'Brazamen, Bitoz, sista du'

'Brazamen, Bitoz, sista du'

M.E.M.A

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2013
Posts
1,373
Reaction score
472
Wale wenye hizo title hapo juu waliozaliwa miaka ya 1978-84..walikuwa wana sifa za pekee ambazo ukiziona tu unawajua. Yaani zile za kumfanya aonekane mtu 'mjanja'. Mi nitataja baadhi kisha endelezeni.
Wanaume:
1. Kuvaa suruali za 'Tokyo, Van Basten'
2. Kubeba mabegi ya 'Montana'
3. Kutembea na 'walkman'
4. Kuchomeka t shirt au shati kwenye mkanda.
5. Kuvaa raba oversize
6. Kunyoa kwa kuchonga nywele za pembeni tuu.
7. Endeleza...

Wanawake:
1. Kuchoma nywele kwa kifuu/kigae
2. Kuvaa magauni/sketi za ngazi 3 na kuendelea.
3. Endelezeni nimezisahau ghafla nyingine.
 
ni kweli VIP zilikuwa zinakatika kale kauzi pale kati.kuna jamaa yangu tunacheza mpira alikuwa winga matata yupo kifua wazi ikatiwa ndefu kakimbia watu wanasangilia akadhani ni uhodari wake wa mbio,loh kumbe VIP imegeuka SIDIRIA.
 
ni kweli VIP zilikuwa zinakatika kale kauzi pale kati.kuna jamaa yangu tunacheza mpira alikuwa winga matata yupo kifua wazi ikatiwa ndefu kakimbia watu wanasangilia akadhani ni uhodari wake wa mbio,loh kumbe VIP imegeuka SIDIRIA.

Najaribu kupata picha..hahaha. Eti sidiria..lol
 
Wanaume kuvaa jeans za 24HRS na 48HRS na t shirt za FUBU

Na zile jeans za Tagara zenye viraka viraka...
 
kuvaa suruali za chuichui, gabs
kuvaa sweta kaba shingo
maviatu makubwa
kutembea kwa kudunda
 
suruali michael jackson au zico,kuna viatu vya kina dada vya mpira vina matundu mengi,tuliviita saa nane utanikoma.
 
Kuvaa raba za rojamila, maradona, ziko na DH na kaunda za mchelemchele. Wadada walikua nacraba flani nyeusi zina shingo kidogo zinaitwa Loso, basi nikiwa std 4 nikaiba za sister nikaenda kuchezea mpira. Kwa kuwa ni kijijini na almost watoto wote mnacheza peku, nilikamua sana siku hiyo tukashinda 5-2 na mi nilifunga matatu. Sasa kw kuwa raba zilikuwa laini sana na watoto wa kijiji wako sugu zilichanika vibaya mno. Kilichonikuta huko home sina hamu ya kusimulia leo aisee
 
Ayaa nimesahau yale mashati ya bawama. Nyuma yanakuwa na rangi moja sanasana nyeusi afu mbele yanakuwa ya maua ya rangi mchanganyiko...
 
Mi naona hawa watoto wa siku hizi kupata div 5 na div 4 za point 40 kuna mambo mengi yanachangia. Kwa mfano hata michezo ya watoto ya asili imepungua sana ukikompea na sisi wa enzi hizo. Mambo ya kombolela, mdako, nage, kuwinda kw manati. Kuendesha ma-ringi, baiskeli za miti, nyumba za udongo, magari ya mabati na maboksi n.k. vyote hivi vilikuwa brain activators. sasa siku hizi ni tamthiliya, bongo movie, play station n.k. eti kuna hadi tuition za chekechea. Nadhan I consider myself privillaged to be born by that time...
 
Mnazikumbuka suruali za ngozi feki zilikuwa zinaitwa EVA GITANO na raba za SUPERGA?
 
Back
Top Bottom