DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Buchosa, Mwanza Tukio la kushangaza linalodaiwa kukiuka taratibu na maadili ya uchaguzi limeibuka katika Jimbo la Buchosa, ambapo mtia nia wa Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Charles Tizeba, anaripotiwa kuwapatia wajumbe wa CCM kiasi cha shilingi elfu ishirini (20,000/=) kwa wajumbe jimbo zima, akidai hawezi kufanywa kitu sababu yeye ametumwa na Rais kuja kugombea na kuwashawishi wamchague katika kura za maoni zitakazofanyika Agosti 2, 2025.
Hata hivyo, wajumbe wa Kata ya Katwe wameibua mshangao kwa kukataa kupokea fedha hizo na kuzirejesha kwa msambazaji, wakidai kuwa hawako tayari kuuza dhamira yao kwa pesa, bali wanahitaji maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Buchosa.
“Hatutaki pesa ya masimango! Tunataka maendeleo ya kweli, na maendeleo hayo tunayayaona kwa Mbunge wetu Eric Shigongo na Diwani wetu Max Mkungu,” alisema mmoja wa wajumbe hao kwa msisitizo.
Wajumbe hao wamesema wanataka kiongozi mwenye dira ya kweli ya maendeleo, si mtu anayetumia fedha kama nyenzo ya kupata uongozi
Juhudi za kumpata Dkt. Charles Tizeba ili atoe ufafanuzi kuhusu tuhuma za kugawa fedha kwa wajumbe zilifanikiwa, ambapo alipokea simu ya mwandishi wetu. Hata hivyo, mara baada ya kusikia swali kuhusu madai hayo, alikata simu ghafla na kui block namba ya mwandishi wetu, hakutaka kuendelea na mahojiano. Jitihada za kumfikia tena hazikufua dafu, kwani hakupokea simu zilizofuata wala kujibu ujumbe wa maandishi aliotumiwa.
Hata hivyo, wajumbe wa Kata ya Katwe wameibua mshangao kwa kukataa kupokea fedha hizo na kuzirejesha kwa msambazaji, wakidai kuwa hawako tayari kuuza dhamira yao kwa pesa, bali wanahitaji maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Buchosa.
“Hatutaki pesa ya masimango! Tunataka maendeleo ya kweli, na maendeleo hayo tunayayaona kwa Mbunge wetu Eric Shigongo na Diwani wetu Max Mkungu,” alisema mmoja wa wajumbe hao kwa msisitizo.
Wajumbe hao wamesema wanataka kiongozi mwenye dira ya kweli ya maendeleo, si mtu anayetumia fedha kama nyenzo ya kupata uongozi
Juhudi za kumpata Dkt. Charles Tizeba ili atoe ufafanuzi kuhusu tuhuma za kugawa fedha kwa wajumbe zilifanikiwa, ambapo alipokea simu ya mwandishi wetu. Hata hivyo, mara baada ya kusikia swali kuhusu madai hayo, alikata simu ghafla na kui block namba ya mwandishi wetu, hakutaka kuendelea na mahojiano. Jitihada za kumfikia tena hazikufua dafu, kwani hakupokea simu zilizofuata wala kujibu ujumbe wa maandishi aliotumiwa.
chanzo: Mwanahabari