langu la mwisho, mwaka huu kuna nini???
 
Kwa huu kuna mgombea ni Dr. pia anaweza kueleza sera na vision yake bila tatizo. hivyo, tunaomba mdahalo ufanyike tupime ukawa wa sera na mgombea ambaye anaweza kuelezea vision yake?
 
UKAWA nao wanapaswa kugoma kuhudhuria midahalo hiyo kama walivyokwishafundishwa na wenzao CCM, katika chaguzi zote zilizopita.
 
Mwaka huu hatuangalii sera, sera yetu ni kubadirisha chama, sera never worked
 
ccm waende kwenye mdahalo wajitekenye wenyewe na wacheke wenyewe sisi ukawa tuko bz kuwaeleza wananchi sera zetu
 
Kwa sehemu tulipo sidhani kama unahitaji mdahalo ili uweze kufahamu kuwa CCM imeua viwanda vyetu vyote, imetufikisha kwenye kuwa na deni la taifa la TZS 40 trillion, imeshindwa kutumia rasilimali zetu kiufasaha kutuwezesha kupata maendeleo, imeua thamani ya shilingi kwa kutufanya kuwa soko la wazalishaji, imeruhusu wizi wa mabilioni ya shilingi za ESCROW, EPA, MEREMETA, KIWIRA, RICHMOND n.k. bila wahusika kufilisiwa wala kushtakiwa, imetufanya tudharaulike kwa majirani zetu kama Rwanda na Burundi kwa kushindwa kutumia hata bandari yetu vizuri, imeua reli na miundombinu, imeua shirika letu la ndege ATC,...yani naweza kuendelea mpaka asubuhi ya kesho.

Inasikitisha sana kwamba hata pipi na big G zinazoongoza kwa kuuzwa Dar es Salaam zinazalishwa Nairobi Kenya, tunahitaji mdahalo wa nini hasa?

Sote tumeshaona na tunayajua mabaya ya CCM na tutawatoa madarakani bila kuwa na haja ya mdahalo wowote.
 
mbona jana wamejitabiria wenyewe na wakashinda wenyewe?na wajue tr25 Watashangaa
 
Tuwe wakweli,

Kwa jinsi ambavyo EL ameshambuliwa kwenye media ( lengo likiwa ni character assassination) mdahalo umekosa maana.

Kampeni zingekuwa ni za kunadi ubora wa sera kwa vyama vyote vya siasa bila personal attacks hapo mdahalo ungekuwa na maana kwa kuwa watu wangejikita kwenye sera. Lakini mambo jinsi yalivyo kwa sasa, mdahalo kwa wagombea is only a nuisance!
 
Wanataka mdahalo wa nini wakati wamesema watashinda kwa 69percent
 
Mwaka 2005 walikataa mdahalo wa wagombea, Mwaka 2010 pia walikataa mdahalo tena kwenye nafasi zote mbili Ubunge na Urais, na mwaka huu kwenye Harakati za kumtafuta mgombea urais kwa ticket yao wenyewe (ccm) wameadhibu watia nia wote walioonesha dalili ya kutaka mdahalo kwamba walikuwa wanafanya kampeni mapema. Maswali yangu ni haya :

1. Kama mdahalo ni muhimu ni kwanini hawakuendesha mdahalo huo ndani ya chama?
2. Kama midahalo ni muhimu kwanini walikataa kushiriki midahalo hiyo miaka ya nyuma kwa ubunge na urais??
3. Ni kwanini tusurudishe kila kipindi cha Shabani Kissu cha midahalo ya wagombea ubunge TBC? https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=72998
4. Langu la mwisho, mwaka huu kuna nini???

Wewe unautaka au maana hata haueleweki
Labda weka wazi hilo
 
NIKIPEWA NAFASI YA KUWASHAURI UKAWA, NITAWAOMBA WASIMPELEKE MGOMBEA WAO KATIKA MIDAHALO. NCHI HII HAINDESHWI KWA MISISIMKO. WALIPOWAHITAJI WENYEWE WAJE MIAKA HIYO WALIKIMBIA, LEO KWA KUWATUKANA MALOFA, MGOMBEA MGONJWA, WAPUMBAVU BILA HATA YA KUOMBWA MSAMAHA UNAENDA KUKAA NA MTU AMBAYE HAMUESHIMIANE. hESHIMA KUBWA NI KWENYE SANDUKU LA KURA.
 
