Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Hii ni mila imetapakaa haswa nchi za africa magharibi(nigeria,ivory coast,liberia etc).Binti akipevuka,vititi vikianza kuchomoza tu,akina mama watu wazima huchukua jiwe la kusagia nafaka,linapashwa moto,then linakandamizwa katika matiti ya binti.Lengo ni kuua glands za matiti ili kuchelewesha kukua kwa hayo matiti.Lakini lengo kuu ni kuwaepusha mabinti na mafataki waroho wa mabinti wanaochipukia wakiamini kuwa binti mwenye kifua 'flat' hana mvuto kwa wanaume hivyo atakuwa salama.Glands za ukuaji wa matiti hujirudi baadaye sana wakati binti ashakuwa mtu mzima na yuko tayari kuolewa.Huku bongo tunahangaika na tohara ya wanawake,afrika magharibi ndo kama hivyo.