luvcyna
JF-Expert Member
- Feb 24, 2009
- 1,848
- 1,938
salam sana wanajamii wenzangu... Napenda kuwaletea taarifa kuwa CCM ndo wamepania kufunika haswa katika kata mama wanayoitegemea kuliko zote kata ya Nkoanrua ambayo katika uchaguzi uliopita ilimbeba mgombea wao Jeremia Sumari vilivyo na kumuachia nassary kura 28. Baada ya CDM kupita maeneo hayo siku ya alhamisi na kufanya mageuzi makubwa ya kifikra na kujaza umati wa ajabu kiasi cha kutoenea uwanja wa shule ya msingi Nkoanrua leo ni muda muafaka kupima muitikio wa wananchi wa kata hii kwa kile walicholishwa Alhamisi na mheshimiwa Dr. W.P.Slaa kama kimekuwa digested ama vomited.
Katika kuonyesha kuwa wamepania vilivyo kuwahadaa wakazi wa eneo hili, CCM wamekuja na wasanii lukuki kama Khadija Kopa, Diamond,Origino Komedy, na vikundi kadhaa vya sanaa. Naye Nchema anasubiriwa vilivyo kujibu tuhuma alizorushiwa katika mkutano wa CDM uliopita.
Nawasilisha natafuta picha kwa hudi na uvumba...mwenye taarifa zaidi ya nilizo nazo tafadhali funguka
Katika kuonyesha kuwa wamepania vilivyo kuwahadaa wakazi wa eneo hili, CCM wamekuja na wasanii lukuki kama Khadija Kopa, Diamond,Origino Komedy, na vikundi kadhaa vya sanaa. Naye Nchema anasubiriwa vilivyo kujibu tuhuma alizorushiwa katika mkutano wa CDM uliopita.
Nawasilisha natafuta picha kwa hudi na uvumba...mwenye taarifa zaidi ya nilizo nazo tafadhali funguka