CCM imelaaniwa - mhadhiri

Mwamba Usemao Kweli

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
744
Reaction score
186
CCM imelaaniwa - Mhadhiri

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinakabiliwa na hali ngumu sasa kutokana na laana ya kushindwa kufuata misingi iliyoasisiwa na viongozi wa chama hicho.Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally, alitoa kauli hiyo mjini hapa jana kwenye mkutano mkuu wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) unaoendelea.

Alisema waanzilishi wa chama hicho waliwaunganisha wakulima na wafanyakazi na kufanikiwa kupata uhuru, lakini viongozi wa sasa wamewaweka pembeni watu hao."TANU wakati ule ilifanikiwa kuondoa dola ya mkoloni kwa kuwaunganisha wakulima na wafanyakazi ingawa haikuwa na polisi wala fedha," alisema.

Alisema kwa sasa vyama vinatumia polisi kujiimarisha na hata kutumia fedha kupata madaraka, hivyo laana hiyo itaendelea kuwatafuna."Msijione wanyonge, ninyi ni mashujaa wa uhuru na wala msikate tamaa…ninyi ni maaskari wa akiba," alisema mhadhiri huyo akiwaambia wakulima.

Alisema tatizo lililopo ni kutokana na dola ‘kushirikiana kitanda kimoja' na watu wenye fedha, jambo ambalo linasababisha wakulima kuendelea kudidimia siku hadi siku.

Aidha, alisema Baba wa Taifa hayati Mwalimu Nyerere alikiri kukosea mambo mawili ambayo ni kuua vyama vya wakulima pamoja na kutoimarisha uongozi wa serikali za vijiji na mitaa ambavyo vingekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wakulima nchini.

Aliwataka wakulima kupigania vita ya hoja kwa kuwa haiwezekani kuwa na mifumo zaidi ya mmoja katika sekta moja.

SOURCE: TANZANIA DAIMA

 
ni kweli wamelaaniwa kwa jinsi ninavyona wanavyokwenda kweli wanalaana tena mbaya na ya hatari kwa afya ya tanzania. mabomu, tindikali, ubaguzi, ukabila, pembe za ndovu, madawa ya kulevya, kutorosha wanyama pori hai, madini yetu kuchukuliwa na wageni, kutolipa wakulima kwa wakati na kwa bei ya chini, shule za kata elimu duni na kukaa chini, hospitali huduma duni, kuombaomba mataifa ya kigeni, kudhurura kutwa kucha kwa fastjet, kutoa kucha na meno raia wema n.k.
 
Na yazidi kulaaniwe zaidi maCCM.... katibu likuu lao kazi kuuza tembo tu, kila siku wanauwa tembo zaidi ya 80.... na laani kibao.
 
Mbaya zaidi waliotoa hiyo laana wametangulia mbele ya haki.
 
Mkuu Bushiru Ally, angalia kibarua kisije ota nyasi, jamaa hawataki kusemwa hadharani kabisa!!
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinakabiliwa na hali ngumu sasa kutokana na laana ya kushindwa kufuata misingi iliyoasisiwa na viongozi wa chama hicho.


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally, alitoa kauli hiyo mjini hapa jana kwenye mkutano mkuu wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) unaoendelea.


Alisema waanzilishi wa chama hicho waliwaunganisha wakulima na wafanyakazi na kufanikiwa kupata uhuru, lakini viongozi wa sasa wamewaweka pembeni watu hao.


“TANU wakati ule ilifanikiwa kuondoa dola ya mkoloni kwa kuwaunganisha wakulima na wafanyakazi ingawa haikuwa na polisi wala fedha,” alisema.
Alisema kwa sasa vyama vinatumia polisi kujiimarisha na hata kutumia fedha kupata madaraka, hivyo laana hiyo itaendelea kuwatafuna.


“Msijione wanyonge, ninyi ni mashujaa wa uhuru na wala msikate tamaa…ninyi ni maaskari wa akiba,” alisema mhadhiri huyo akiwaambia wakulima.
Alisema tatizo lililopo ni kutokana na dola ‘kushirikiana kitanda kimoja’ na watu wenye fedha, jambo ambalo linasababisha wakulima kuendelea kudidimia siku hadi siku.


Aidha, alisema Baba wa Taifa hayati Mwalimu Nyerere alikiri kukosea mambo mawili ambayo ni kuua vyama vya wakulima pamoja na kutoimarisha uongozi wa serikali za vijiji na mitaa ambavyo vingekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wakulima nchini.


Aliwataka wakulima kupigania vita ya hoja kwa kuwa haiwezekani kuwa na mifumo zaidi ya mmoja katika sekta moja.
 
Yani neno "Laana" ni kali sana kulitumia kisa ni mpinzani wako kimawazo ,kimtazamo au kisiasa.Ni vyema tutafute maneno mengine ya kuyatumia ilihali heshima zetu tunaendelea kuzitunza
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinakabiliwa na hali ngumu sasa kutokana na laana ya kushindwa kufuata misingi iliyoasisiwa na viongozi wa chama hicho.


Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally, alitoa kauli hiyo mjini hapa jana kwenye mkutano mkuu wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) unaoendelea.


Alisema waanzilishi wa chama hicho waliwaunganisha wakulima na wafanyakazi na kufanikiwa kupata uhuru, lakini viongozi wa sasa wamewaweka pembeni watu hao.


“TANU wakati ule ilifanikiwa kuondoa dola ya mkoloni kwa kuwaunganisha wakulima na wafanyakazi ingawa haikuwa na polisi wala fedha,” alisema.


Alisema kwa sasa vyama vinatumia polisi kujiimarisha na hata kutumia fedha kupata madaraka, hivyo laana hiyo itaendelea kuwatafuna.


“Msijione wanyonge, ninyi ni mashujaa wa uhuru na wala msikate tamaa…ninyi ni maaskari wa akiba,” alisema mhadhiri huyo akiwaambia wakulima.


Alisema tatizo lililopo ni kutokana na dola ‘kushirikiana kitanda kimoja’ na watu wenye fedha, jambo ambalo linasababisha wakulima kuendelea kudidimia siku hadi siku.


Aidha, alisema Baba wa Taifa hayati Mwalimu Nyerere alikiri kukosea mambo mawili ambayo ni kuua vyama vya wakulima pamoja na kutoimarisha uongozi wa serikali za vijiji na mitaa ambavyo vingekuwa mstari wa mbele kupigania haki za wakulima nchini.


Aliwataka wakulima kupigania vita ya hoja kwa kuwa haiwezekani kuwa na mifumo zaidi ya mmoja katika sekta moja.
 
Umesema..
"Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally, alitoa kauli hiyo mjini hapa jana kwenye mkutano mkuu wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) unaoendelea...."

Mjini wapi huko mkuu?
 
yani neno "laana" ni kali sana kulitumia kisa ni mpinzani wako kimawazo ,kimtazamo au kisiasa.ni vyema tutafute maneno mengine ya kuyatumia ilihali heshima zetu tunaendelea kuzitunza
hakuna nenolingine linalo wafaa zaidi ya hilo
 
CCM imelaaniwa mpaka inatia huruma!!!!!!!!
 
C C M Chota Chako Mapema C U F Chukua Ule Fasta N C C R Nenda Chukua Chako Rudi"MAGEUZI"U D P Upatapo Donge Ponda. D P P Dumisha Papara ya Pesa C H A D E M A Chukua Hatua Ambazo Daima ni Endelevu kwa Maisha ya Amani.
Umeandika vizuri sana... Hongera sana
 

Nimeipenda ya CHADEMA. Take like...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…