Jana kwa mara ya kwanza waandishi wa habari walizuiwa kurekodi shughuli za vikao vya Bunge. Hawakuwa na sababu ya kuwepo bungeni. Nikiwaza kwa sauti na kiujinga ujinga tu nashindwa kuelewa.
1. Pamoja na uozo na ubovu na umizigo wa watendaji wa serikali ya JM Kikwete lakini hatukuona hata mara moja rais mcheshi JK akiwaficha watendaji wake nyuma ya pazia.
Serikali ya JPM na wateule wake wamejinabaisha mbele ya ulimwengu kwamba wako makini na wenye kuichukia rushwa na ufisadi. Tangu mapambano ya dhidi ya ufisadi yaanze hapa nchini, huchokonolewa kwanza bungeni. Sasa, hawa wa utawala huu wanachokificha au wanachotaka kukificha ni nini? Kwa nini wanataka mambo yao yatendeke nyuma ya pazia?
2. Imejulishwa kuwa serikali ya JK haikuwa na makusanyo makubwa ya mapato kama hii ya JPM. Pamoja na umasikini wa serikali ya JK haikuinyima fedha TBC. Alitaka muhimili mwingine wa utawala uonwe na uonekane.
Sasa vipi, serikali ya JPM yenye kukusanya mara dufu mapato kuliko ile ya JK ishindwe kuipatia fedha TBC ioneshe moja kwa moja shughuli za vikao vya muhimili huu- Bunge?
Haya, serikali haina fedha. Wapo wenye fedha, Azam TV, StarTV nk basi waruhusuni hao waoneshe! Hamtaki! Kumbe mnachotaka kuficha nini?
3. Imedaiwa kuwa mara kadha serikali imetumia mabavu na mbinu kadha kuudhibiti muhimili huu (Bunge). Pamoja na hayo, JK hakufika pahala akalizima bunge. Imekuwaje awamu hii mnataka kulizima bunge? Nini mnatafuta? Je! Mnataka serikali tu mwonekane, bunge je?
Kwa mwendo huu, wa kukosa kuliona bunge live hakika Kikwete tutakukumbuka. Serikali yako ilikuwa wazi. Ililiacha bunge liiumbue serikali yako iliyojaa mawaziri mizigo.
Ati serikali hii haina mawaziri mizigo ILA haitaki kuumbuliwa hadharani!
HEKO zako Kikwete kukubali kukosolewa na kuikosoa serikali yako hadharani. Hakika katika hili la Uhuru wa Vyombo vya Habari ulijitahidi kuwa muungwana; japo mwishoni ulijikwaa kuja na sharia ya mitandaoni.
UTAKUMBUKWA JK!
1. Pamoja na uozo na ubovu na umizigo wa watendaji wa serikali ya JM Kikwete lakini hatukuona hata mara moja rais mcheshi JK akiwaficha watendaji wake nyuma ya pazia.
Serikali ya JPM na wateule wake wamejinabaisha mbele ya ulimwengu kwamba wako makini na wenye kuichukia rushwa na ufisadi. Tangu mapambano ya dhidi ya ufisadi yaanze hapa nchini, huchokonolewa kwanza bungeni. Sasa, hawa wa utawala huu wanachokificha au wanachotaka kukificha ni nini? Kwa nini wanataka mambo yao yatendeke nyuma ya pazia?
2. Imejulishwa kuwa serikali ya JK haikuwa na makusanyo makubwa ya mapato kama hii ya JPM. Pamoja na umasikini wa serikali ya JK haikuinyima fedha TBC. Alitaka muhimili mwingine wa utawala uonwe na uonekane.
Sasa vipi, serikali ya JPM yenye kukusanya mara dufu mapato kuliko ile ya JK ishindwe kuipatia fedha TBC ioneshe moja kwa moja shughuli za vikao vya muhimili huu- Bunge?
Haya, serikali haina fedha. Wapo wenye fedha, Azam TV, StarTV nk basi waruhusuni hao waoneshe! Hamtaki! Kumbe mnachotaka kuficha nini?
3. Imedaiwa kuwa mara kadha serikali imetumia mabavu na mbinu kadha kuudhibiti muhimili huu (Bunge). Pamoja na hayo, JK hakufika pahala akalizima bunge. Imekuwaje awamu hii mnataka kulizima bunge? Nini mnatafuta? Je! Mnataka serikali tu mwonekane, bunge je?
Kwa mwendo huu, wa kukosa kuliona bunge live hakika Kikwete tutakukumbuka. Serikali yako ilikuwa wazi. Ililiacha bunge liiumbue serikali yako iliyojaa mawaziri mizigo.
Ati serikali hii haina mawaziri mizigo ILA haitaki kuumbuliwa hadharani!
HEKO zako Kikwete kukubali kukosolewa na kuikosoa serikali yako hadharani. Hakika katika hili la Uhuru wa Vyombo vya Habari ulijitahidi kuwa muungwana; japo mwishoni ulijikwaa kuja na sharia ya mitandaoni.
UTAKUMBUKWA JK!