Naitazama CCM ya JK kama timu ya mpira ambapo Golini yupo mzee mzima JK ambapo pamoja na umahiri wake wa kupiga dana dana mijadala ya kisiasa ni dhahiri kwamba atafungwa tu kutokana na beki wake no mbili bwana Billal kuwa bize sana na kuhudhuria misiba na kuwa mgeni rasmi kwenye funguzi za saccos...
Namba tatu akiwa bwana mkubwa Pinda ambaye hatujui kwanini kakabidhiwa no hiyo huku akiangushwa na no tano (kwa maana ya baraza zima la mawaziri) ambao jukumu lao lilitakiwa kufuta makosa ya watendaji wakuu wa serikali...
No nne tulitegemea sana wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha wanapambana na mipira iliyomshinda golikeeper na kumiliki mikiki mikiki ya mashambulizi ya upinzani ( Wananchi) kwa kuhakikisha wanasimamia haki...
No sita na nane ni watendani wa kada mabli mbali za serikali mfano ualimu,masuala ya kilimo na ufugaji ambao kama wangetabua majukumu yao hasa uwanjani wangehakikisha wanachezesha samba ambalo mashabiki wangekua na uhakika wa ushindi kwa maana ya maisha bora!
No saba haingekuwa na umuhimu sana ikiwa beki no mbili angesimama vizuri kwa kuwa nilitaraji angekuwa na uwezo wa kupanda na kushuka...
No tisa walistahili kusimama makada waandamizi wa chama ambao kazi yao kubwa ni kukaa na mabeki wa upinzani ili kuwamaliza kisaikologia na kuirahisishia no kumi na moja ya chama ambayo ni utekelezaji mzuri wa sera na ahadi kupiga mashuti golini huku watendaji wa serikali za wilaya na mitaa wakisimama no kumi kumalizia mipira iliyotemwa na golikipa wa upinzani wakati akipangua mashuti ya no 11..