BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,859
Msanii Nyota kutoka Nigeria, Burna Boy ameonesha hisia zake baada ya kifo cha msanii AKA ambaye aliuawa kwa kupigwa Risasi siku ya Birthday yake February 10, 2023 jiji Durban wakati akitoka mgahawani na rafiki zake.
Ikumbukwe Burna na AKA walikuwa na tofauti za kimuziki baada ya kupishana kauli kupitia Twitter ambapo Burna alijiapiza kumchapa AKA siku wakikutana.
Beef hiyo ilidumu hadi Januari 2023 ambapo AKA alisema yeye hana tatizo na Burna na Mungu aendelee kumbariki.
AKA anatarajiwa kuzikwa Jumamosi Februari 18, 2023.