CCM beki hazikabi

CCM beki hazikabi

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Sasa ni dhahiri kuwa CCM inazidiwa ujanja wa kisiasa na CHADEMA na wengineo. Wakati CHADEMA,wapinzani wetu wa jadi, wakichanja mbuga na kupasua anga kwa chopa kujenga chama chao,sisi CCM tunaketi maofisini na kupiga majungu na kujadili makundi/kambi ndani ya chama. Sasa tunaelekea pabaya. Kama chama tawala,inabidi tujipange upya kupambana kisiasa.

Kutwa kucha kushinda Lumumba, Makao Makuu Dodoma na Ofisi nyinginezo kupanga makundi ndani ya chama na kuchagua pa kuibuka napo 2015.Basi. Kweli!? Kwani viongozi wa 2015 tutachagua sisi CCM peke yetu? Si wananchi wote wa Tanzania wenye umri na sifa nyinginezo za kupiga kura? Hatufanyi haki kwa chama chetu. Tunakiangamiza.

Umefika wakati wa mabadiliko. Matamko ya Katibu wa Itikadi na Uenezi hayatakibeba chama. Nasi twende kwa wanachi.Wao pale;sisi kule. Tusibaki maofisini na kuishia kupendekeza kufukuzana kwa wale wanaothubutu kuendana na moto wa demokrasia yasasa ya nchi. Mambo yamebadilika. Siasa imeimarika. Majungu,fitina,makundi,kubweteka na kujiamini ndio maadui wakuu wa kukiangamiza chama chetu cha CCM.

Tubadilike.Tuwajibike.Tusonge mbele.Kwa hali ilivyo sasa (kwakuwa nimetembelea mikoa mbalimbali na kushuhudia shughuli za chama), CCM beki hazikabi.Watendaji badala ya kutegemea hoja zao na yale yaliyotekelezwa Kiilani,wao wanategemea vyombo vya dola. Hii haisaidii. Tunapotea. Hata kama hatuna chopa,twende hata na magari. Muda ni huu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Mkuu bado hujapona,hakika nakuambia make yote uliyoeleza yanaihusu chadema sijui kama hujaligundua hilo au umejua halafu ukajifanya hujui make bavicha kwa vituko hamjambo.
 
Unasikitisha unampigia mbuzi gitaa
Kweli mkuu kwa chama kama chadema ambacho kimepoteza kabisa mwelekeo halafu unakaa unakipigia hadithi kama hizi ni kutungwa maji kwenye kinu.
 
Mkuu bado hujapona,hakika nakuambia make yote uliyoeleza yanaihusu chadema sijui kama hujaligundua hilo au umejua halafu ukajifanya hujui make bavicha kwa vituko hamjambo.
dada tulia sindano ikuingie....
 
Mkuu bado hujapona,hakika nakuambia make yote uliyoeleza yanaihusu chadema sijui kama hujaligundua hilo au umejua halafu ukajifanya hujui make bavicha kwa vituko hamjambo.

Avatar yako nzuri sana; inatayarisha masabuli(makalio)
 
Kweli mkuu kwa chama kama chadema ambacho kimepoteza kabisa mwelekeo halafu unakaa unakipigia hadithi kama hizi ni kutungwa maji kwenye kinu.

dada angu juzi ulisahau pampers pale ambience....vp ulikumbuka kuzifuata??
 
Mkuu bado hujapona,hakika nakuambia make yote uliyoeleza yanaihusu chadema sijui kama hujaligundua hilo au umejua halafu ukajifanya hujui make bavicha kwa vituko hamjambo.

aliyekuroga yuko sudan kusin sijui utafikaje.
 
John Guninita vs Nnape Nnauye
Philip Mangula vs Edward Lowassa
Samwel Sitta vs Benard Membe
Khamis Kagasheki vs Amani Anatoly

Kazi ipo!
 
