Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,344
- 9,845
Maisha yanaenda yakibadilika kila siku,tekinoloji nayo inabadilika na hata uwezo wa watu wa kutazama mambo unabadilika.
Katika chaguzi zilizopita CCM haikuwa na kazi kubwa sana.Watu ambao hata bila kufanyiwa kampeni waliipigia kura CCM walikuwa wengi.Upinzani ulikuwa umegawanyika na haukuwa na wafuasi wengi sana.Ilikuwa rahisi sana kwa CCM kuhujumu,kudhulumu na kushinda hata kwa single moja tu ya kapteni Komba.
Jambo ambalo CCM hawajaweza kulimeng'enya ni kwanza kutambua athari ya muungano wa vyama vya upinzani na Pili athari ya Vigogo waliokuwa CCM waliohamia upinzani.
Mambo haya mawili yamebadili upepo katika uwanja wa kampeni na CCM ilipaswa kutambua hili.
Kwanza Muunganiko wa Upinzani umewafanya wafuasi wa upinzani kuwa kitu kimoja na kuzungumza lugha moja na hili limeongeza mara dufu wapiga kura wa mgombea wa upinzani wenye maamuzi tayari~decided voters.
Pili kuhamia upinzani kwa waliokuwa vigogo wa CCM kumeimega CCM kwa sehemu kubwa na waliomegeka ni wapiga kura wenye maamuzi tayari.
Ni kukosa kufikiri tu kutamfanya mgombea yoyote kati ya Lowasa na Magufuli wajinadi kwa wafuasi wachache ambao kimsingi ni wafia chama wa Act na TLP.
Kwenye kampeni za kisasa,vyama na wagombea huweka mikakati mingi juu ya wapigakura ambao hawajafanya maamuzi~undecided voters.
Swali linakuja,Wapiga kura ambao hawajafanya maamuzi ni wapi katika uchaguzi huu?
Jibu liko dhahiri; ni wanachama waliobakia CCM na wapiga kura wachache wasio na vyama.
Kampeni za toroka uje,vuka mto,ulipo tupo zinawalenga wapigakura waliobakia CCM.
Sera za elimu bure,riba kwa mkulima na nyingine zinawalenga wapigakura wasio na vyama zaidi!
Hii inaitwa "targeting in campaign".
CCM inauza sera za jumla jumla kwa watu wote.Unaweza kurusha jiwe kwenye kundi la ndege elfu usipate hata mmoja.
CCM haijui wafuasi wake kindakindaki wamebaki wangapi na wala imlenge nani,hii ni hatari kubwa.
Kampeni za tshirt,wali na kofia ni kampeni za kizamani.
Katika chaguzi zilizopita CCM haikuwa na kazi kubwa sana.Watu ambao hata bila kufanyiwa kampeni waliipigia kura CCM walikuwa wengi.Upinzani ulikuwa umegawanyika na haukuwa na wafuasi wengi sana.Ilikuwa rahisi sana kwa CCM kuhujumu,kudhulumu na kushinda hata kwa single moja tu ya kapteni Komba.
Jambo ambalo CCM hawajaweza kulimeng'enya ni kwanza kutambua athari ya muungano wa vyama vya upinzani na Pili athari ya Vigogo waliokuwa CCM waliohamia upinzani.
Mambo haya mawili yamebadili upepo katika uwanja wa kampeni na CCM ilipaswa kutambua hili.
Kwanza Muunganiko wa Upinzani umewafanya wafuasi wa upinzani kuwa kitu kimoja na kuzungumza lugha moja na hili limeongeza mara dufu wapiga kura wa mgombea wa upinzani wenye maamuzi tayari~decided voters.
Pili kuhamia upinzani kwa waliokuwa vigogo wa CCM kumeimega CCM kwa sehemu kubwa na waliomegeka ni wapiga kura wenye maamuzi tayari.
Ni kukosa kufikiri tu kutamfanya mgombea yoyote kati ya Lowasa na Magufuli wajinadi kwa wafuasi wachache ambao kimsingi ni wafia chama wa Act na TLP.
Kwenye kampeni za kisasa,vyama na wagombea huweka mikakati mingi juu ya wapigakura ambao hawajafanya maamuzi~undecided voters.
Swali linakuja,Wapiga kura ambao hawajafanya maamuzi ni wapi katika uchaguzi huu?
Jibu liko dhahiri; ni wanachama waliobakia CCM na wapiga kura wachache wasio na vyama.
Kampeni za toroka uje,vuka mto,ulipo tupo zinawalenga wapigakura waliobakia CCM.
Sera za elimu bure,riba kwa mkulima na nyingine zinawalenga wapigakura wasio na vyama zaidi!
Hii inaitwa "targeting in campaign".
CCM inauza sera za jumla jumla kwa watu wote.Unaweza kurusha jiwe kwenye kundi la ndege elfu usipate hata mmoja.
CCM haijui wafuasi wake kindakindaki wamebaki wangapi na wala imlenge nani,hii ni hatari kubwa.
Kampeni za tshirt,wali na kofia ni kampeni za kizamani.