CCM imepoteza fursa ya kumshauri rais?

CCM imepoteza fursa ya kumshauri rais?

mr mkiki

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
5,722
Reaction score
11,930
IMG_20170808_132358.jpg


Nitahitimisha mjadala huu kwa kuchambua makundi mawili yaliyopoteza fursa ya kumshauri rais wenu.

Kundi la kwanza la washauri rasmi wa rais ni baraza la mawaziri. Hiki ni chombo muhimu sana chenye hadhi ya juu ya kumshauri rais. Ni vema kueleweka kwamba baraza la mawaziri ni tanuru la fikra la rais.

Ndio maana katika baadhi ya nchi zenye mifumo dhabiti ya kitaasisi waziri mara baada ya kuteuliwa hutakiwa kudhibitishwa na mamlaka nyingine.Lengo ni kwamba mtu anayetakiwa kumshauri rais anapaswa kuwa mtu makini,mweledi na mwaadilifu. Mara nyingi bunge hutumika kama sehemu ya kuidhinisha wateule wa rais.

Bunge ni eneo nyeti lenye utakatifu na upekee wa aina yake. Viongozi wakubwa wa dunia,wafalme na wenye mamlaka hawapendi hata kutembelea maeneo ya bunge. Katika nchi zinazoheshimu demokrasia, Bunge lina heshima kubwa kuliko hata mhimili wa utawala na ule wa mahakama

Kwa sababu ndipo sheria hutungwa na ndipo viongozi wa mhimili wa utawala huidhinishwa, wakiwemo mawaziri na wateule wengeni wa mhimili wa utawala, Kwa hiyo,baraza la mawaziri ndipo chombo cha juu cha ushauri kwa taasisi ya urais.

Kuthibitisha hoja hiyo, Katiba ya jamhuri ya muungano ya mwaka 77 ibara 54(3) inasema "bila ya kuathiri masharti yaliyomo Katika ibara ya 37(1) ya katiba hii, Baraza LA mawaziri litakuwa ndicho chombo kikuu cha kumshauri raisi juu ya mambo yote yanayohusika na utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya katiba hii,na litamsaidia na kumshauri rais juu jambo lolote litakalowasilishwa kwenye baraza hilo kwa mujibu wa maagizo maalum au maagizo ya jumla yatakayotolewa na rais

Pamoja na ukweli huu, rais halazimishwi kufuta ushauri wa mtu yoyote. Anaweza kusikiliza ushauri, lakini asiufute. Anaweza akajigeuza mshauri mkuu wa kushauri washauri wake mwenyewe.

Mlolongo huo mrefu unaweza kutengeneza ugumu wa kumshauri rais, Kwan hofu kwamba, si lazima ushauri ufuate. Huu umekuwa mlima mwingine mrefu Sana kwa washauri hawa rasmi kuukwea. Wengi huchagua kukaa kimya kwa kuhofia kuwa wanaweza kueleweka vibaya ama wasaliti wa dhamira ya rais. Mara nyingi, viongozi wengi wa kiafrika hupenda sana kushauriwa yale wanayojishauri wenyewe wakiwa faragha!

Kundi la pili la washauri wa rasmi wa rais ni chama cha rais ambacho kinaingia moja kwa moja kwenye kundi rasmi la kumahauri. Sababu zipo mbili: mosi chama ndicho chenye ilani inayotekelezwa na serikali iliyopo madarakani.

Mifumo yetu ya uchaguzi inatoa fursa hiyo, yaani chama kinachoshinda kinachukua Lila kitu "winner take all". Katika msingi huohuo, CCM wanna turufu ya kumshauri rais, fursa wanayoanza kuipoteza sasa.

Pili, udhaifu wa serikali ni kushindwa kwa CCM. Chama cha mapinduzi Kama ilivyo kwa vyama vyote dola ndicho kilichoingia mkataba na wananchi.

Mkataba huu ni miaka mitano na mtekelezaji ni serikali.

Ni bahati mbaya Sana, CCM imepoteza fursa hiyo ya kitaasisi katika kuishauri serikali.










Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja yako nzuri lakini kama haijakamilika vizuri. Nahisi kama haujamailizia unachotaka kusema, mkuu funguka vizuri. Yani sema kabisa waziwazi hivyo unavyohisi hashauriwi vizuri ukitoa na mifano halisi.
 
Kabisa Mkuu mtu anayejiona anajua kila kitu kwa sababu tu ana Phd uchwara, wameshamgundua hao wapumbavu ndani ya Serikali yake wanamwambia kila atakacho kukisia ili kulinda ajira zao. Mfano alipokurupuka kuondoa nusu trillion kwenye mzunguko wa pesa nchini washauri wake wa uchumi walijua nini kitatokea lakini wakaamua kulinda ajira zao hivyo kukaa kimya.

Huyu babu unaanzia wapi kumshauri? acha aende anavyotaka na hivi ni mpenda sifa.
 
