Col FEN
JF-Expert Member
- Jun 16, 2017
- 327
- 460
CCM MTUMIENI LIPUMBA LAKINI MTATOA TU
Na: Mzee Jabir Ali
Alhaj Mstaafu Ibrahim Haruna Lipumba, anachokifanya sasa nidhana ya litote tugawane mbao vinginevyo tukae mezani tusameheane, hapa sio mbao tu hata misumari haichomolewi wala hakuna meza ya msamaha kwa kibaraka msaliti. Waambie mabwana zako CCM mpingo wa Tabora ni wakupikia Tumbaku, hauyeyushi chuma cha pua.
Tunajua mabwana zako CCM wamekutuma utumie falsafa ya Harry Truman "If you can't Convince Them, Confuse Them" uwajengeshe chuki wanachama wa CUF BARA dhidi ya Katibu MKUU wao, kuwa chama ulichokisusa kikafanya vizuri ktk chaguzi kuliko kipindi ulipokiongoza wewe, wakuamini kuwa kimeuzwa kwa CHADEMA, ili CUF igawanyike kuwe na CUF mbili CUF BARA na CUF ZNZ, kwa msingi huo kitakuwa kimepoteza sifa ya kuwa chama cha siasa nchini, nakufutiwa usajili wake, kwa maslahi ya mabwana zako CCM.
Lipumba unawahadaa na kuwapumbaza wenye gonjwa la kupendapenda, eti Maalim Seif kauza CUF kwa CHADEMA. Looo!!! Mnafiki mkubwa we, eti Alhaj!! bora ulivyostaafu, wakati wewe Lipumba unaanzisha mashirikiano na CHADEMA kwenye Bunge la katiba Maalim Seif alikuwepo? wakati unawaongoza CHADEMA kususia Bunge Maalim alikuwepo? Wakati mnatembea nchi nzima kuwaaminisha watu CUF imeungana na CHADEMA ktk UKAWA Maalim Seif alikuwepo? Wakati mnaandaa miongozo na utaratibu wa mashirikiano na CHADEMA Maalim Seif alikuwepo? Wakati mlipopanga vigezo vya kuachiana majimbo Maalim Seif alikuwepo? Wakati mnagawana majimbo ya kuweka wagombea Maalim Seif alikuwepo?
Maalim Seif alikuwepo Jangwani kama shuhuda pamoja na sisi wote na Watanzania wengine waliona live kupitia runinga Wenyeviti mkisaini mikataba ya mashirikiano na Makatibu Wakuu nao wakasaini kama mashahidi.
KTK HILI ALHAJ MSTAAFU LIPUMBA NDIE ULIEIUZA CUF KWA CHADEMA.
Na nyie CCM Mabwana zake Lipumba kama mmeona njia muafaka kwenu ni kumtumia Lipumba kuisambaratisha CUF ili iwe manusura kwenu ya kukatalia kuitoa ZANZIBAR.
TUNAWAHAKIKISHIA MTATOA MTAKE MSITAKE.
Sent using Jamii Forums mobile app
Na: Mzee Jabir Ali
Alhaj Mstaafu Ibrahim Haruna Lipumba, anachokifanya sasa nidhana ya litote tugawane mbao vinginevyo tukae mezani tusameheane, hapa sio mbao tu hata misumari haichomolewi wala hakuna meza ya msamaha kwa kibaraka msaliti. Waambie mabwana zako CCM mpingo wa Tabora ni wakupikia Tumbaku, hauyeyushi chuma cha pua.
Tunajua mabwana zako CCM wamekutuma utumie falsafa ya Harry Truman "If you can't Convince Them, Confuse Them" uwajengeshe chuki wanachama wa CUF BARA dhidi ya Katibu MKUU wao, kuwa chama ulichokisusa kikafanya vizuri ktk chaguzi kuliko kipindi ulipokiongoza wewe, wakuamini kuwa kimeuzwa kwa CHADEMA, ili CUF igawanyike kuwe na CUF mbili CUF BARA na CUF ZNZ, kwa msingi huo kitakuwa kimepoteza sifa ya kuwa chama cha siasa nchini, nakufutiwa usajili wake, kwa maslahi ya mabwana zako CCM.
Lipumba unawahadaa na kuwapumbaza wenye gonjwa la kupendapenda, eti Maalim Seif kauza CUF kwa CHADEMA. Looo!!! Mnafiki mkubwa we, eti Alhaj!! bora ulivyostaafu, wakati wewe Lipumba unaanzisha mashirikiano na CHADEMA kwenye Bunge la katiba Maalim Seif alikuwepo? wakati unawaongoza CHADEMA kususia Bunge Maalim alikuwepo? Wakati mnatembea nchi nzima kuwaaminisha watu CUF imeungana na CHADEMA ktk UKAWA Maalim Seif alikuwepo? Wakati mnaandaa miongozo na utaratibu wa mashirikiano na CHADEMA Maalim Seif alikuwepo? Wakati mlipopanga vigezo vya kuachiana majimbo Maalim Seif alikuwepo? Wakati mnagawana majimbo ya kuweka wagombea Maalim Seif alikuwepo?
Maalim Seif alikuwepo Jangwani kama shuhuda pamoja na sisi wote na Watanzania wengine waliona live kupitia runinga Wenyeviti mkisaini mikataba ya mashirikiano na Makatibu Wakuu nao wakasaini kama mashahidi.
KTK HILI ALHAJ MSTAAFU LIPUMBA NDIE ULIEIUZA CUF KWA CHADEMA.
Na nyie CCM Mabwana zake Lipumba kama mmeona njia muafaka kwenu ni kumtumia Lipumba kuisambaratisha CUF ili iwe manusura kwenu ya kukatalia kuitoa ZANZIBAR.
TUNAWAHAKIKISHIA MTATOA MTAKE MSITAKE.
Sent using Jamii Forums mobile app