KingKimpa
Member
- Feb 5, 2018
- 50
- 60
Habari za Jumamosi njema wana-Jamvi.. Natumai mmeinza salama, na kwa wale walioingia kwenye kuchakarika naomba niwatakie kila la kheri.
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika hapa. Hawa jamaa wanaojiita BrighterMonday nadhani wameishiwa kabisa strategy za kuwafikia wateja wao, and now is nothing but a SCAM. Nina shuhuda kadha wa kadha za ku-support hili.
Kimsingi, niko sokoni natafuta ajira mwezi wa sita sasa baada ya mradi uliokuwa umeniajiri kufungwa (kwa maana ya kukamilika). Hali ya kusaka ajira mpya kila kukicha imenifanya niwe natembelea job boards mbali mbali za ndani na nje ya nchi. Naomba nikiri kuwa ZoomTz ni moja kati ya site mbili za kwanza kuzitembelea kila siku iendayo kwa Mungu, honestly nawapongeza kwa platform ile. Sasa hawa hawa jamaa wa BrighterMonday wana account yao pale ZoomTz na wamekua wakiitumia kutangaza nafasi za kazi zikiwa na referral links kwenda kwenye portal yao (My take, nadhani wanaitumia kuongeza traffics tu kwenye site yao). Kutangaza fursa za ajira ni jambo jema sana, linapaswa kuungwa mkono, lakini kinachokera hawa jamaa wanawaingiza watu chaka, tena idadi kubwa sana ya watu. Nimejaribu kuzifuatilia sana post zako kwa miezi mitatu iliyopita, zimejaa upotoshaji mwingi sana.
Mimi mmoja kati ya watu ambao huwa hawajiridhishi na chanzo kimoja tu cha habari, hivyo huwa naperuzi zaidi. Kwa mfano, NGO na iNGO nyingi zina mifumo yao ya ndani ya kutangaza nafasi za ajira ikiwa na mchakato mzima wa kuajiri (nina uzoefu wa miaka 10 katika hili). Hii inajumuisha masharti na taratibu za kutuma maombi. Hawa BrighterMonday wapo repost hizi adverts wanawaelekeza waombaji kutuma maombi kupitia kwao (ambapo utalazimika kujisajili kwenye mfumo wao pamoja na kupandisha CV yako), kitu ambacho ni upotoshaji mkubwa ukilinganisha na uhalisia toka kwa muajiri. Matangazo mengine yanaelekeza kabisa kuwa "Muajiri hapokei maombi yoyote toka Agency kwa niaba ya Muombaji" lakini bado hawa jamaa wanayaweka tu. Lengo lao ni kukusanya CV za watu na namna zao za mawasiliano na kuanza kuwasumbua kwa emails na text zisizo na msingi wowote, tena bila ridhaa ya wahusika. Wasaka ajira ndio tunakua victims wa hili.
Naamini vibaraka wanaopewa kazi hii na BM watapata taarifa za kwenye uzi huu, Tafadhalini achaneni na upuuzi huu, tafuteni mbinu mbadala. Kuna wakala kibao zinafanya vizuri kwenye tasnia yenu, sio mbaya kuazima mikakati.
WITO WANGU:
ZoomTz ili kuilinda brand na profile yao nadhani wawe na mfumo thabiti wa kuhakiki vyanzo vya matangazo ya kazi kabla hawajayaruhusu kuja hewani. Sio mbaya hata wakiomba vielelezo vya maandishi toka kwa pande zote.
Nawashauri pia BM, waifumue timu yao ya sales and marketing, waajiri watu wanaoweza kuwa wabunifu na kupandisha profile yao ya waajiri (wawape kazi on their behalf) na wasaka ajira (tuwaamini).
Ni hayo tu, Ahsanteni..
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika hapa. Hawa jamaa wanaojiita BrighterMonday nadhani wameishiwa kabisa strategy za kuwafikia wateja wao, and now is nothing but a SCAM. Nina shuhuda kadha wa kadha za ku-support hili.
Kimsingi, niko sokoni natafuta ajira mwezi wa sita sasa baada ya mradi uliokuwa umeniajiri kufungwa (kwa maana ya kukamilika). Hali ya kusaka ajira mpya kila kukicha imenifanya niwe natembelea job boards mbali mbali za ndani na nje ya nchi. Naomba nikiri kuwa ZoomTz ni moja kati ya site mbili za kwanza kuzitembelea kila siku iendayo kwa Mungu, honestly nawapongeza kwa platform ile. Sasa hawa hawa jamaa wa BrighterMonday wana account yao pale ZoomTz na wamekua wakiitumia kutangaza nafasi za kazi zikiwa na referral links kwenda kwenye portal yao (My take, nadhani wanaitumia kuongeza traffics tu kwenye site yao). Kutangaza fursa za ajira ni jambo jema sana, linapaswa kuungwa mkono, lakini kinachokera hawa jamaa wanawaingiza watu chaka, tena idadi kubwa sana ya watu. Nimejaribu kuzifuatilia sana post zako kwa miezi mitatu iliyopita, zimejaa upotoshaji mwingi sana.
Mimi mmoja kati ya watu ambao huwa hawajiridhishi na chanzo kimoja tu cha habari, hivyo huwa naperuzi zaidi. Kwa mfano, NGO na iNGO nyingi zina mifumo yao ya ndani ya kutangaza nafasi za ajira ikiwa na mchakato mzima wa kuajiri (nina uzoefu wa miaka 10 katika hili). Hii inajumuisha masharti na taratibu za kutuma maombi. Hawa BrighterMonday wapo repost hizi adverts wanawaelekeza waombaji kutuma maombi kupitia kwao (ambapo utalazimika kujisajili kwenye mfumo wao pamoja na kupandisha CV yako), kitu ambacho ni upotoshaji mkubwa ukilinganisha na uhalisia toka kwa muajiri. Matangazo mengine yanaelekeza kabisa kuwa "Muajiri hapokei maombi yoyote toka Agency kwa niaba ya Muombaji" lakini bado hawa jamaa wanayaweka tu. Lengo lao ni kukusanya CV za watu na namna zao za mawasiliano na kuanza kuwasumbua kwa emails na text zisizo na msingi wowote, tena bila ridhaa ya wahusika. Wasaka ajira ndio tunakua victims wa hili.
Naamini vibaraka wanaopewa kazi hii na BM watapata taarifa za kwenye uzi huu, Tafadhalini achaneni na upuuzi huu, tafuteni mbinu mbadala. Kuna wakala kibao zinafanya vizuri kwenye tasnia yenu, sio mbaya kuazima mikakati.
WITO WANGU:
ZoomTz ili kuilinda brand na profile yao nadhani wawe na mfumo thabiti wa kuhakiki vyanzo vya matangazo ya kazi kabla hawajayaruhusu kuja hewani. Sio mbaya hata wakiomba vielelezo vya maandishi toka kwa pande zote.
Nawashauri pia BM, waifumue timu yao ya sales and marketing, waajiri watu wanaoweza kuwa wabunifu na kupandisha profile yao ya waajiri (wawape kazi on their behalf) na wasaka ajira (tuwaamini).
Ni hayo tu, Ahsanteni..