Mwaka 2005 walikataa mdahalo wa wagombea, Mwaka 2010 pia walikataa mdahalo tena kwenye nafasi zote mbili Ubunge na Urais, na mwaka huu kwenye Harakati za kumtafuta mgombea urais kwa ticket yao wenyewe (ccm) wameadhibu watia nia wote walioonesha dalili ya kutaka mdahalo kwamba walikuwa wanafanya kampeni mapema. Maswali yangu ni haya :

1. Kama mdahalo ni muhimu ni kwanini hawakuendesha mdahalo huo ndani ya chama?
2. Kama midahalo ni muhimu kwanini walikataa kushiriki midahalo hiyo miaka ya nyuma kwa ubunge na urais??
3. Ni kwanini tusurudishe kila kipindi cha Shabani Kissu cha midahalo ya wagombea ubunge TBC? CCM yakatakaza wagombea wake kuonekana TBC1, Tido Mhando ataarifiwa
4. Langu la mwisho, mwaka huu kuna nini???


Mkuu umeuliza maswali magumu sana kiasi kwamba hata kama mi ningekuwa CCM ningejiuzulu uanachama baada ya kusoma maswali haya. Ni balaaa.
Nadhani ndo wanajaribu kuitumia hiyo kama karata yao ya mwisho ila nawatahadhari kuwa wasijaribu kabisaaaaa kufanya hiyo kitu. Inaenda kuwaadhiri na kuwaweka wazi uchi wao ambao tayari uko wazi kwa kiasi fulani
 
Mgombea was ccm anatoa ahadi nitafanya hili nitafanya lile badala ya kutueleza nimefanya haya na nimefanya yale na nimeshindwa haya na nitafanya hivi.kwahiyo sioni huo mdahalo watatueleza nini kwakuwa nawaona ni watu wa kutoa ahadi tu kila kukicha na wamo zaidi ya miaka 50sasa wanatutwala.
 
Kwa majibu ya wengi kwenye uzi huu yanadhihirisha kauli ya kwamba watanzania walio wengi ni wavivu wa kufikiri.Huwezi leo kutetea hoja ya CCM kukataa midahalo vipindi vilivyopita ETI iwe sababu ya CHADEMA kuikataa wakati huu.Huo ni ufupi wa kufikiri.Watu wenye nia njema ya kushika hatamu ya dola hawatafuti sababu za kushindwa kufanikiwa bali hupambana na vikwazo vyote hadi tamati.Kwa utetezi huu wa watu ninaowaamini humu kuwa ni wasomi basi Tanzania ipo pabaya.
Nawaza kizezeta
 
Haina haja ya kwenda kufanya huo mdahalo.Mana wenyewe walianzisha ngoja na sie ukawa tumalizeeee.LOWASA ni rais wangu.
 
Midahalo kwanchi zawenzetu zilizo na Demokrasia yakweli nimizuri sana kwani inatoa nafasi kwa raia kuwapima wagombea nakujiridhisha juu yakile wanachoahidi kuwafanyia pindi wakichaguliwa, na uelewa wao juu yamambo mbalimbali yanayoikabili jamii husika.

Ila kwanchi kama yakwetu mimi binafsi wala sihitaji mgombea wakuongea vizuri kwenye midahalo wala kwenye kampeni kwasababu kamakuwa naviongozi waongeaji tumekuwanao miaka nendarudi. Wanaongea saaana majukwaani lakini mala tu tukishawachagua tunashuhudia usaliti mkubwa dhidi yetu kutoka kwao.

Tulimshuhudia Mkapa akitawala mdahalo 1995 akijinasibu kwamba atapambana na rushwa kwanguvu nauwezo wake wote, baada yakuchaguliwa aliyoyafanya akiwa Ikulu kilammoja nishahidi. Hadi akajiuzia mgodi bilahata haya wkt anajua yeye ndomkuu wanchi.

Tukirudi kwa Jk yeye chama chake kilikataa katakata asishiriki mdahalo wowote. Sababu nikwanini walimzuia wanajua wao. Ila kama binadamu mimi nahisi Ccm walijua Jk simzuri ktk kukabiliana namaswali yawatu nguli wakuuliza maswali magumu au walijua wana makandokando mengi ambayo wasingependa mgombea wao aulizwe hadharani.

Nadhani wakati umefika iwapo kama Taifa tunadhani kunahaja yakuwa na midahalo kwa wagombea, basi Tume iliweke kwenye kanuni zake ili iwe nilazima kila chama kilijue kwamba nilazima kushiriki nasiyo kamailivyo sasa ambapo kinachofanyika ni vyama kuviziana kwakuangalia niainagani yawagombea walionao. Kamawanaona watamudu basi wanajitokeza kuwaruhusu kushiri, bali wakiona hawana uwezo wakujenga hoja nakujibu maswali basi wanawazuia wasishiriki.

Kwahiyo miminadhani kwasasa hiyo midahalo yakuviziana kwalengo lakutimiza matakwa yakisiasa badala yakijamii haifai. Nawashauri wapinzani wote waikatae maana haina tija kwa Taifa.
 
Back
Top Bottom