BVR Moja, WapigaKura 1,300 ndani ya Siku 7 tu.

BVR Moja, WapigaKura 1,300 ndani ya Siku 7 tu.

UKAWA UKAWA

Member
Joined
Sep 24, 2014
Posts
53
Reaction score
15
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI KATIKA HILI MMEKOSEA SANA YANAHITAJIKA MAREKEBISHO MAPEMA


Wakuu,
naamini sote humu ndani tunakumbuka kuwa TUME ya Taifa ya Uchaguzi itaanza Zoezi la KUANDIKISHA Wapigakura kesho Jumanne Tarehe 16/06/2015 kuanzia Saa 2:00 asubuhi kwa Mikoa ya Manyara, Kilimanjaro, Mara na Arusha, baada ya kuliahirisha kwa wiki moja inayomalizika leo.

WILAYA YA SERENGETI

Huku Serengeti Mara,
CCM kupitia kwa Watendaji wabovu waliomo Serikalini, tayari wameanza hujuma katika baadhi ya maeneo kwa lengo la kuminya haki ya Wananchi kuandikishwa.

Mfano;
Kijiji cha Nyansurura
ambako ni Makao Makuu ya Kata ya Nyansurura ndani ya Wilaya ya Serengeti, TUME YA UCHAGUZI kupitia kwa Watendaji wake wabovu, wamekwepa kuweka Kituo cha Kuandikisha Wapigakura, licha ya Eneo hilo kuwa na Taasisi za Umma zaidi ya tatu ambazo ni Shule ya Msingi Nyansurura, Shule ya Sekondari Nyansurura, Zahanati ya Kijiji cha Nyansurura, Kituo cha Polisi Mto Mara na Ofisi ya Kijiji cha Nyansurura.

Matokeo yake wametoa Kituo kimoja pekee katika Kijiji kizima chenye Wapigakura zaidi ya 1,300 na wamekipanga katika Eneo ambalo ni pembezoni mwa Kijiji liitwalo Matanka ambako ni mbali karibu Kilomita tano (5Km) kutoka kwa Wakazi wa Vitongoji vingine.

Licha ya Wananchi kulalamikia sana suala hili kwa Watendaji wa TUME waliofika Kijijini kukagua Vituo ndani ya Kata ya Nyansurura, lakini hadi sasa hakuna dalili zozote za Tume kurejesha Kituo katika Eneo hili kwa kigezo kwamba, Wakazi wanaoishi huku wengi wao hawaiungi mkono CCM, hivyo wakipewa Kituo, watajiandikisha wengi waiangushe vibaya kwenye Uchaguzi Mkuu ujao wa mwezi Oktoba 2015.

Kwa msisitizo,
tunaishauri TUME ya Taifa ya Uchaguzi chini Mwenyekiti wake Mzee Damian Lubuva, ione umuhimu wa kuweka Kituo kwenye Eneo hili liitwalo Nyansurura (Centre) kutokana na uhalisia wa Jiografia ya Eneo hili, umbali wa Eneo kilipowekwa Kituo cha kwanza yaani Matanka na wingi wa Idadi ya Wapigakura wanaotarajiwa kuandikishwa katika Kijiji hiki.

Mwenyekiti Serikali ya Kijiji,
Kijiji cha Nyansurura,
S. L. P 81,
Mugumu, Serengeti.
Francis Muhingira Garatwa

0785881009/0767881009
Ahsanteni sana!
 
Ccm kwa mbinu zao hizo tumezoa kila sehemu cha msingi ni nyie viongozi muangalie namna ya kusaidiana na wananchi ikiwemo kupeleka haya mambo kwa viongozi wakuu ili litatulike haraka mkilemaa inakula kwa wananchi
 
Pole mwenyekiti.
Nakushauri uendelee kupigania hatua hiyo.
Tafuta wenzio wenye influence muongozane kwa Mkurugenzi wa halmashauri.
Bila shaka mtafanikiwa kutetea haki za watu wenu.
 
Ase mkuu kama raia wapo mtu mwenye speed ao wote anafuta.
Wachace sana
 
BVR moja wastani inaandika watu 150 kutwa
Kwa hiyo 150 x 7= 1,050

watu 250 watakosa kuanidikishwa
 
Mtumishi wa Mungu-Mwal. J.K Nyerere utuombee.
 
Mbinu za ccm kutaka kulazimisha ushindi kutasababisha wananchi wengi sana wakose haki yako ya kupiga kura.. Leo wananchi wanatoa rushwa ili waipate haki yao ya kikatiba ya kuandikishwa kwenye mashine zao za kuokoteza..!
 
Mbinu za ccm kutaka kulazimisha ushindi kutasababisha wananchi wengi sana wakose haki yako ya kupiga kura.. Leo wananchi wanatoa rushwa ili waipate haki yao ya kikatiba ya kuandikishwa kwenye mashine zao za kuokoteza..!

Hii huyu Mkude Simba analijua?Au ndiyo lile sikio la kufa..Nina uhakika come October waliojindikisha kupiga kura watakuwa chini ya milioni 8
 
Back
Top Bottom