Acheni uvivu wa kufikiri na siasa za chini ya vitanda, magufuli ameongea Kama rafiki wa raila na hajaongea kwa niaba ya CCM au serikali , mnalikuza jambo hili kwa maslahi ya ovyo ovyo tu, gazeti la raia mwema siku hizi nalo linaandika udaku tu.Magufuli na raila ni marafiki hata nje ya uwaziri wao Ana haki Kama raia yeyote kummunga mkono raila kwa uwazi bila kificho Kama alivyofanya.
Nashangaa Huyu wenje ambaye hata mwanza wamemchoka anakurupuka kutoa matamko yasiokuwa na msingi, acheni watu wafanye siasa za maana sio kuongea usikike kuwa wewe ni msemaji au wa waziri kivuli wa mambo ya Nje.
Mwaliko binafsi,maoni yake binafsi hakuna tatizo hapa.
it wasnt a public rally,it was ODM's national deligates meeting. Magufuri alialikwa kama rafiki,akaongea kama rafiki.koso lake liko wapi?mkuu wataalamu wa sheria za kikanda na kimataifa itabidi watueleze hali km hii inakuwaje.
je katiba ya kenya inaruhusu mgombea kupigiwa debe na foreigner?
sheria zetu je zinaruhusu citizen wa tz kwenda kumpigia kampeni mgombea wa nchi nyingine? inawezekana magufuli akawa ameweka precedent ktk shauri hili. tijadili.
Tusiandikie mate,
tumsikilize Mh. Raila Odinga akimtambulisha Dr. Magufuli kama waziri wa ujenzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya dakika moja na sekunde 37 za mwanzo za clip hii na kuzungumzia kampeni yake ya kutaka Urais wa Kenya na kumtaka Dr. John Pombe Magufuli afikishe salamu za shukrani kwa mshikamano wake kumpa moyo juu ya hamu yake mh. Odinga kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya.:
Raila's speech during ODM delegates conference 07/Dec/2012
Source: ktnkenya.tv
Haswa, ndio alivyo siku zote.Tukisema Magufuli ni kichwamaji mnakataa!
Kama ni suala la urafiki angemtembelea nyumbani kwake na sio kwenye mkutano wa hadhara. Tusichanganye urafiki na dhamana tulizopewa.