CCM mfukuzeni Jaji J.S.Warioba

CCM mfukuzeni Jaji J.S.Warioba

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Kama kweli mnaamini kuwa Jaji Warioba amewasaliti,mfukuzeni. Kama kweli mnaamini kuwa Jaji Warioba na Tume yake 'wamepika' Rasimu kwa chuki na hila zao na kuacha maoni ya wananchi kama mnavyodai,mfukuzeni chamani mwenu. Kama kweli mnaamini kuwa mnahitaji muda wa kutosha wa kumkashifu,kumtusi,kumsimanga na kumkebehi Jaji Warioba ndani ya chama chenu,Bungeni na kwingineko,mtimueni chamani kwa kumvua uanachama wake.

Mkifanya hivyo itakuwa poa. Mtakuwa na kila nafasi na muda wa kusema mtakayo juu yake. Wafuatiliaji wa siasa za nchi hii mnatuchosha. Tunawaona ni wa ndimi-mbili kuigiza kumponda Jaji Warioba wakati mnaye chamani.Na mnamheshimu kama Kada mkongwe na mtiifu kwa chama. Kama mmeweza kumfukuza Mansoor wa Kiembesamaki hivi karibuni,mnashindwa nini kwa Jaji Warioba.

Kama hamuwezi,mwacheni Jaji Warioba asimamie anachokiamini. Asimamie Maoni ya Wananchi aliyoyakusanya na Tume yake toka sehemu mbalimbali za nchi hii na kuyaainisha katika Rasimu. Msiendelee na kuonyesha mchezo wa kuigiza.
 
Kama kweli Komba na wenzie huko Dodoma wanaamini wana hoja basi wamuite Jaji Warioba kwa Q & A.
 
hawezi kufukuzwa uanachama,lakini hakuna asiyejua kama data na maamuzi yao juu ya rasimu ya katiba yana walakini.mfano mzuri Zanzibar kulikuwa na 2 au mkataba,na neno mkataba na serikali tatu ni maneno yenye maana tofauti kabisa.sasa sijui wao Tatu wametoa wapi!
 
Mambo yenu ya ufipa yanawashinda mtaweza ya CCM?
 
^^
Siri ya Warioba anayo Warioba na Kikwete,, kitendo cha hatua zote za rasimu kuhakikiwa kabla ya uzinduzi rasmi wa Rasimu na ikaruhusiwa kujadiliwa ilihali dola iliyopo madarakani inajua athari zake, isitoshe tuzo ya Muungano akapewa, kinanipa shaka, wanasiasa hawa wanajua CD inayochezwa!
^^
 
Kama kweli mnaamini kuwa Jaji Warioba amewasaliti,mfukuzeni. Kama kweli mnaamini kuwa Jaji Warioba na Tume yake 'wamepika' Rasimu kwa chuki na hila zao na kuacha maoni ya wananchi kama mnavyodai,mfukuzeni chamani mwenu. Kama kweli mnaamini kuwa mnahitaji muda wa kutosha wa kumkashifu,kumtusi,kumsimanga na kumkebehi Jaji Warioba ndani ya chama chenu,Bungeni na kwingineko,mtimueni chamani kwa kumvua uanachama wake.

Mkifanya hivyo itakuwa poa. Mtakuwa na kila nafasi na muda wa kusema mtakayo juu yake. Wafuatiliaji wa siasa za nchi hii mnatuchosha. Tunawaona ni wa ndimi-mbili kuigiza kumponda Jaji Warioba wakati mnaye chamani.Na mnamheshimu kama Kada mkongwe na mtiifu kwa chama. Kama mmeweza kumfukuza Mansoor wa Kiembesamaki hivi karibuni,mnashindwa nini kwa Jaji Warioba.

Kama hamuwezi,mwacheni Jaji Warioba asimamie anachokiamini. Asimamie Maoni ya Wananchi aliyoyakusanya na Tume yake toka sehemu mbalimbali za nchi hii na kuyaainisha katika Rasimu. Msiendelee na kuonyesha mchezo wa kuigiza.

