Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,372
Habari wakuu,
Hivi kweli kuna bajeti ya wizara yoyote hapa nchini inayostahili kuungwa mkono kwa asilimia mia moja?
Binafsi huwa nashangwaza sana na wabunge wanaosimama na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja wakati bajeti hizo zimejaa mapungufu mengi ikiwa ni pamoja na kutengewa fedha kidogo na ahadi ambazo hazikutekelezwa katika bajeti zilizopita.
Kwa mfano, bajeti ya wizara ya kilimo ilikuwa na mapungufu mengi ikiwa ni pamoja na kutotekeleza ahadi za upelekaji wa chakula cha njaa katika maeneo mbali mbali nchini,matatizo ya pembejeo,bei zisizoridhisha kwa mazao ya kilimo na madudu mengine mengi tu.Pia tukumbuke bajeti ya wizara ya kilimo inayopigiwa chapuo na serikali imetengewa asilimia kumi tu ya bajeti nzima ya serikali!
Hata hivyo,utashanga kusikia baadhi ya wabunge wakisimama na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja!Mimi nasema wabunge wa aina hii ni wasaliti,wabinafsi na ni wanafiki wakubwa na wasiopaswa kuchaguliwa tena!Ukiwachunguza kwa makini utagungua kuwa wengi wao wanajipendekeza tu kwa serikali kwa nia ya kupata ama uwaziri au kupata nafasi zingine za uteuzi!
Ukweli ni kwamba,hata kama kuna utekelezaji umefanywa na serikali katika bajeti husika, hakuna jimbo ambalo limetekelezewa kila kitu kwa asilimia mia moja na hivyo kumfanya mbunge husika kustahili kusimama na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Hivi kweli inaiingia akilini kumsika mbunge mwenzako analalamika kuwa jimboni kwake watu wanakufaa njaa kutokana na serikali kutotekeleza ahadi zake za kupeleka chakula alafu mbunge anaefuata anasimama na kusema naunga hoja mkono asilimia mia moja!Hivi kwanini usimsaidie mbunge mwenzako kuibana serikali itekeleze ahadi zake badala ya kujipendekeza?Hivi kweli sisi ni taifa moja au ni unafiki tu wa kauli za wabunge ndani ya bunge?
Wabunge wanaounga hoja mkono kwa asilimia mia moja hawawakilishi wanaanchi wao bali ni wasaliti na dawa yao ni kuwapiga chini 2015.Hatupingi serikali kupongezwa ila sio kwa asilimia hiyo mia moja wakati watu wanakufa njaa na hakuna pembejeo na mambo mengine mengi tu.
Wabunge timizeni wajibu wenu na muache kuleta siasa katika maisha ya watu.
Hivi kweli kuna bajeti ya wizara yoyote hapa nchini inayostahili kuungwa mkono kwa asilimia mia moja?
Binafsi huwa nashangwaza sana na wabunge wanaosimama na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja wakati bajeti hizo zimejaa mapungufu mengi ikiwa ni pamoja na kutengewa fedha kidogo na ahadi ambazo hazikutekelezwa katika bajeti zilizopita.
Kwa mfano, bajeti ya wizara ya kilimo ilikuwa na mapungufu mengi ikiwa ni pamoja na kutotekeleza ahadi za upelekaji wa chakula cha njaa katika maeneo mbali mbali nchini,matatizo ya pembejeo,bei zisizoridhisha kwa mazao ya kilimo na madudu mengine mengi tu.Pia tukumbuke bajeti ya wizara ya kilimo inayopigiwa chapuo na serikali imetengewa asilimia kumi tu ya bajeti nzima ya serikali!
Hata hivyo,utashanga kusikia baadhi ya wabunge wakisimama na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja!Mimi nasema wabunge wa aina hii ni wasaliti,wabinafsi na ni wanafiki wakubwa na wasiopaswa kuchaguliwa tena!Ukiwachunguza kwa makini utagungua kuwa wengi wao wanajipendekeza tu kwa serikali kwa nia ya kupata ama uwaziri au kupata nafasi zingine za uteuzi!
Ukweli ni kwamba,hata kama kuna utekelezaji umefanywa na serikali katika bajeti husika, hakuna jimbo ambalo limetekelezewa kila kitu kwa asilimia mia moja na hivyo kumfanya mbunge husika kustahili kusimama na kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Hivi kweli inaiingia akilini kumsika mbunge mwenzako analalamika kuwa jimboni kwake watu wanakufaa njaa kutokana na serikali kutotekeleza ahadi zake za kupeleka chakula alafu mbunge anaefuata anasimama na kusema naunga hoja mkono asilimia mia moja!Hivi kwanini usimsaidie mbunge mwenzako kuibana serikali itekeleze ahadi zake badala ya kujipendekeza?Hivi kweli sisi ni taifa moja au ni unafiki tu wa kauli za wabunge ndani ya bunge?
Wabunge wanaounga hoja mkono kwa asilimia mia moja hawawakilishi wanaanchi wao bali ni wasaliti na dawa yao ni kuwapiga chini 2015.Hatupingi serikali kupongezwa ila sio kwa asilimia hiyo mia moja wakati watu wanakufa njaa na hakuna pembejeo na mambo mengine mengi tu.
Wabunge timizeni wajibu wenu na muache kuleta siasa katika maisha ya watu.