Bundi atua tena UVCCM

Bundi atua tena UVCCM

mwekundu

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2013
Posts
22,477
Reaction score
21,023
Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) linakutana leo jini Dodoma huku hatma ya Mwenyekiti wa umoja huo, Sadifa Hamisi Juma ikiwa mashakani. Mkutano huo wa baraza ulitanguliwa na kikao cha Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM kilichokaa jana jioni mjini Dodoma kwenye Ukumbi wa White House ambako ni makao makuu ya CCM.

Sadifa, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Donge, analalamikiwa kutokana na matatizo mbalimbali ya kiutawala, matumizi mabaya ya fedha na usimamizi mbovu wa mali za chama hicho.

Alipoulizwa juu ya kuwapo kwa vuguvugu la kumng'oa, Sadifa alijibu kwa kifupi tu; "Asante Nashukuru." "Ninaambiwa nimekuwa mtu wa kutukana watu, nimemtukana nani? Asante Nashukuru.,"aliongeza Sadifa hata pale mwandishi alipomuuliza kwa zaidi ya mara tatu aliishia kutoa jibu: "Asante nashukuru."

Naye Katibu Mkuu wa UVCCM, Sixtus Mapunda, alipoulizwa na Mwananchi jana, alisema kuwa hana taarifa za kuwapo mpango wa kumng'oa mwenyekiti wake kama inavyoelezwa.

"Sikiliza, mimi ndiye Mtendaji Mkuu wa UVCCM, ajenda za mkutano, sisi kama sekretarieti tumeshaziandaa na hakuna agenda kama hiyo. Umoja huu unaendeshwa kwa kanuni na taratibu,"alisema Mapunda.

Mapunda aliyechukua mikoba hiyo Agosti mwaka huu, alipoulizwa kuhusu mkutano huo kugharamiwa na CCM makao makuu badala ya Jumuiya yenyewe, alikanusha taarifa zilizozagaa akisema: "Mimi ndiye niliyeitisha mkutano huu, sasa chama kinatoka wapi?"

Mjumbe aanika madudu ya UVCCM

Mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Ruvuma, Alex Nchimbi alifafanua hakuna njama za kumtoa ila mambo anayotakiwa kurekebisha ndio yanaweza kumtoa.

Nchimbi alisema kuwa UVCCM inakabiliwa na tatizo la matumizi mabaya ya fedha na kibaya zaidi hesabu za chama hicho hazijakaguliwa kwa muda mrefu.

Alisema jumuiiya hiyo hupata kiasi cha Sh80 milioni kutokana na miradi mbalimbali kama jengo lililoko makao makuu ya UVCCM, lakini fedha hizo zinafujwa.

"Ila utashangaa kaka yaani zile fedha zinavyofujwa. Hadi kwa mwezi jumuiya inabakiwa na Sh8 milioni au wakati mwingine hadi Sh6milioni," aliongeza Nchimbi.

source; Bundi atua tena UVCCM - Siasa - mwananchi.co.tz
 
Mjumbe aanika madudu ya UVCCM

Mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Ruvuma, Alex Nchimbi alifafanua hakuna njama za kumtoa ila mambo anayotakiwa kurekebisha ndio yanaweza kumtoa.

Nchimbi alisema kuwa UVCCM inakabiliwa na tatizo la matumizi mabaya ya fedha na kibaya zaidi hesabu za chama hicho hazijakaguliwa kwa muda mrefu.

Alisema jumuiiya hiyo hupata kiasi cha Sh80 milioni kutokana na miradi mbalimbali kama jengo lililoko makao makuu ya UVCCM, lakini fedha hizo zinafujwa.

“Ila utashangaa kaka yaani zile fedha zinavyofujwa. Hadi kwa mwezi jumuiya inabakiwa na Sh8 milioni au wakati mwingine hadi Sh6milioni,” aliongeza Nchimbi.


source; Bundi atua tena UVCCM - Siasa - mwananchi.co.tz

...huyu Nchimbi angekuwa Bavicha angekuwa sasa anaandaliwa zengwe la kufukuzwa uanachama, nashangaa kwanini CCM ina demokrasia kuliko Chadema?...
 
Wana hangaika kuiua CHADEMA huku nyumba zao zinazidi kuteketea kwa moto.
 
...huyu Nchimbi angekuwa Bavicha angekuwa sasa anaandaliwa zengwe la kufukuzwa uanachama, nashangaa kwanini CCM ina demokrasia kuliko Chadema?...

CCM mpaka mchwa wana demokrasia ili waendelee kutafuna mali za wtz pasipo kubugudhiwa.
 
ngoja tusubiri maamuzi yao, baada ya kikao, maana hii jumuiya siku hizi haina nguvu kabisa, imekuwa ni sehemu ya kutengeneza mitandao badala ya chama, hususani kuhamasisha vijana.
 
Habari kutoka Dodoma sasa hivi zinasema kuna makundi mbalimbali ya wajumbe wa baraza kuu toka Jana usiku na asubuhi ya Leo wamekua wakijadili namna ya kumtoa mwenyekiti wa umoja wa vijana wa ccm Bwana sadifa, japo kuna habari pia wajumbe wa umoja huo toka Zanzibar hawakubaliani na mpango huo kwani wanaufananisha na ule uliomtoa masauni ambaye nae alitolewa kipindi kilichopita kwa tatizo la umri wake kuwa mkubwa tofauti na kanuni za umoja huo.