They ain't got no balls to do that coz they know for sure it will come to bite their asses!!!
 
hawezi kufukuzwa uanachama,lakini hakuna asiyejua kama data na maamuzi yao juu ya rasimu ya katiba yana walakini.mfano mzuri Zanzibar kulikuwa na 2 au mkataba,na neno mkataba na serikali tatu ni maneno yenye maana tofauti kabisa.sasa sijui wao Tatu wametoa wapi!

Mkataba ungevunja Muugano maana ingekuwa sawa na ilivyo East Africa Community. Na hadidu rejea zilisema Muungano uboreshwe na sio kuvunjwa.

Hivyo namna pekee ya kudumisha Muungano na kuondokana na kero za miaka 50 ni serikali 3, pendekezo ambalo linakubalika Zanzibar (badala ya serikali 2).
 
pamoja na makelele yote ya ndugu KOMBA AND CO LTD ccm hawana uwezo wa kumfukuza MZALENDO WARIOBA .
 
Mkuu wahenga wamenena baniani mbaya lakini kiatu chake ni dawa na fadhila za punda ni mashuzi kwa sababu shida yao emekwesha ni sawa sawa na pale tunapowachagua viongozi wetu na wakishapata tuj basi huwaoni tena wako bezy na biashara zao za unga wa sembe na kwa yote haya ameweka historia jaji warioba katika taifa hili la tanganyika kwa hiyo kazi ya rasimu na hakuna kiongozi yoyote atakaimfikia hata marihemu hamfikii yaani nyerere na tumeunda tume tatu na zote jibu ni 3 na ombi langu kwa jaj warioba usiwajibu kaa kimya poza mawazo yako hawa ni kama fisi mkono kudondoka
 
Ccm kwa ujumla ni matamata yaani matondo.
 
^^
Siri ya Warioba anayo Warioba na Kikwete,, kitendo cha hatua zote za rasimu kuhakikiwa kabla ya uzinduzi rasmi wa Rasimu na ikaruhusiwa kujadiliwa ilihali dola iliyopo madarakani inajua athari zake, isitoshe tuzo ya Muungano akapewa, kinanipa shaka, wanasiasa hawa wanajua CD inayochezwa!
^^

Wewe una akili kuliko wabunge na mashabiki wote wa ccm wanaochezeshwa shere na mwenyekiti wao wa taifa. Warioba na Kikwete wana makubaliano juu ya hii rasimu. Warioba pia ana makubaliano na ukawa. Tungoje tuone mwisho wa game hii jinsi watu watakavyoumbuka mchana kweupe.
 
Mafuriko huwa yanakuja wakati mvua zinavyozidi kunyesha, tume zimeundwa TATU, na majibu yako Sawa, Wale watafiti wenzangu I mean Profs and Drs mko wp? Mbona Leo hii mnakataa vyeti vyenu? Mambo yaliyofanyiwa research mnayakataa AMA Kweli njaa haina adabu kwa mwanadamu, ukweli ni kwamba mafuriko ya Katiba yamekuja, tunasubiri muda tuu yaanze kubomoa weak points na baadae ukuta kuanguka, JK sio Mungu kama step amebugi tusubiri samaki kujikaanga kwa Mafuta yake, tume huru ya serikali imewaletea mapendekezo ya wananchi Leo hii, mmeyakataa, Shule ziliwekwa ili watu wafikiri na kuelewa na sio kujibu, hata mjinga ANA majibu lkn haelewi wala hafikiri, UKAWA WAKO SAHIHI, HONGERA MZEE WARIOBA our only remaining LEGEND.
 
Fukuzeni wazalendo wote basi CCM mbaki na wafisadi
 
Fukuzeni wazalendo wote basi CCM mbaki na wafisadi

ukimchukua komba kitumbo tele ( mlala fofo) + wassira Mzee wa utalii (mlala fufu) = kibaji Lusinde mzee wa mipasho hapo tegemea katiba mpya?
 
Akija chama chochote kinachounda UKAWA tunamsimamisha shujaa huyu angalau awamu moja awe mgombea wetu wa Uraisi 2015 na atazoa kura kama njugu!
 
Back
Top Bottom