Career vs Family

Anfibix

Senior Member
Joined
Dec 1, 2018
Posts
190
Reaction score
308
Habari wakuu. Kuna swala naomba tushirikiane maana imekua argument. Kutokana na maswala ya matatizo ya uzazi kuongezeka siku hadi siku na mfumo wa kimaisha ulivyo ambapo wengi huchelewa kupata watoto sababu ya kusubiri kuwa na kipato cha kutosha au ndoa, so mtu anajikuta anaanza kutafuta mtoto from 29 na kuendelea. Je hili swala ni sawa na je ni vyema kutanguliza familia au career (kazi) kwenye maisha? Na je ni vipi tutaweza kukabiliana na maswala ya uzazi hasa pale umri unapoenda bila kuwa na kipato cha kutosha kulea mtoto. Asanteni
 
Ukizaa mtoto huku hauna namna ya kumlea hilo ni tatizo.
Ni bora kupambana na maisha upate namna ya kumlea mtoto wenu.
Lakini haimaanishi ndiyo upambane hadi uzeeke, no pambana ukiwa bado kijana mbichi 20-30. Baada ya hapo utakuwa na uwezo wa kulea watoto.
 
Huwa nakutana na hili swali mara nyingi, kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki. Huwa nalijibu kwa maswali mawili, maybe yanaweza kusaidia

1. Kama unatafuta kipato kwanzo, what are you doing differently? Maana wengi tunasema natafuta kipato kwanza lakini hakuna cha ziada unachofanya zaidi ya kuamka asubuhi kwenda kazini kurudi jioni. The same thing day after day.

Kama umeamua kupambana kwanza, pambana kweli basi, la sivyo you are just wasting time.

2. Una malengo gani? Mostly in terms of time. Yaani, wewe upo tayari kusubiri mpaka umri gani? Then unafanya nini in the mean time.

Usually muda wa kuwa na familia ni maamuzi ya mtu. Lakini vile vile hutaki mtoto wako akuite babu or bibi.
Weka clear malengo, kama ni kujenga maisha kwanza, jua ni maisha gani unayo yataka uyapate kabla ya maisha? Unafanya nini kuyapata?

Kuna situations ambazo kuwa na familia inakupa motivation ya ku move forward. Au partner wako akawa msaada mkubwa kwenye maendeleo yako badala ya kupambana mwenyewe.
 
Very true. Na unakutana na hilo swali cause ni dilemma kubwa kwa sisi vijana. Kazi na familia vyote ni muhimu, tatzo linakuja jinsi ya kuvibalance
 
Je ukichelewa kupata hicho kipato. Maana riziki znatofautiana??
 
Kila kitu kina muda wake, mpango wake na malengo pia. Vile vile maisha yetu hayafanani ndo maana wapo wanaozaa na miaka 20 na wengine 30na hata wengine 18!

Pale mtu atakapojihisi yupo tayari afanye tuu maamuzi yake!
Unaweza ukawa tayari ila hali na watu wanaokuzunguka vikapingana na hilo [emoji848]
 
mwenzangu ukifikisha 40,huna mtoto tafuta hata kwa vituo vya yatima,u adopt,life limekua challenging sio kwa sisi wanawake tu...hata wakaka wanahofia kuzaa pasipo na kipato cha kueleweka cha kumlea huyo mtoto
 
Career na family ni vitu viwili ambavyo vinapatikana in two different worlds na vina sarve 2 different purposes, kila kimoja kina muda na nafasi yake.

Kuna watu walianza kupata familia when they had nothing lakini wakatengeneza career zao wakiwa pia wanaendelea kutengeneza familia zao. Wapo pia walioanza kutengeneza career zao na familia zikaja baadae. Wengine walianza career at the same time wakaanzisha familia.
 
sijuka kama mleta mada unaelewa tofauti iliyopo kati ya career na kipato. binafsi nadhani hivi ni vitu viwili tofauti.
Kama Sakayo alivyo sema kila mtu na malengo yake kwani pia kuna watu unakuta yuko vizuri lakini bado hana hajafikilia kuoa ama hajaoa kwa sababu anazozijua yeye binafsi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…