Mkuu bado hujapona,hakika nakuambia make yote uliyoeleza yanaihusu chadema sijui kama hujaligundua hilo au umejua halafu ukajifanya hujui make bavicha kwa vituko hamjambo.

Mtoto mantashahu ka bata ushungu...ukiruka ruka hivi dozi ndo inakuingia maridhiwa kabisa
 
Kweli mkuu kwa chama kama chadema ambacho kimepoteza kabisa mwelekeo halafu unakaa unakipigia hadithi kama hizi ni kutungwa maji kwenye kinu.

Du!! Inawezekana we ukawa sio mtu wa kawaida aisee!!!.
 
Naitazama CCM ya JK kama timu ya mpira ambapo Golini yupo mzee mzima JK ambapo pamoja na umahiri wake wa kupiga dana dana mijadala ya kisiasa ni dhahiri kwamba atafungwa tu kutokana na beki wake no mbili bwana Billal kuwa bize sana na kuhudhuria misiba na kuwa mgeni rasmi kwenye funguzi za saccos...

Namba tatu akiwa bwana mkubwa Pinda ambaye hajui kwanini kakabidhiwa no hiyo huku akiangushwa na no tano (kwa maana ya baraza zima la mawaziri) ambao jukumu lao lilitakiwa kufuta makosa ya watendaji wakuu wa serikali...

No nne tulitegemea sana wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha wanapambana na mipira iliyomshinda golikeeper na kumiliki mikiki mikiki ya mashambulizi ya upinzani ( Wananchi) kwa kuhakikisha wanasimamia haki...

No sita na nane ni watendani wa kada mabli mbali za serikali mfano ualimu,masuala ya kilimo na ufugaji ambao kama wangetabua majukumu yao hasa uwanjani wangehakikisha wanachezesha samba ambalo mashabiki wangekua na uhakika wa ushindi kwa maana ya maisha bora!

No saba haingekuwa na umuhimu sana ikiwa beki no mbili angesimama vizuri kwa kuwa nilitaraji angekuwa na uwezo wa kupanda na kushuka...

No tisa walistahili kusimama makada waandamizi wa chama ambao kazi yao kubwa ni kukaa na mabeki wa upinzani ili kuwamaliza kisaikologia na kuirahisishia no kumi na moja ya chama ambayo ni utekelezaji mzuri wa sera na ahadi kupiga mashuti golini huku watendaji wa serikali za wilaya na mitaa wakisimama no kumi kumalizia mipira iliyotemwa na golikipa wa upinzani wakati akipangua mashuti ya no 11..
 
kwa CCM ni kipindi cha mavuno baada ya kampeni ya baba, mama na watoto (BMW) we ulidhan walikua wanafanya umisionari.
 
Hahahaha!! siyo beki pekee isiyokaba karibu timu nzima hakuna kitu! Kapteni mwenyewe haeleweki kuwa anacheza mechi gani kila siku kiguu na njia... nasikitika sana! Uongozi wote wa ccm ni uwozo, tangu mwenyekiti wao hadi wajumbe wa nyumba kumi. Ndiyo maana mbinu ya kubeba watu mikutanoni haikemewi na viongozi wao: Hii ni aibu sana!!
 
Kweli mkuu kwa chama kama chadema ambacho kimepoteza kabisa mwelekeo halafu unakaa unakipigia hadithi kama hizi ni kutungwa maji kwenye kinu.
angalia tu usijeota kibiongo maana ni zaidi ya ushabiki Chadema isijeringanishwa na CCM hata siku moja chama kinachorudisha nchi miaka mia moja nyuma sio cha kujidai nacho ndio maana umewekwa kuzuia mashambulizi 24/7 sijui unalala na kuenda chooni saa ngapi
 
Beki kama ya Man u Wanakaba kwa Macho na kumkaribisha adui aingi kwenye sita .....Aguero akuachiiiiiii!:A S 27:
 
Back
Top Bottom