MSHINO
JF-Expert Member
- Jul 26, 2013
- 1,069
- 713
TANGU kuanza kwa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010, kumekuwa na mjadala mahsusi kuhusu sera ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ya kutoa elimu bure kuanzia ngazi ya chekechea hadi kidato cha sita.
Sera hii imepingwa na kuzomewa vikali na Chama cha Mapinduzi (CCM). Binafsi awali sikutilia manani upinzani wa kutoa elimu bure kwa sababu ulitolewa na Kampeni Meneja wa chama hicho, Abdulrahmani Kinana, nikidhani kwamba alifanya hivyo kwa sababu za kisiasa na kipropaganda ukizingatia kwamba vyama vya siasa viko katika ushindani mkubwa wa kuomba ridhaa ya wapiga kura.
Hata hivyo, nimeanza kutilia manani upinzani huu baada ya Rais Jakaya Kikwete naye kujitokeza hadharani kupinga sera hii na kuungwa mkono na aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta. Upinzani wa sera hii kutoka kwa viongozi hawa wakuu katika nchi yetu umetia uzito wa kipekee hoja ya kwamba elimu bure haiwezekani kutolewa katika nchi maskini kama Tanzania.
Bila kufafanua dhana ya kutoa elimu bure na uwezekano wake, wananchi wataanza kuamini kwamba hili ni jambo lisilowezekana hasa watapoambiwa na viongozi wa chama tawaka na serikali yake. Ufafanuzi huu ni muhimu ukizingatia kuwa tupo katika jamii ambayo imejengwa katika mfumo wa kipropaganda wa kuamini au kuaminishwa kuwa chochote kinachosemwa na viongozi wa serikali na chama tawala kuwa ni kweli.
Aidha bado kuna watu katika jamii yetu ambao hutilia shaka chochote kinachosemwa na viongozi wa vyama vya upinzani na wanaharakati wengine, bila kuzingatia mantiki ya hoja.
Pengine kabla ya kufafanua juu ya uwezekano wa kutoa elimu bure, ni vizuri kuweka kumbukumbu sawa. CCM wana historia ya kupinga sera zenye kujaribu kuwapunguzia wananchi makali ya maisha, na hawajaanza na hili la elimu bure.
Itakumbukwa kuwa mwaka 1995 wapinzani waliahidi kufuta kodi ya kichwa (CCM waliita kodi ya maendeleo) ambayo ilikuwa inaleta adha kubwa kwa wananchi hadi wengine kufikia hatua ya kujificha porini ili wasikamatwe na askari mgambo.
CCM walipinga vikali sera hii wakisema kuwa haiwezekani kuendesha serikali bila kodi hiyo. Hata hivyo, baada ya uchaguzi mkuu wa 1995 serikali ya CCM iliifuta kodi hii, aghalabu kwa shinikizo.
Mwaka 2000 wapinzani walikuja na sera ya kufuta ada katika shule za msingi kama njia ya kuwawezesha watoto wengi zaidi kujiunga na elimu ya msingi. Kama kawaida yao, CCM walicharuka tena wakidai kuwa wapinzani wanaota ndoto.
Hata hivyo baada ya uchaguzi wa 2000 ada katika shule za msingi ilifutwa, japokuwa kwa shinikizo kubwa la Benki ya Dunia. Kwa hiyo, kwamba CCM leo hii wanapinga vikali tena bila aibu sera ya elimu bure sio jambo la kustaajabu.
Pengine jambo pekee la kustajaabu ni kwamba wapinzani wa sera ya elimu bure ni viongozi wa chama kinachojiita cha kijamaa. Haingii akilini hata kidogo kwa kiongozi wa chama kinachojiita cha ujamaa kupinga sera ya kutoa elimu bure. Msingi wa ujamaa ni usawa na fursa kwa wote.
Wana ujamaa popote walipo wanakubaliana kwamba njia rahisi ya kufikia usawa na kutoa fursa kwa kila mtu ni kuhakikisha kwamba elimu na huduma zingine za jamii zinamfikia kila mtu. Ili kutimiza hili, wana ujamaa wanakubaliana pia kwamba ni muhimu na lazima kwa huduma hizi kugharamiwa na serikali bila wananchi kuzilipia moja kwa moja.
Hii ni mantiki ya msingi ya ujamaa ambayo mwanachama wa kawaida wa chama kinachojiita cha kijamaa anapaswa kuielewa, achilia mbali kiongozi wake.
Wapinzani wa sera ya kutoa elimu bure wametumia kigezo cha gharama katika kuhalalisha upinzani wao. Kwamba haiwezekani kutoa elimu bure kwa sababu kufanya hivyo itamaanisha serikali iache kutekeleza majukumu mengine ya msingi.
Katika makala hii ninaonyesha kwa ufupi sana jinsi ambavyo inawezekana kwa serikali kulipia gharama ya elimu kwa kutumia fedha za walipa kodi bila kumbebesha mzazi gharama za ziada.
Katika kufanya hivi nitaenda hatua kwa hatua, nikianzia na kufafanua dhana ya elimu bure kwa mazingira ya Tanzania, na kubainisha vyanzo mbadala vya mapato kwa serikali ili iweze kulipia kikamilifu gharama za elimu na huduma zingine za jamii.
