CCM mpya na Tanzania mpya hii hapa..

CCM mpya na Tanzania mpya hii hapa..

Mwamba Usemao Kweli

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
744
Reaction score
186
CCM mpya Tanzania mpya

Hayawi hayawi sasa yanaenda kutimia...Tunahesabu masaa kuanzia leo kabla ya tarehe 23.7.2016 ambapo nchi mpya inaenda kuzaliwa. Ni nchi yenye jina lilelile Tanzania ila yenye mtazamo, utamaduni wa kutenda na utashi mpya katika kusimamia maendeleo ya watu wake na njia zake kuu za uchumi inaenda kuundwa.

Naona mabadiliko makubwa katika utumishi wa umma, jumuia na shughuli za mtu mmoja mmoja unaenda kusimikwa na kuanza kutumika kuwezesha uzalishaji mali wenye tija na maslahi katika nchi yetu, maeneo husika ni pamoja na:-

1. Viwanda na uzalishaji
2. Kilimo
3. Uvuvi
4. Madini
5. Mifugo
6. Misitu na nyuki
7. Teknolojia, elimu na utafiti
8. Utalii na maliasili
9. Biashara ya ndani na nje
10. Ujenzi
10. Elimu
11. Siasa na jamii
12. Sheria na usimamizi wake katika kupambana na rushwa na ufisadi.
13. Ulinzi na usalama wa nchi yetu

Maeneo tajwa na mengineyo mengi yaliyo sahaulika kwa pamoja yanaenda kupewa msukumo mpya ndani ya Tanzania.

Rais wetu Magufuli ni tunu ya kipekee kabisa ambayo watanzania tulimuomba mungu na hatimaye ametupatia. Tumpe ushirikiano. Wapo watakao umia katika utekelezaji wake lakini hakuna njia nyengine kwani siku zote dawa/matibabu ya ugonjwa sugu huwa yana changamoto nyingi.

Watanzania tujipange nchi hii ni tajiri na inauwezo wa kupiga hatua kubwa kimaendeleo. Tumuunge mkono mheshimiwa J.P.J Magufuli.

CCM mpya na Tanzania mpya chini ya J. P. J. Magufuli.

Mungu ibariki tanzania.
 
ccm ni ile ile ooooh ni ileile tatizo chama kina mafisadi wengi,biashara ya meno ya tembo humohumo,wahujumu uchumi humohumo,madawa ya kulevya humohumo,wanaompinga rais magufuri kuwa mwenyekiti wamo humohumo na hii ndio ccm.
 
mtoto alidumaa kadumaa tu hata umpe lishe ya kiwango cha juu, CCM sina hamu nao
 

Kulikuwa na Mtanzania aliyeandika kama haya ndani ya miezi ya mwaka wa kwanza ya watawala(Marais) wa CCM waliopita.


Sio mbaya kuona na wewe ukutumaini yale yale, pengine hata na mjukuu wako atakaye zaliwa miaka ya Baadaye akaandika kama aliyo yaandika Babu yake (Kipindi hiko akiendelea kununua sukari kwa Tsh 8500 kwa kilo.)
 
Watoto wa wakubwa naona wameshaanza kusogea dodoma maana wanatupia pic kwa mbwembwe mitandaoni!
1469028086079.jpg
 
CCM mpya Tanzania mpya

Hayawi hayawi sasa yanaenda kutimia...Tunahesabu masaa kuanzia leo kabla ya tarehe 23.7.2016 ambapo nchi mpya inaenda kuzaliwa. Ni nchi yenye jina lilelile Tanzania ila yenye mtazamo, utamaduni wa kutenda na utashi mpya katika kusimamia maendeleo ya watu wake na njia zake kuu za uchumi inaenda kuundwa.

Naona mabadiliko makubwa katika utumishi wa umma, jumuia na shughuli za mtu mmoja mmoja unaenda kusimikwa na kuanza kutumika kuwezesha uzalishaji mali wenye tija na maslahi katika nchi yetu, maeneo husika ni pamoja na:-

1. Viwanda na uzalishaji
2. Kilimo
3. Uvuvi
4. Madini
5. Mifugo
6. Misitu na nyuki
7. Teknolojia, elimu na utafiti
8. Utalii na maliasili
9. Biashara ya ndani na nje
10. Ujenzi
10. Elimu
11. Siasa na jamii
12. Sheria na usimamizi wake katika kupambana na rushwa na ufisadi.
13. Ulinzi na usalama wa nchi yetu

Maeneo tajwa na mengineyo mengi yaliyo sahaulika kwa pamoja yanaenda kupewa msukumo mpya ndani ya Tanzania.

Rais wetu Magufuli ni tunu ya kipekee kabisa ambayo watanzania tulimuomba mungu na hatimaye ametupatia. Tumpe ushirikiano. Wapo watakao umia katika utekelezaji wake lakini hakuna njia nyengine kwani siku zote dawa/matibabu ya ugonjwa sugu huwa yana changamoto nyingi.

Watanzania tujipange nchi hii ni tajiri na inauwezo wa kupiga hatua kubwa kimaendeleo. Tumuunge mkono mheshimiwa J.P.J Magufuli.

CCM mpya na Tanzania mpya chini ya J. P. J. Magufuli.

Mungu ibariki tanzania.



Haya uliyo yaandika yatawezekana pale ccm utakapo toka madarakani
 
Tangu lini tembo akageuka kuwa sungura?
 
Back
Top Bottom