Cape Verde yaishangaza dunia!

Kile kisiwa kidogo chenye watu laki tano tuu Cape Verde kimefanikiwa kuingia kwenye fainali za Kombe la Afrika (Africa Cup of Nations) baada ya kucharagaza Cameron na akina Eto'o. Cameroon wametupwa nje baada ya kufungwa jumla ya mabao 3-2 na haka kanchi. Cape Verde watacheza kwenye fainali mwakani South africa. Tanzania tuko wapi? Kanchi kama kama haka kanatinga finaili tena kwa kuichapa Cameroon, sie bado......
EMT

Umenifanya nicheke kidogo.

Hivi kuna vinchi vidogo duniani? Ina watu laki tano tu?

Hivi Cape Verde inaishi chini ya kivuli cha nchi ipi? Cape Verde inajitegemea? Je ni maskini kama Tanzania?

Nje ya mada kidogo...kuna mijadala hapa JF inasema Zanzibar haiwezi kuwa nchi.
Pili, Wapo wanaosema Zanzibar itaishi chini ya kivuli cha Tanganyika siku zote.

Je tumewazibia njia Zanzibar kuwa Cape Verde ya Tanzania?

Utaelewa kwa nini mada yako imenifanya nicheke kidogo.Jenerali Ulimwengu alishasema kuwa sisi Tanzania tumeamua kufanya "upuuzi" katika kila kitu. Baya zaidi ni kuwa hata huo upuuzi hatuupangilii. Hata kama tutafurahi kuwa mabingwa katika kufanya upuuzi basi hatutachukua nafasi ya kwanza kwani Congo/ Zaire ambayo inaongoza kwa upuuzi, yenyewe imepangilia upuuzi wake.

Link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...imwengu-hata-kwenye-upuuzi-tuko-dhaifu-3.html
 
EMT

Umenifanya nicheke kidogo.

Hivi kuna vinchi vidogo duniani? Ina watu laki tano tu?

Hivi Cape Verde inaishi chini ya kivuli cha nchi ipi? Cape Verde inajitegemea? Je ni maskini kama Tanzania?

Nje ya mada kidogo...kuna mijadala hapa JF inasema Zanzibar haiwezi kuwa nchi.
Pili, Wapo wanaosema Zanzibar itaishi chini ya kivuli cha Tanganyika siku zote.

Je tumewazibia njia Zanzibar kuwa Cape Verde ya Tanzania?

Utaelewa kwa nini mada yako imenifanya nicheke kidogo.Jenerali Ulimwengu alishasema kuwa sisi Tanzania tumeamua kufanya "upuuzi" katika kila kitu. Baya zaidi ni kuwa hata huo upuuzi hatuupangilii. Hata kama tutafurahi kuwa mabingwa katika kufanya upuuzi basi hatutachukua nafasi ya kwanza kwani Congo/ Zaire ambayo inaongoza kwa upuuzi, yenyewe imepangilia upuuzi wake.

Link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...imwengu-hata-kwenye-upuuzi-tuko-dhaifu-3.html

Yea, there are small countries in the world, but with big hearts and lots of spirit which have made them where they are.
 
Tatizo letu hatu'practise soka la halisia,utakuta team licha ya kufanya bonge la usajili wa bei mbaya na kumleta Kocha Mzungu wa bei mbaya vilevile bado inahangaika kutumia njia mbadala za kupata ushindi wa uwanjani,zinatenga mafungu ya waamuzi na watu wengine wenye infulence ya kutengeneza matokeo ya uwanjani waziwazi hadi wachezaji wao wanajua,wachezaji wanakuwa wanafahamu kabisa kama tukicheza na team fulani tutacheza na mipango itakayotusaidia tupate ushindi hata iweje,kama ni watu watatolewa kwa card nyekundu au penalt zitamwagwa,sasa mchezaji kama huyu unapokwenda kumpambanisha na nchi nyingine zisizotumia style hii unategemea nini?
Mi nimeshangazwa sana juzi kwenye ile mechi ya kugombe ticket ya kwenda AFCON kati ya Uganda na Zambia,kwenye 1st eleven line up ya Uganda kulikuwa na wachezaji fulani wasio na majina na wala wasiochezea team zenye majina mfano Baba Kizito, the 19 years old boy alicheza vizuri sana,fikiria wakati sisi hapa Bongo kuna watu wanamwona Okwi kama MUNGU mtu au Kiiza kama ni the all time best striker kule Uganda MUNGU mtu huyu na mwenzake wanawekwa benchi na watu kama kina Baba Kizito,hii ni dalili kuwa Tanzania bado ina safari ndefu sana kwenye soka.
 
Sisi ni mabingwa wa porojo imagine laki 5 vs milioni 40 nilitarajia kupata wachezaji wengi na wazuri out of 40mil.
Not seriously invested in Sports tumekalia usimba na uyanga team zina nusu karne almost hata viwanja hawana
 
Mkuu EMT mie nilivyoona Taifa la Cameroun linahaha katika kuhakikisha linampata Eto'o ili aweze kucheza katika mchezo huo na kumtumia ujumbe mzito kule Russia ili akubali kucheza katika mechi ile nikabaki nashangaa. Nikasema hawa Cameroon wameishiwa kiasi hicho hata kuogopa timu ambayo haina history yotote katkka soka la Afrika ukilinganisha na nchi kama Ghana, Nigeria, Egypt, Algeria etc? Sasa naelewa baada ya kuona matokeo ya mchezo huo. Taifa dogo linalokadiriwa kuwa na population ya watu 500,000 linafanya vizuri kuliko Taifa lenye watu 45 million!!!! Kweli Bongo ni kichwa cha mwendawazimu!!!! Kila kitu ni hovyo hovyo tu hakuna hata kimoja ambacho unaweza kusema hiki tuna ahueni!!!! Hata enzi za wakongwe akina Kibadeni, Dilunga, Chogo Chemba n.k. tulikuwa tunavuma katika bara la Afrika...siku hizi hilo soka la Bongo hata kulisikia sitaki!!! Badala ya kuendeleza vipaji vya Watanzania nao wamejiingiza katika kusajili wacheza toka nchi za nje!!!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT

Similar Discussions

Back
Top Bottom