Matatizo ya sadifa ni yafuatayo:
1.kuchagua baadhi ya wakuu wa idara bila kushirikisha kamati ya utekelezaji
2.kuropoka ropoka hovyo
3. Kutaka yeye tuu kuwa muongeaji ndani ya vikao vya umoja huo na kuongea pumba kwenye vikao vya juu haswaa Kamati kuu ya ccm
4.akili zake inasemeka Kama chizi flani hivi(fyatu).. Maana ata uvaaji wake ni kituko.
 
Hawakuyajua yote hayo?????!!!!!!

Personality ya mtu mnayempa uongozi haikujulikana????!!

Hivi hili ndio tanuri la viongozi???!!!

Nalazimika kuanza kujiuliza umuhimu na umakini wa taasisi hii
 
...huyu Nchimbi angekuwa Bavicha angekuwa sasa anaandaliwa zengwe la kufukuzwa uanachama, nashangaa kwanini CCM ina demokrasia kuliko Chadema?...
Kumbuka chadema ni saccos
 
ukiona ngumi uvccm , basi ujue kuna posho inagombewa ! Yaani wako kama vitoto vya mbwa vile , vikiona mfupa tu ni ugomvi !
 
Habari kutoka Dodoma sasa hivi zinasema kuna makundi mbalimbali ya wajumbe wa baraza kuu toka Jana usiku na asubuhi ya Leo wamekua wakijadili namna ya kumtoa mwenyekiti wa umoja wa vijana wa ccm Bwana sadifa, japo kuna habari pia wajumbe wa umoja huo toka Zanzibar hawakubaliani na mpango huo kwani wanaufananisha na ule uliomtoa masauni ambaye nae alitolewa kipindi kilichopita kwa tatizo la umri wake kuwa mkubwa tofauti na kanuni za umoja huo.

Matatizo ya sadifa ni yafuatayo:
1.kuchagua baadhi ya wakuu wa idara bila kushirikisha kamati ya utekelezaji
2.kuropoka ropoka hovyo
3. Kutaka yeye tuu kuwa muongeaji ndani ya vikao vya umoja huo na kuongea pumba kwenye vikao vya juu haswaa Kamati kuu ya ccm
4.akili zake inasemeka Kama chizi flani hivi(fyatu).. Maana ata uvaaji wake ni kituko.

5. U.sho.ga
 
Sijaona 'bundi aliyetua tena UVCCM'. Ni bundi yule yule (ukipenda wale wale) ambao wameweka makao kwenye huu mti (UVCCM) kwa muda mrefu tangu uchaguzi wa viongozi uliopita.

Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) linakutana leo jini Dodoma huku hatma ya Mwenyekiti wa umoja huo, Sadifa Hamisi Juma ikiwa mashakani. Mkutano huo wa baraza ulitanguliwa na kikao cha Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM kilichokaa jana jioni mjini Dodoma kwenye Ukumbi wa White House ambako ni makao makuu ya CCM.

Sadifa, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Donge, analalamikiwa kutokana na matatizo mbalimbali ya kiutawala, matumizi mabaya ya fedha na usimamizi mbovu wa mali za chama hicho.

Alipoulizwa juu ya kuwapo kwa vuguvugu la kumng'oa, Sadifa alijibu kwa kifupi tu; "Asante Nashukuru." "Ninaambiwa nimekuwa mtu wa kutukana watu, nimemtukana nani? Asante Nashukuru.,"aliongeza Sadifa hata pale mwandishi alipomuuliza kwa zaidi ya mara tatu aliishia kutoa jibu: "Asante nashukuru."

Naye Katibu Mkuu wa UVCCM, Sixtus Mapunda, alipoulizwa na Mwananchi jana, alisema kuwa hana taarifa za kuwapo mpango wa kumng'oa mwenyekiti wake kama inavyoelezwa.

"Sikiliza, mimi ndiye Mtendaji Mkuu wa UVCCM, ajenda za mkutano, sisi kama sekretarieti tumeshaziandaa na hakuna agenda kama hiyo. Umoja huu unaendeshwa kwa kanuni na taratibu,"alisema Mapunda.

Mapunda aliyechukua mikoba hiyo Agosti mwaka huu, alipoulizwa kuhusu mkutano huo kugharamiwa na CCM makao makuu badala ya Jumuiya yenyewe, alikanusha taarifa zilizozagaa akisema: "Mimi ndiye niliyeitisha mkutano huu, sasa chama kinatoka wapi?"

Mjumbe aanika madudu ya UVCCM

Mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Ruvuma, Alex Nchimbi alifafanua hakuna njama za kumtoa ila mambo anayotakiwa kurekebisha ndio yanaweza kumtoa.

Nchimbi alisema kuwa UVCCM inakabiliwa na tatizo la matumizi mabaya ya fedha na kibaya zaidi hesabu za chama hicho hazijakaguliwa kwa muda mrefu.

Alisema jumuiiya hiyo hupata kiasi cha Sh80 milioni kutokana na miradi mbalimbali kama jengo lililoko makao makuu ya UVCCM, lakini fedha hizo zinafujwa.

"Ila utashangaa kaka yaani zile fedha zinavyofujwa. Hadi kwa mwezi jumuiya inabakiwa na Sh8 milioni au wakati mwingine hadi Sh6milioni," aliongeza Nchimbi.

source; Bundi atua tena UVCCM - Siasa - mwananchi.co.tz
 
Back
Top Bottom