Kama tunajifurahisha ni sawa ila kama ni ukweli CCM wamekuwa wakipata watu wengi sana. Juzi Mwigulu alikuwa Nkinga bila hata mgombea alikuwa na mkutano mkubwa mno kuliko alifanya Dr Slaa siku tatu zilizopita. Ulikuwa mkutano mkubwa mno mpaka nikashangaa wamefuata nini. Halafu huyo jamaa ana namna ya kuongea kwa namna mpaka watu wanaamini, anaharibu sana kama pale ali water down hotuba yote ya slaa yaani kama kuna mtu amebaki na yale ya slaa ni aliyemwelewa tu wengine walibadilika sana mpaka wengine waka diriki kusema Mwigulu agombee urais. Nimemsikiliza anawavutia kwa kutoa mifano kwa kisukukuma, kinyaturu, kinyiramba, kinyamwezi halafu watu wetu bwana wanamshangilia kweli. Pia kafanya mkutano mwingine mkubwa simbo, nanga na nyandekwa na amebadilisha watu kweli. Ana mvuto fulani wa maneno na staili ya kuhutubia watu hawachoki. Akizunguka kote jimbo litakuwa gumu kutabiri tofauti n mtoa thread alivyosema. Ngoja niwatafutie picha