Busara za Nyerere zisisahaulike

Busara za Nyerere zisisahaulike

mavumbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2013
Posts
596
Reaction score
328
Mara mbili katika matukio muhimu nchini, Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa ushauri ambao huenda tumeanza kuusahau.

Moja ni pale alipowashauri wa Tz kuukubali mfumo wa vyama vingi vya kisiasa - alisema, pamoja na kwamba waliokataa ni wengi, lakini hawa wachache wana umuhimu wake la sivyo tutabweteka na kusinzia tukidhani kwa vile tunapendwa tukaona yote tunayofanya ni sahihi hata pale penye uzembe mkubwa.

Pili aliposhauri kuhusu hatari ya ubaguzi wakati wa mvutano kuhusu muungano alisema, tukikubali kubaguana, hatutaishia hapa, tutaendelea kutafuta nani tumbague hadi tutafikia kujibagua wenyewe!

Leo najiuliza: tumefikia mahali tunaona hakuna umuhimu tena wa mawazo ya wachache hadi tunaingiza mambo ya kuwalazimisha kuondoka?

Pili, kwa huu ubaguzi wa wazi tukishawaondoa hawa kitakachofuata nini?

Ni heri kuwa na mbuzi wa kafara ambaye ukimtoa gharama yake ni ndogo, kuliko kufikia kumtoa ng'ombe mzima kafara, ati kwa vile tulikataa kuwa na subira na uvumilivu.

Mark my words ubaguzi unatoka mtaani kwetu sasa unaingia nyumbani mwetu
Na wala si kesho kutwa...ni kesho!
 
Mara mbili katika matukio muhimu nchini, Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa ushauri ambao huenda tumeanza kuusahau.

Moja ni pale alipowashauri wa Tz kuukubali mfumo wa vyama vingi vya kisiasa - alisema, pamoja na kwamba waliokataa ni wengi, lakini hawa wachache wana umuhimu wake la sivyo tutabweteka na kusinzia tukidhani kwa vile tunapendwa tukaona yote tunayofanya ni sahihi hata pale penye uzembe mkubwa.

Pili aliposhauri kuhusu hatari ya ubaguzi wakati wa mvutano kuhusu muungano alisema, tukikubali kubaguana, hatutaishia hapa, tutaendelea kutafuta nani tumbague hadi tutafikia kujibagua wenyewe!

Leo najiuliza: tumefikia mahali tunaona hakuna umuhimu tena wa mawazo ya wachache hadi tunaingiza mambo ya kuwalazimisha kuondoka?

Pili, kwa huu ubaguzi wa wazi tukishawaondoa hawa kitakachofuata nini?

Ni heri kuwa na mbuzi wa kafara ambaye ukimtoa gharama yake ni ndogo, kuliko kufikia kumtoa ng'ombe mzima kafara, ati kwa vile tulikataa kuwa na subira na uvumilivu.

Mark my words ubaguzi unatoka mtaani kwetu sasa unaingia nyumbani mwetu
Na wala si kesho kutwa...ni kesho!
Huna akili wewe pimbi. Wananchi wameamaua kwa ballot box unataka nini? Mpaka uone Zitto au Mbowe ni wabunge ndio ufurahi?
 
Nyie Arsenal kampiga Man U hukoo. Yaani ukichanganya na Simba kushinda jana., nasikia rahaaa
 
Nyerere alikubali vyama vingi kwa kuona mbali Sana maana aliona Ni bora kudeal na wapinzani jukwaani kuliko kuzuia upinzani halafu uzalishe magaidi watakaoingia msituni.
Hivyo unapoua upinzani wa majukwaani tegemea kujitokeza vikundi vitakavyokupinga vikiwa msituni hapa utatumia nguvu kubwa kuviondoa.​
 
Haya watakaolewa ni watanzania wengi sana wapumbavu wachache hawataelewa.Hv kama Mwl.Nyerere anayeheshimika kama mwanafalsafa nguli Africa na ulimwenguni aliweza kuona mbali kiasi hicho kwa kipindi kile sasa imagine Leo mtu haoni sasa unadhani kuna akili hapo lzm uwe na wasiwasi na akili za watu.Yaani wachache sana naamini kabisa hawataelewa ila wengi wanajua hatari ijayo wapumbavu wachache hawataelewa kabisa ambao baba wa Taifa alisema ukiwalazimisha kuelewa utawauwa tu.
 
Kwenye mfumo ya chama kimoja namna pekee ya kuiangusha serikali ni coup d'etat. Tutakipata tunachokitafuta. Mwalimu mwenyewe alikua shahidi, alinusurika karibu mara tatu.
 
Back
Top Bottom