Bundi wawa lulu Afrika Kusini

Bundi wawa lulu Afrika Kusini

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Kufuatia tatizo la panya wanaoshambulia watoto katika Jimbo la Johanesburg,ndege aina ya bundi wanatumika kuwaangamiza panya hao. Serikali ya Jimbo hilo inawatumia bundi ambao hula sana panya wakati wa usiku.

Tayari kuna mafanikio katika kuwadhibiti panya hao kwa kutumia bundi. Kimsingi,bundi wamekuwa lulu Jimboni humo.

Chanzo: BBC
 
....

....
50932204.jpg
 
Bundi hapa kwetu tunampiga vita.Wenzetu wanamtumia

Mzee Tupatupa
 
Hao ndege ni wazuri sana ktk kudhibiti panya.Niliwahi kufanya kazi stores kulikuwa na godowns tumehifadhi mbegu mbalimbali na panya walikuwa wanakula sana mbegu.Ilikuwa ni kampuni ya wazungu wakawa wanafuga bundi kwa ajili ya kudhibiti panya na kwa kweli ilifanikiwa sana hiyo plan. Hua wanauwa panya kwa kuwakata vichwa na kula kisha viwiliwili hawana mpango navyo.
 
Kufuatia tatizo la panya wanaoshambulia watoto katika Jimbo la Johanesburg,ndege aina ya bundi wanatumika kuwaangamiza panya hao. Serikali ya Jimbo hilo inawatumia bundi ambao hula sana panya wakati wa usiku.

Tayari kuna mafanikio katika kuwadhibiti panya hao kwa kutumia bundi. Kimsingi,bundi wamekuwa lulu Jimboni humo.

Chanzo: BBC

Bundi hapa kwetu tunampiga vita.Wenzetu wanamtumia

Mzee Tupatupa

Hao ndege ni wazuri sana ktk kudhibiti panya.Niliwahi kufanya kazi stores kulikuwa na godowns tumehifadhi mbegu mbalimbali na panya walikuwa wanakula sana mbegu.Ilikuwa ni kampuni ya wazungu wakawa wanafuga bundi kwa ajili ya kudhibiti panya na kwa kweli ilifanikiwa sana hiyo plan. Hua wanauwa panya kwa kuwakata vichwa na kula kisha viwiliwili hawana mpango navyo.
Mnanishangaza! Yaani bundi wana uwezo wa kudhibiti panya zaidi kuliko paka?
 
Kufuatia tatizo la panya wanaoshambulia watoto katika Jimbo la Johanesburg,ndege aina ya bundi wanatumika kuwaangamiza panya hao. Serikali ya Jimbo hilo inawatumia bundi ambao hula sana panya wakati wa usiku.

Tayari kuna mafanikio katika kuwadhibiti panya hao kwa kutumia bundi. Kimsingi,bundi wamekuwa lulu Jimboni humo.

Chanzo: BBC

Jimbo la Johannesburg? Ulimaanisha Gauteng?
 
Hebu tuelimishaneni kwa mashiko , tabia za Bundi si kama za Njiwa/Kuku/Khanga etc (domestic animals)
Bundi unamdhibitije ili akufanyie uyatakayo? Kwa mfano huu ina maana hata Kunguru basi anafugika?
 
Ila sishangai sana Bundi kuwa Elizabeth Michael huko Sauzi maana hata sie hapa Mtwara hao panya washakuwa pia Lulu kuwapata ni nadra sana hadi natamani na mie ningekuwa ninaishi huko dar
 
Mkuu, hao ndege kwa kudhibiti panya ni wazuri sana.Hiyo kama nilivoeleza hapo juu niliishuhudia mwenyewe kwani nilikuwa stores.
 
Mnanishangaza! Yaani bundi wana uwezo wa kudhibiti panya zaidi kuliko paka?

Bora hii mkuu., mi nlikutana na hyo ya nyani kula vifaranga vya kuku,humu humu Jf...yaan imeniacha njia panda hadi Leo.
 
Back
Top Bottom