Kwani wapumbavu watashauri nini kwa aliyewateua hao wapumbavu na wala yeye siyo?? Alishasema hapangiwi cha kufanya,tulia muisome namba

Sent From Kisana Kiki Iphone
 
Kabisa Mkuu mtu anayejiona anajua kila kitu kwa sababu tu ana Phd uchwara, wameshamgundua hao wapumbavu ndani ya Serikali yake wanamwambia kila atakacho kukisia ili kulinda ajira zao. Mfano alipokurupuka kuondoa nusu trillion kwenye mzunguko wa pesa nchini washauri wake wa uchumi walijua nini kitatokea lakini wakaamua kulinda ajira zao hivyo kukaa kimya.
Huyu siyo binadamu ni nungu nungu mkuu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
View attachment 561145

Nitahitimisha mjadala huu kwa kuchambua makundi mawili yaliyopoteza fursa ya kumshauri rais wenu.

Kundi la kwanza la washauri rasmi wa rais ni baraza la mawaziri. Hiki ni chombo muhimu sana chenye hadhi ya juu ya kumshauri rais. Ni vema kueleweka kwamba baraza la mawaziri ni tanuru la fikra la rais.

Ndio maana katika baadhi ya nchi zenye mifumo dhabiti ya kitaasisi waziri mara baada ya kuteuliwa hutakiwa kudhibitishwa na mamlaka nyingine.Lengo ni kwamba mtu anayetakiwa kumshauri rais anapaswa kuwa mtu makini,mweledi na mwaadilifu. Mara nyingi bunge hutumika kama sehemu ya kuidhinisha wateule wa rais.

Bunge ni eneo nyeti lenye utakatifu na upekee wa aina yake. Viongozi wakubwa wa dunia,wafalme na wenye mamlaka hawapendi hata kutembelea maeneo ya bunge. Katika nchi zinazoheshimu demokrasia, Bunge lina heshima kubwa kuliko hata mhimili wa utawala na ule wa mahakama

Kwa sababu ndipo sheria hutungwa na ndipo viongozi wa mhimili wa utawala huidhinishwa, wakiwemo mawaziri na wateule wengeni wa mhimili wa utawala, Kwa hiyo,baraza la mawaziri ndipo chombo cha juu cha ushauri kwa taasisi ya urais.

Kuthibitisha hoja hiyo, Katiba ya jamhuri ya muungano ya mwaka 77 ibara 54(3) inasema "bila ya kuathiri masharti yaliyomo Katika ibara ya 37(1) ya katiba hii, Baraza LA mawaziri litakuwa ndicho chombo kikuu cha kumshauri raisi juu ya mambo yote yanayohusika na utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya katiba hii,na litamsaidia na kumshauri rais juu jambo lolote litakalowasilishwa kwenye baraza hilo kwa mujibu wa maagizo maalum au maagizo ya jumla yatakayotolewa na rais

Pamoja na ukweli huu, rais halazimishwi kufuta ushauri wa mtu yoyote. Anaweza kusikiliza ushauri, lakini asiufute. Anaweza akajigeuza mshauri mkuu wa kushauri washauri wake mwenyewe.

Mlolongo huo mrefu unaweza kutengeneza ugumu wa kumshauri rais, Kwan hofu kwamba, si lazima ushauri ufuate. Huu umekuwa mlima mwingine mrefu Sana kwa washauri hawa rasmi kuukwea. Wengi huchagua kukaa kimya kwa kuhofia kuwa wanaweza kueleweka vibaya ama wasaliti wa dhamira ya rais. Mara nyingi, viongozi wengi wa kiafrika hupenda sana kushauriwa yale wanayojishauri wenyewe wakiwa faragha!

Kundi la pili la washauri wa rasmi wa rais ni chama cha rais ambacho kinaingia moja kwa moja kwenye kundi rasmi la kumahauri. Sababu zipo mbili: mosi chama ndicho chenye ilani inayotekelezwa na serikali iliyopo madarakani.

Mifumo yetu ya uchaguzi inatoa fursa hiyo, yaani chama kinachoshinda kinachukua Lila kitu "winner take all". Katika msingi huohuo, CCM wanna turufu ya kumshauri rais, fursa wanayoanza kuipoteza sasa.

Pili, udhaifu wa serikali ni kushindwa kwa CCM. Chama cha mapinduzi Kama ilivyo kwa vyama vyote dola ndicho kilichoingia mkataba na wananchi.

Mkataba huu ni miaka mitano na mtekelezaji ni serikali.

Ni bahati mbaya Sana, CCM imepoteza fursa hiyo ya kitaasisi katika kuishauri serikali.










Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu bunge letu kibogoyo Linasubiri kukaushwa Mate
 
Si Kila washauri wanakua na Uwezo wa kushauri.
Miaka ya awamu ya nne, mamlaka hizo ulizotaja zilimshauri kwa kiwango cha ubora gani Mheshimiwa Jakaya Kikwete, mpaka kuambulia lawama lukuki toka kwa wapinzani na Wananchi kwa ujumla kwamba nchi imemshinda!
Tuanzie hapo.
Mfumo unaouelezea hapa ni colonialism system.
Inawezakana ukaleta matunda au la.

Wakati nchi inapigwa kwa ufisadi, huku Rais Kikwete kiguu na njia, nchi za ughaibuni, Baraza la mawaziri na Chama mpaka kufikia kupelekea kutaka kutolewa madarakani na upinzani, nn ushauri huo ulipelekea?
Tuache Rais Magufuli atumikie wapiga kura wake.
Muda ukiisha, atoke tumchambue ubora na ubaya wake, kama tulivyofanya kwa Kikwete


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom