Mwananchi Huru
JF-Expert Member
- Nov 20, 2021
- 1,448
- 1,003
RAIS SAMIA NI CHUMA CHA PUA DHIDI YA WABADHIRIFU
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha uimara mkubwa katika kuwabana wabadhirifu na wala rushwa na kwamba Chama Cha Mapinduzi kinamuunga mkono katika hilo.
Shaka amesema hayo leo Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, baada ya kupewa nafasi ya kuwasalimia wananchi akiwa katika msafara wa Rais Samia ambaye amemaliza ziara ya siku mbili mkoani humo na kuingia Mkoa wa Kigoma.
”Mikono ya Rais Samia ni mepesi kama pamba katika kumwaga fedha za maendeleo kwa watanzania. Mikono ya Rais Samia ni migumu kama chuma cha pua kwa wabadhirifu na wanaotumia vibaya fedha za maendeleo za Watanzania. Tuendelee kumuunga mkono Rais Samia," amesema Shaka #CCMImara #KaziIendelee