CCM ilihamisha mzoga ili kuondoa nzi!!

CCM ilihamisha mzoga ili kuondoa nzi!!

funaku

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2011
Posts
38,535
Reaction score
31,199
Hii ni kauli ya Katibu wa CCM Morogoro.

Walichofanya kina Mangula baada ya kuona nzi wamezunguka mzoga na waliamua kuondoa mzoga.

Ukawa wamepokea Mzoga sasa wana kazi ya kufukuza nzi.
 
Mhh haya bwana hata kama ni siasa kuita mtu mzoga.

Sidhani kama wanamaanisha Lowassa ni mzoga, literally! Wanamaanisha matatizo yaliyokuwa yanawakosesha usingizi ccm, sasa wameyahamishia UKAWA...si mnaona sasa mnavyokosa usingizi??
 
Hivi escrow lowasa alikula billion ngapi? Ccm wanamizoga mingi sana, sana sana na kuna vimizoga nimeota vingine vimeongezeka Mwana wa mwenye nyumba na yule February Mauzi
 
  1. MaKapi
  2. Oil chafu
  3. Wapumbavu
  4. MaLofa
  5. Mzoga
  6. ......
  7. .......
Hadi 25 Oktoba tutasikia mengi sana. Kama una kikatio chako tukutane kwenye sanduku la kura!
 
Wanaangahika sana.Watakuja na misamiati,wanajiona wao hawatoshi hadi wanakodi akina Slaa,Makamba,lakini msimamo wetu bado upo pale pale.Watueleze miaka 53 ya kuongoza.nchi wametufanyia nn.Mm nina uhakika wakati Mwalimu anapokea nchi toka kwa wakoloni hakuna mwanafunzi aliyekuwa anakalia kipande cha tofali na pia madawa yalikuwa tele kwenye hospitali zetu.Mwaka 70 mliwakaribisha hao wazungu kuja kuona tulikofikia.Leo ni miaka 53 sijasikia tena mnawaita waje kuona.maenderleo yetu.Mtadai labda wakina Turnbul wameshakufa.Mwiteni hata. mtoto wa Elzabeth aje aone
Mnaona aibu.Dola 1 ilikuwa shs7.50 wakati mnakabidhiwa nchi.Hatutaki cha muadhin wala mnadi sala.Nendeni kando kwanza tuanze kujipanga upya.Hii ni zaidi ya aibu.
 
Mkapa kaita watanzania malofa.Huyu naye anawaita nzi.Hivi hii ni ccm ya Nyerere kweli ?Nyerere umetuacha leo sisi tunaitwa wapumbavu,malofa,nzi,na mizoga kweli! Ulofa na upumbavu wetu nani kasababisha?kama leo watanzania tunabaguana na kuitana haya majina ni UJINGA uliokithiri hasa kwa hao wasiojizuia kutukana.
 
Wanaangahika sana.Watakuja na misamiati,wanajiona wao hawatoshi hadi wanakodi akina Slaa,Makamba,lakini msimamo wetu bado upo pale pale.Watueleze miaka 53 ya kuongoza.nchi wametufanyia nn.Mm nina uhakika wakati Mwalimu anapokea nchi toka kwa wakoloni hakuna mwanafunzi aliyekuwa anakalia kipande cha tofali na pia madawa yalikuwa tele kwenye hospitali zetu.Mwaka 70 mliwakaribisha hao wazungu kuja kuona tulikofikia.Leo ni miaka 53 sijasikia tena mnawaita waje kuona.maenderleo yetu.Mtadai labda wakina Turnbul wameshakufa.Mwiteni hata. mtoto wa Elzabeth aje aone
Mnaona aibu.Dola 1 ilikuwa shs7.50 wakati mnakabidhiwa nchi.Hatutaki cha muadhin wala mnadi sala.Nendeni kando kwanza tuanze kujipanga upya.Hii ni zaidi ya aibu.

"Wetu"?? sema msimamo wako, wengine kuna maswali tumejiuliza (siyo ya ufisadi) mengine tu na tumerudi kwa Makufili. Tutajipanga tena.
 
Hii ni kauli ya Katibu wa CCM Morogoro.

Walichofanya kina Mangula baada ya kuona nzi wamezunguka mzoga na waliamua kuondoa mzoga.

Ukawa wamepokea Mzoga sasa wana kazi ya kufukuza nzi.

Mizoga bado ipo ndani ya ccm
 

Attachments

  • 1441623412166.jpg
    1441623412166.jpg
    97.1 KB · Views: 297
Sera yao ni matusi, Mwaka huu watakula matusi
 
Mbona wale nzi wakubwa wa rangi ya kijani bado wanaonekana katika mikutano ya CCM?Mfano:BWM,JMK,AT,AC n.k!
 
Back
Top Bottom