Chanzo:Tanzania Daima
Sera hii imepingwa na kuzomewa vikali na Chama cha Mapinduzi (CCM). Binafsi awali sikutilia manani upinzani wa kutoa elimu bure kwa sababu ulitolewa na Kampeni Meneja wa chama hicho, Abdulrahmani Kinana, nikidhani kwamba alifanya hivyo kwa sababu za kisiasa na kipropaganda ukizingatia kwamba vyama vya siasa viko katika ushindani mkubwa wa kuomba ridhaa ya wapiga kura.
Hata hivyo, nimeanza kutilia manani upinzani huu baada ya Rais Jakaya Kikwete naye kujitokeza hadharani kupinga sera hii na kuungwa mkono na aliyekuwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta. Upinzani wa sera hii kutoka kwa viongozi hawa wakuu katika nchi yetu umetia uzito wa kipekee hoja ya kwamba elimu bure haiwezekani kutolewa katika nchi maskini kama Tanzania.
Bila kufafanua dhana ya kutoa elimu bure na uwezekano wake, wananchi wataanza kuamini kwamba hili ni jambo lisilowezekana hasa watapoambiwa na viongozi wa chama tawaka na serikali yake. Ufafanuzi huu ni muhimu ukizingatia kuwa tupo katika jamii ambayo imejengwa katika mfumo wa kipropaganda wa kuamini au kuaminishwa kuwa chochote kinachosemwa na viongozi wa serikali na chama tawala kuwa ni kweli.
Aidha bado kuna watu katika jamii yetu ambao hutilia shaka chochote kinachosemwa na viongozi wa vyama vya upinzani na wanaharakati wengine, bila kuzingatia mantiki ya hoja.
Pengine kabla ya kufafanua juu ya uwezekano wa kutoa elimu bure, ni vizuri kuweka kumbukumbu sawa. CCM wana historia ya kupinga sera zenye kujaribu kuwapunguzia wananchi makali ya maisha, na hawajaanza na hili la elimu bure.
Itakumbukwa kuwa mwaka 1995 wapinzani waliahidi kufuta kodi ya kichwa (CCM waliita kodi ya maendeleo) ambayo ilikuwa inaleta adha kubwa kwa wananchi hadi wengine kufikia hatua ya kujificha porini ili wasikamatwe na askari mgambo.
CCM walipinga vikali sera hii wakisema kuwa haiwezekani kuendesha serikali bila kodi hiyo. Hata hivyo, baada ya uchaguzi mkuu wa 1995 serikali ya CCM iliifuta kodi hii, aghalabu kwa shinikizo.
Mwaka 2000 wapinzani walikuja na sera ya kufuta ada katika shule za msingi kama njia ya kuwawezesha watoto wengi zaidi kujiunga na elimu ya msingi. Kama kawaida yao, CCM walicharuka tena wakidai kuwa wapinzani wanaota ndoto.
Hata hivyo baada ya uchaguzi wa 2000 ada katika shule za msingi ilifutwa, japokuwa kwa shinikizo kubwa la Benki ya Dunia. Kwa hiyo, kwamba CCM leo hii wanapinga vikali tena bila aibu sera ya elimu bure sio jambo la kustaajabu.
Pengine jambo pekee la kustajaabu ni kwamba wapinzani wa sera ya elimu bure ni viongozi wa chama kinachojiita cha kijamaa. Haingii akilini hata kidogo kwa kiongozi wa chama kinachojiita cha ujamaa kupinga sera ya kutoa elimu bure. Msingi wa ujamaa ni usawa na fursa kwa wote.
Wana ujamaa popote walipo wanakubaliana kwamba njia rahisi ya kufikia usawa na kutoa fursa kwa kila mtu ni kuhakikisha kwamba elimu na huduma zingine za jamii zinamfikia kila mtu. Ili kutimiza hili, wana ujamaa wanakubaliana pia kwamba ni muhimu na lazima kwa huduma hizi kugharamiwa na serikali bila wananchi kuzilipia moja kwa moja.
Hii ni mantiki ya msingi ya ujamaa ambayo mwanachama wa kawaida wa chama kinachojiita cha kijamaa anapaswa kuielewa, achilia mbali kiongozi wake.
Wapinzani wa sera ya kutoa elimu bure wametumia kigezo cha gharama katika kuhalalisha upinzani wao. Kwamba haiwezekani kutoa elimu bure kwa sababu kufanya hivyo itamaanisha serikali iache kutekeleza majukumu mengine ya msingi.
Katika makala hii ninaonyesha kwa ufupi sana jinsi ambavyo inawezekana kwa serikali kulipia gharama ya elimu kwa kutumia fedha za walipa kodi bila kumbebesha mzazi gharama za ziada.
Katika kufanya hivi nitaenda hatua kwa hatua, nikianzia na kufafanua dhana ya elimu bure kwa mazingira ya Tanzania, na kubainisha vyanzo mbadala vya mapato kwa serikali ili iweze kulipia kikamilifu gharama za elimu na huduma zingine za jamii.
Chanzo:Tanzania Daima