CCM mtaondoka tu, hili halina mjadala

CCM mtaondoka tu, hili halina mjadala

Ulevi mwingine unakunyima hata aibu. Watanzania wengi waliichukia ccm kwa hali ilivyokuwa.
Kwa haya anayofanya JPM nina uhakika hata upinzani wanashangaa mno. Hali hii ikiendelea kwa miaka 5 kwa kweli ni ndoto kiongozi yoyote kumpiku JPM kwenye uchaguzi ujao. Achane kula pesa za watu ninyi wapambe. Tafuteni kazi nyingine za kufanya.
 
Ulevi mwingine unakunyima hata aibu. Watanzania wengi waliichukia ccm kwa hali ilivyokuwa.
Kwa haya anayofanya JPM nina uhakika hata upinzani wanashangaa mno. Hali hii ikiendelea kwa miaka 5 kwa kweli ni ndoto kiongozi yoyote kumpiku JPM kwenye uchaguzi ujao. Achane kula pesa za watu ninyi wapambe. Tafuteni kazi nyingine za kufanya.

Yaani Mungu aisaidie sana hii nchi aisee,kwa upinzani wa waselawasela huu wa hawa jamaa ni majanga tuu. Hivi kweli ni kwa nini sijui upinzani bora haupo nchi hii. Duuuuh. Watu wanalalamika kwa nini CCM haitaki kutoka madarakani wakati mwenyekiti wetu pia hataki kuachia madaraka . Huu ni uhuni kabisa
 
Naelewa wengi mtakuwa kwenye ndoto kuwa CCM itaikalia Tz mpaka mwisho wa dunia ,mbona mnajidanganya kwa hali ninavyoiona ni suala la mida tu ,ila mnakwenda na maji ,hii kamata kamata bin vunjavunja haitowasaidia zaidi ya kuwadumaza na kubaki na mawazo ya kuitawala nchi kwa kutegemea polisi na vyombo vingine ,mpaka lini mtakuwa hamjiamini hadi ifikie kuwakamata viongozi wavyama vikuu vya upinzani ,Mandela alikamatwa na kuswekwa jela ,hivi Waafrika waliobakia uraiani waliogopa vifaru vya kaburu ?

Siuoni muelekeo wa CCM kuwa Chama kinachopendwa na wananchi muelekeo huo haupo bado wananchi walio wengi wana imani Tanzania iliyobora na yenye serikali inayopendwa na wananchi itatokea katika vyama vya upinzani ,Tanzania inayoongozwa na serikali yenye kulinda haki ya raia zake na inayohakikisha sheria haipindishwi na wengine kuwa juu ya sheria na vyama vyote vinahukumiwa kwa mujibuwa sheria itatokea upinzani na sio kutoka kwenye serikali zaCCm.

CCM haina mvuto kwa wananchi hilo nadhani halina ugonvi ,unajua wananchi bado hawapo huru ndani ya nchi yao na ndio ikaona CCM wanafanya wanavyotaka na hili sio linafanywa kwa viongozi waupinzanihata wananchi huko mitaani bado hali ni tete kwa maana inakuwa rahisi kudhulumiwa ikiwa tu atakumbana na CCM katika mahitaji ya kila siku ,tunawaona watu wanapigwa zaidi kwa sasa ni upande wa Zanzibar ,polisi hawana habari na wao huwa siku zote ni wenye kulzifanyia uchunguzi habari hizo ,

Hivi viongozi wa CCM hawajawahi kutoa viashirio vya uchochezi ? Ni lini polisi waliwaita kwenye vituo na kuwahoji ?

Juhudi za Mh.Magufuli zitakuwa hazina faida kama kuna upande unagandamizwa ,sheria zinatumikia upande mmoja ,wananchi walio wengi wakichoka na uovu basi hakuna cha kuwasimamisha na ndipo tulipo hakuna cha kuwasimamisha katika kuhakikisha liwe liwalo CCM inaondoka maddarakani.


NAKUBALIANA NA WEWE 1000...%. HATA RAIS MAGUFULI AKIPENDWA SIO CCM NI YEYE LAKINI CCM NDOHO! NA YEYE ASIPO JIPAMBANUA TUKATOFAUTISHA YEYE NA CCM, HATA MIAKA 5 MINGI NAKUHAKIKISHIA. KUMBUKA USEMI WA TENDA WEMA NENDA ZAKO, USINGOJE SHUKRANI. KWA HIYO NI RAHISI SANA KUSAHAU WEMA 1000% KULIKO UBAYA WA 10%. MIMI KWA UPANDE WANGU CCM SITAISAMEHE KAMA CHAMA PAMOJA NA MANUFAA MENGI NILIYO YAPATA KWAYO WAKATI WA NYERERE.
 
wanabana elimu eti watawale milele...hawajui kuongeza dimbwi la watu wanye maisha magumu ni soo baadae kwa afya yao
ccm badilikeni hii nchi ni ya waTZ msijibinafsishie..............
 
Back
Top Bottom